google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 24, 2015

Hatua Muhimu Zitakazokuongoza Kufanya Maamuzi Yatakayokupa Mafanikio Makubwa.

No comments :
Ni kitu ambacho kinawezekana kabisa katika maisha yako kuwa unaouwezo mkubwa wa kuwa na maisha yenye mafanikio kama unavyotaka iwe kwako. Ili uweze kufikia mafanikio hayo unayoyataka kwako ni lazima ujifunze kutumia uwezo mkubwa ulionao kuchunguza maamuzi unayoyafanya kila siku juu ya maisha yako. Maamuzi unayofanya, ndio msingi mkuu wa mabadiliko ya maisha yako.

Mara nyingi maamuzi unayofanya kila siku juu ya maisha yako ndiyo yanayotabiri au kukupa picha kamili ya maisha yako yanaekea wapi. Kama unafanya maamuzi mabovu kila wakati na kila mara uwe na uhakika maisha yako ni lazima yatakuwa sio mazuri. Kwa kulijua hilo ni muhimu sana kwako kuwa makini na maamuzi unayofanya kila siku ili uweze kuboresha maisha yako zaidi.

Ni kweli kwamba kuna wakati inaweza ikawa ni ngumu kwako kufanya maamuzi yatakayokupa mafanikio makubwa katika maisha yako, yote hiyo ni kwa sababu pengine ya kutaka kuona matokeo ya haraka zaidi. Kama umeamua kuwekeza ni muhimu sana kwako ukawa mvumilivu na kujipa muda ili kuweza kupata matokeo ya kile unachokitaka. Ukifanya hivyo, ule ugumu wa maamuzi unaouona hautakuwa shida kwako.


Kwa haraka haraka mpaka hapo unaona kuwa maamuzi ni kitu cha msingi sana katika maisha yako kuliko unavyofikiri.  Unapokesea kufanya maamuzi hata kama ni madogo vipi, ndivyo unavyozidi kubomoa maisha yako hata kama hujui. Hivyo basi, ni muhimu kwako kuwa na maamuzi mazuri na sahihi kila siku yatakayoweza kubadili maisha yako na kuwa ya mafanikio makubwa.

Unapokuwa na maamuzi haya sahihi, hii itakusaidia wewe kukuwezesha kustawisha uwezo wako  wa kuchagua maisha yanayofaa kila siku. Katika makala hii ya leo utaweza kujifunza hatua muhimu unazotakiwa kuzichukua katika maamuzi yako ili kuweza kuishi maisha ya mafanikio. Je, unajua ni hatua zipi zitakazokuongoza kuchagua kuishi maisha ya mafanikio?

Hizi Ndizo Hatua Muhimu Zitakazokuongoza Kufanya Maamuzi Yatakayokupa Mafanikio Makubwa.

1. Fikiria matokeo ya maamuzi yako.
Kabla ya kufanya uamuzi wowote ule katika maisha yako, fikiria kwa makini matokeo ya uamuzi wako huo. Ukichunguza matokeo ya uamuzi wa unaotaka kuuchukua hiyo itakusaidia kuwa makini sana na uamuzi wowote unaouchukua kwenye maisha yako. Kwani utakuwa umejua uamuzi huu unaweza kuboresha ama kubomoa maisha yangu kwa kiasi gani.

Pia kabla hujafanya uamuzi wowote ule jiulize hivi, uamuzi wangu huu utakuwa na matokeo gani katika maisha yangu baada ya mwaka mmoja, miaka miwili au hata miaka kumi ijayo. Kama uamuzi huo unaouchukua utaona unaharibu maisha yako kwa sehemu kubwa, ni bora ukaachana nao na ukafanya uamuzi tofauti utakao boresha maisha yako.



2. Chunguza kwa makini maamuzi unayohitaji kufanya.
Ni muhimu sana kuchunguza maamuzi unayotaka kufanya na sio tu kujifanyia maamuzi ambayo wakati mwingine hayawezi kukusaidia zaidi ya kukugharimu. Wengi wetu huwa ni watu wa kuiga maamuzi ya wengine kitu ambacho huweza kuathiri maisha yako moja kwa moja. Ni muhimu kujichunguza maamuzi unayotaka kuyafanya mara kwa mara.

Kwa mfano kama unataka kuwa na maisha mazuri ni lazima kwako kujiliza na kujichunguza ni kipi  ukifanye ambacho kitaweza kukupa hayo maisha unayoyatamani. Haitawezekana kwako kufikia maisha hayo kama tu utakuwa bado mtu wa kuishi maisha yaleyale ya kuendekeza marafiki wa uzembe ama kuendekeza matumizi ya hovyo. Ukiweza kujichunguza kwanza maamuzi unayoyafanya yatakusaidia kusonga mbele.

Kwa kumalizia makala hii, tambua kuwa hizo ndizo hatua muhimu ambazo zinaweza kukuongoza kufanya maamuzi ambayo yatakupa maisha ya mafanikio kwako na sio tu kujifanyia maamuzi ambayo hayawezi kukusaidia. Kumbuka kabla hujafanya maamuzi yoyote ni muhimu kufikiria matokeo ya maamuzi yako na kujichunguza kwa makini maamuzi unayoyataka kufanya yatakusaidia vipi kuboresha maisha yako.

Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio na endelea kuwashirikisha wengine kujifunza kupitia mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO ili kuboresha maisha yetu.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE.

IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.