google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 27, 2015

Kama Unataka Mafanikio Makubwa, Hakikisha Unabadili Kitu Hiki Haraka Sana.

No comments :
Habari za leo mpenzi msomaji wa DIRA YA MAFANIKIO, nimatumaini yangu ya kuwa umzima na unaendelea vyema katika shughuli nzima ya kuboresha maisha yako. Kama nilivyosema katika makala iliyopita kuwa katika makala ya leo tutajifunza juu ya kubadili fikra zetu ili kuweza kufikia mafanikio makubwa.
 
Ikumbukwe kuwa fikra ni kitu cha muhimu sana kutuwezesha kufikia mafanikio makubwa tuliyojiwekea. Bila kuwa na fikra sahihi ni vigumu sana kuweza kufikia mafanikio yoyote yale. Hivyo, hiyo inatuhakikishia kuwa kama kweli unataka mafanikio makubwa, kitu cha kwanza unachotakiwa kukibadili kwa haraka ni fikra zako. 

Kumbuka,kufikiri ni kufikiri, wengi ndivyo tunavyamini. Huwa tunachukulia kufikiri kwetu kama jambo ambalo halituhusu kabisa. Inawezekana kabisa hapo ulipo ulishasahau kwamba huwa unafikiri  hadi hivi sasa unaposoma kuhusu kufikiri.
Ni ajabu sana kwa sababu, huku kufikiri ndiko kunakokufanya tuhisi au kutenda kwa namna hii au ile maishani. Kila tunachofanya na mengi kama siyo yote kati ya yale yanayotutokea kwenye maisha yetu yanatokana na kufikiri kwetu.


Katika kutafuta kufanikiwa ni lazima kufikiri kwetu kuwe katika mkabala wa kufanikiwa kwanza. Kama kufikiri kwetu kuko katika mkabala wa kushindwa, tunakuwa sawa na mtu anayeomba watu wasukume gari lake kwenda mbele huku akiwa tayari amewaomba wengine kulisukuma gari hilo kurudi nyuma.


Kama binadamu, tunatofautiana katika mambo yanayoenda vichwani mwetu na mambo hayo ni mengi sana. Wataalamu wamethibitisha kwamba, kwa kutwa moja binadamu anapitiwa na mawazo zaidi ya elfu hamsini. Lakini jambo ambalo hatutofautiani ni ukweli kwamba, kufikiri kwetu huko kwa namna-kufikiri kuzuri na kufikiri kubaya.

Singependa kuzungumzia kufikiri vizuri na kufikiri vibaya kwa sababu, inahitaji maelezo mengi na hata hivyo, haitasaidia sana katika muktadha huu. Bali ninachoweza kusema ni kwamba, kufikiri vizuri ni ile hali ya kuingiza fikani mwetu yale mambo ambayo hayatuumizi kihisia, kiroho na kimwili, wala kuwaumiza wengine kwa njia hiyo.

Kufikiri vizuri ni kuingiza fikirani mwetu yale tu ambayo tunaamini kwamba yatatupa moyo, kutuongezea matumaini na kutujengea uhusiano mzuri na wengine. Yale tu ambayo ndiyo tunayotaka , tunayoyatamani na kupenda yatokee maishani mwetu.


Kufikiri vibaya, kwa kifupi naweza kusema kuwa ni kufanya kinyume na kufikiri vizuri. Pale ambapo kile tunachokiruhusu kuingia fikrani mwetu ni chenye kutuumiza kihisia, kiroho na kimwili au kuwaumiza wenzetu kwa njia hiyohiyo, ndipo tunapaswa kujua kwamba, tunafikiri vibaya. Kufikiri vibaya ni kuingiza mawazoni mwetu yale tusiyoyataka au kuyatamani ama kuyapenda.

Unachopaswa kufanya kama kweli unataka mafanikio maishani mwako ni kujiuliza kuhusu mfumo wako wa kufikiri . je, mawazo yako mara nyingi yanabeba mambo gani? 

Inawezekana kabisa huwa unaamini kwamba wewe ni dhaifu, wewe huwezi kupata cheo, wewe huwezi biashara fulani kama wengine au wewe ni msindikizaji tu. Kama unajiita ‘mlalahoi’ hujitendei haki. Kama unajiita ‘dhaifu’hujitendei haki. Kama unajiita mnyonge hujitendei haki. Kama unajiambia una mkosi ndiyo kabisa na kama unajilaumu kila wakati, tambua kwamba unajifuja kupita kiasi.

Kama unafikiri vibaya inabidi ubadilike na kuanza kufikiri vizuri, yaani kuingiza fikrani mwako yale tu ambayo yatakusaidia katika kufika kule unakotaka bila kujiumiza au kuwaumiza wengine. Kuingiza ffikrani mwako yale tu unayotaka  au kuyatamani, na siyo kuingiza yale usiyoyataka.

Kwamba unaweza kufanya au kupata kile unachokitaka maishani ni jambo lililowazi kabisa, bila kujali kama umesoma au hukusoma, un rangi nyeusi au nyeupe, unatoka kwenye familia maskini au ya kitajiri, unasali au husali. Sifa au vigezo vya kupata kile unachokitaka vinafahamika, lakini kama nilivyosema sifa ya kwanza ni kufikiri.

Wale wote waliofanikiwa, ukiwauliza watakwambia kwamba waliamini kuwa watafanikiwa walifanya juhudi wakijua kuwa iko siku. Kuna wakati rais wa zamani wa marekani Abraham Lincolin( Alikuwa rais mwaka 1860) ambaye alianguka na kushindwa zaidi ya mara ishirini katika mambo mbalimbali ikiwemo katika uchaguzi, kufilisika biashara na hadi kuchaganyikiwa. Lakini aliendelea bila kusema , ‘ninamkosi’ au ‘siwezi’ hadi akaja kuwa kiongozi maarufu duniani.


Kwenye kitabu chake cha Unlimited power, Anthony Robbins anamzungumzia mtu ambaye alipata ajali ya barabarani akaumia sana kiasi ch akuharibika kabisa mwili. Mtu huyu alikuja tena akapata ajali yaa ngege ambapo alipooza kuanzia kiunoni kwenda chini. Bila kujali ulemevu na uharibifu wa sura na mwili, mtu huyu alisema, ‘ninawea na nitafanya’. Aliweza na kuwa miongoni mwa mamilionea wa marekani. Kwa wenzetu wengi, kwa ulemavu wa aina hiyo hunyoosha miguu na kuanza kuomba wakiamini hawawezi tena.

Anthony Robbins mwenyewe hakusoma zaidi ya elimu ya kidato cha sita, lakini kwa kuamini kwamba, inawezekana mtu anapoamua, alifanya maajabu. Kwa kiwango chake hicho cha elimu aliweza kwa muda mfupi tu, kutoka katika hali ya uhohehahe wa kuishi chumba kimoja chenye mende, hadi kuaminika katika kuwafundisha watu kuhusu maisha wakiwemo viongozi wan Nchi.

Sasa hivi Robbins ni bilionea na hakuiba  wala kutumia ujanjaujanja, bali kanuni za kimaumbile katika kujenga uwezo wa binadamu. Kama angeamini kuwa, kwa sababu hakusoma sana asingeweza, ni wazi asingeweza, lakini wa sababu hakujiwekea vizingiti amemudu.

Uwezo wa mawazo yetu unaonekana vizuri kwa mtu na wazi kwa zaidi kwa mtu aitwaye Stephen Hawking, ambaye ni miongoni mwa wanasayansi bora ambao karne iliyopita na karne hii zimeweza kumshuhudia. Kwa nini mtu huyu ni mfano bora wa namna mawazo yalivyo na nguvu?

Akiwa na umri wa miaka 13 aliugua maradhi yanayofahamika kama amyotrophic lateral screrosis u lo gehrig’s, hali ambayo hulemaza mwili. Hawking alilemaa mwili mzima isipokuwa shingo, kichwa na mkono wake wa kushoto. Pia alikuwa hana uwezo wa kuzungumza.

Akiwa kwenye hali hiyo, aliweza kufanya maajabu kwenye eneo la fizikia na kutoa nadharia nyingi ambazo zimesaidia kuibadili dunia katika maeneo mbalimbali. Kwa kuamini kwamba anaweza, kupania na kujua anataka nini, ameshangaza wengi. Kwa sababu bado yu hai, atashangaza wengi zaidi. 

Ukiweza kuyabadili mawazo yako, yanauwezo wa kukupa mafanikio makubwa ukiamua. Kitu unachotakiwa ni kuacha kabisa kujidharau na kujishusha, utafanikiwa.

TUPO PAMOJA KATIKA SAFARI YAKO YA MAFANIKIO,

IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.