google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 14, 2015

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo.

No comments :
Je, huwa unaingia kwenye msongo wa mawazo haraka au kirahisi? Kama jibu ni ndiyo, kwa nini usijiulize ni kwa vipi unaingia kwenye kusongeka? Kitu ninachoamini kwa kujiuliza ni kwa nini mtu anasongeka, kunakuwa kuna mengi ya kujifunza, lakini wakati mwingine, mengi ya kushangaza pia.

Kusongeka humfanya mtu kuona kwamba, kila kitu kinakwenda hovyo, kila kitu kiko shaghalaghabala, kila kitu kiko hovyo. Wanaoingia kwenye kusongeka kiakili hujiambia siku zote kwamba, kila kitu hakina maana, yakiwemo maisha yao pia.

Je, kitu cha kujiuliza hapa kama itatokea nikaingia kwenye kusongeka kiakili nitakuwa nazungumza vipi, yaani kwa sauti namna gani? Bila shaka nitakuwa nazungumza kwa sauti ya chini na pia ya kuburuza. Siyo kuzungumza tu, bali hata kusimama au kutembea kwangu kutakuwa ni kwa kujiinamia na kuona kila kitu kwangu kimeharibika.

Hivi ndivyo wengi wanavyojiona wanapokuwa wamesongeka kimawazo, ingawa kuna wakati mwingine huweza hata kuonyesha nyuso za huzuni na simanzi, hiyo yote huweza kutusaidia sisi kubaini na kutambua wazi kinachoendelea kwenye akili zao kuwa wana mawazo mengi au kusongeka sana ndiko kunakowasumbua.



Kama upo kwenye kusongeka na unaendeleza mawazo hayohayo kila mara ambayo yanakupekea wewe kusongeka hiyo inakuwa sawa na wewe kuamua kujichanganya kwenye maisha yako. Na unapoamua kujichanganya mwenyewe kwenye maisha yako, tambua kabisa hakuna utakachoweza kufanikisha, zaidi ya kuharibu maisha yako tu.

Ni vizuri kwako kujua kuwa unaouwezo wa kuweza kubadili kusongeka kwako kimawazo na kuishi huru kabisa. Najua inaweza ikawa kwako sio rahisi kuelewa, lakini ninachotaka kukwambia kuwa unaweza kuondokana na kusongeka kwako, ikiwa tu utaweza kubadili namna ya kuyatazama mambo au matukio katika maisha yako.

Ni kweli kwamba, kusongeka kiakili husababishwa na mambo mbalimbali, lakini sisi huweza kufanya kusongeka huko kushika mizizi kwa namna tunavyokaa, kusimama au hata kwa namna yetu tunavyofikiri na kutafsiri mambo. Tunapokaa au kufikiri kwa namna ya kinyonge, tunafanya mawazo yanayotupitia kuwa ya kinyonge pia.

Kwa kuhakikisha hili zaidi, hebu jaribu kumuuliza au kumchunguza mtu anayetembea huku akiwa ameinama na Yule anayejiinamia kama atakwambia kuwa anafikiria mambo mazuri. Ni wazi kabisa mtu kama huyu ni lazima atakuwa anafikiria mambo mabaya yanayopelekea kusongeka kwake kimawazo.

Kufikiri kwetu kukiwa nako ni kule kunakotutia hofu, mashaka na kutuingiza kwenye kijicho, ni lazima tutajikuta tukianza kusimama au kutembea kwa njia yenye kuonesha kukata tamaa, wanyonge na hata tusiojiweza. Kwa nini tusibadili mambo hayo ili tuweze kuondoka kwenye huzuni kali au kusongeka? Kwa kujiambia mambo yenye kutia huzuni na simanzi tunajiingiza kwenye huzuni bila kujua.

Lakini kumbuka kuwa kwa kujiambia mambo mazuri na yenye kutia moyo ndivyo tunajikuta ambavyo tunaingia mahali ambapo tunayaona au kuyatazama maisha katika mwanga mkubwa zaidi. Na hivi ndivyo tunavyoweza kuondokana na msongo wa mawazo kwa kujiambia mambo mazuri kila mara katika maisha yetu na si vinginevyo.

Kwa kuwa tunaweza kufikiri kwa namna isiyoumiza, tunaweza kwa hali hiyo kujitoa kwenye kusongeka. Kuna wakati mtu mwenye msongo wa mawazo anahitaji tabasamu tu au kujiambia kimoyomoyo kwamba, kila kitu kiko sahihi na kinakwenda kama kilivyotarajiwa. Halafu, ni kweli, ataanza kuhisi tofauti, kuhisi ukamilifu na uwezo zaidi katika maisha yake na kuondokana na kusongeka ambako kunaweza kuwa kunamtesa.

Ninaomba nikutakie mafanikio mema, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza zaidi.

MAKALA HII IMEANDIKWA NA DEVOTA KAUKI WA MANYONI, SINGIDA.

Kama una maoni au ushauri unaweza kuwasiliana na mwandishi wa makala hii kwa email truesuccess89@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.