google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 12, 2015

Iheshimu Leo Isije Kukugharimu Kesho.

No comments :
Hivi umewahi kufanya kitu fulani halafu miaka ikapita ukajiuliza kama ni wewe umefanya hilo jambo, mimi nimewahi. Kuna wakati katika maisha unaweza ukajikuta umefanya jambo fulani halafu baadaye ukaja kujuta, ukajiona ni mjinga au hata limbukeni. Wakati mwingine linaweza likawa fundisho kwako kiasi cha kwamba hata mtu akushawishi vipi huwezi kurudi kufanya jambo hilo tena.

Hata hivyo tikirudi nyuma huenda wakati unafanya hayo mambo ulikuwa unashauriwa, hivyo ukajikuta ukawa sikio la kufa lisilosikia dawa. Au huenda hukupata nafasi ya mtu kukwambia unachofanya siyo na kwamba kitakuja kukugharimu maishani. Tuachane na sisi ambao tumepitia huko, tukajifunza na tukamwomba Mungu hiyo historia isije kujirudia tena katika maisha yetu.

Leo, naongea na wale wenzangu na mimi ambao tunaingalia leo. Kesho ni kama hatuijui vile au kama haitakuwapo kutokana na mambo tunayoyafanya. Wengine husema ‘kesho itajijua’. Kama ingekuwa hivyo basi tusingekuwa tunaihangaikia kesho.

Inafahamika wazi kuwa kila mtu ana uhuru wa kufanya kile anachokisikia, lakini ukweli unabaki palepale kwamba hata uhuru wa mtu binafsi una mipaka yake. Huwezi kufanya kila kitu bila kuzingatia mambo muhimu hasa ya kimaadili. 


Unajua kwa sisi vijana kuna mambo mengi tunayafanya kwa sababu ndio wakati wake, ujana si maji ya moto bwana. Ni kweli wala siyo uongo lakini wengi wetu tunafanya kwa kufuata mkumbo. Kuiga sijui fulani kafanya hivi na mimi nifanye, mwingine kaenda huku na wewe huyo kama kumbikumbi vile. Sasa unavyofanya hivyo unajua mwenzako kwa nini anafanya?

Wengi hasa wasichana wanaona fahari kumuiga fulani kafanya hivi ama vile. Kapate kile yeye atafanya kile akiwezacho hata kama kitamgharimu maisha yake lakini bora tu awe kama fulani. Kumbuka kuna kesho katika maisha yako, Yule unayemuiga hufahamu alivyojipanga hadi akafanya yale unayoyaona. Mambo mengine ni siri ya mtu. Sasa wewe unaingia kichwa kichwa utaumia.

Mwingine anaweza kuona rafiki yake, kachora tattoo na yeye huyo. Hivi unafahamu kwamba unaweza kukatisha ndoto za kuwa na mafanikio kuliko uliyonayo kwa sababu ya kufuata mkumbo? Kuna vitu tunaweza kuviona ni vya kawaida lakini kuna watu hadi leo wakikumbuka jinsi vilivyowagharimu katika maisha yao inakuwa inauma. Kuwa mtu na msimamo wako, maisha yako ni yako. Mwisho wa siku utakuja kusimama wewe kama wewe kwenye mambo yako ya msingi.

Nakumbuka kuna jamaa mmoja alipata nafasi ya kazi serikalini lakini alikuwa amechora tattoo. Kila siku akawa mtu wa kuvaa mashati yenye mikono mirefu, hata kukiwa na joto la aina gani hata mikono hawezi kukunja.

Alipoona watu wanamuuliza sana na kuna baadhi ya watu walianza kuhisi kwamba kuna kitu anaficha, alilazimika kwenda india kufanyiwa upasuaji. Huko alichomwa sindano ile ngozi ya juu iliyokuwa imechorwa ikaamuka halafu ikakatwa. Baada ya hapo aliuguza kidonda na kurejea akiwa na kovu. Hadi leo anakovu kwenye mikono. Sasa shida zote za nini? Iheshimu leo, isije ikakugharimu kesho.

NAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YAKO YA MAFANIKIO, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kupata elimu na maarifa bora yatakayoboresha maisha yako.
  •      Makala hii imeandikwa na Suzan mwillo wa Gazeti La Mwananchi.
  •                Mawasiliano suzanmwillo@yahoo.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.