google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 21, 2015

Sifa 15 Ambazo Matajiri Wa Kweli Huwa Nazo.

No comments :
Ni ukweli uliowazi kwamba ili uweze kuwa tajiri wa kweli katika maisha yako huwa kuna sifa zake muhimu ambazo zinamfanya tajiri huyu wa kweli aweze kutofautiana na tajiri Yule ambaye anaweza kuwa ametumia njia za mkato ama ujanjaujanja fulani ambao huweza hata kuwaumiza wengine kihisia au kimwili ilimradi tu kuweza kufikia utajiri huo anaoutaka. Sifa hizi ndizo huwa zinaleta upekee na kuwafanya matajiri wa kweli kuwa muhimu sana duniani.

Sifa za matajiri wa kweli ambazo tunazizungumzia katika makala hii, ni za wale matajiri  ambao wameamua kupigania maisha yao kutoka chini kabisa mpaka kufanikiwa, ni wale ambao wameamua kutumia nguvu ya kuamua na kuvikabili  vikwazo mpaka kufanikiwa. Swali ambalo unaweza ukawa umeshaanza kujiuliza ni sifa zipi ambazo matajiri wa kweli huwa nazo, ambazo hata wewe unaweza kuzitumia katika maisha yako na kukuwezesha kuwa tajiri?

Hizi Ndizo Sifa Ambazo Matajiri Wa Kweli Huwa Nazo.

1. Wamenuia.
Watu wenye mafanikio wanakuwa wamenuia kufanikiwa. Wanachapa kazi na kila mara wanajifunza mambo mapya. Wanafanya kila jambo ambalo litawawezesha angalau kufanikisha ndoto zao. Ndani ya nafsi zao wanakuwa na shauku kubwa ya kufanikiwa hali ambayo inapelekea wafanye kila linalowezekana hadi waweze kufanikisha hizo ndoto zao.



2. Wamedhamiria.
Ukiwa una dhamira kubwa, utasababisha mambo yako mengi, kusonga mbele. Watu wenye mafanikio huwa wepesi sana kujua mambo gani ni ya kuyafatilia na mambo gani ya kuyapuuza. Kwa mambo waliyodhamiria huamua kufanya kazi kwa nguvu kubwa hadi kufanikiwa katika malengo yao.


3. Hujitoa mhanga
Mara nyingi watu wenye mafanikio hujitoa mhanga lakini zaidi zaidi ni majasiri . Wako tayari kuwekeza na kufanya maamuzi yanayoonekana  kuwa ya HATARI kwa watu wa kawaida. Katika suala zima la kujitoa mhanga huwa hawaogopi kitu na hawajali nani atasema nini? Wanachoangalia ni matokeo ya mbele yatakayowasaidia.

4. Hawakati tamaa.
Hawana msamiati wa “kukata tamaa” kwenye kufikiri zao na hata kuzungumza kwao au hata kwenye hisia zao. Hakuna kitu kama hicho kwenye ubongo wa mtu mpenda mafanikio. Wanaendelea kusonga mbele hata kukiwa na vikwazo lukuki. Wanachojua ni kufanya kazi mpaka kuweza kutimiza kile wanachokihitaji katika maisha yao.

5.Wabunifu.
Kila mtu anapenda kufanya maamuzi ya ubunifu katika maisha yake kwa kiasi fulani. Lakini watu wenye mafanikio wamegundua kwamba kuzama kwenye mafanikio huku ukiwa ndani mwako una ubunifu ni kitu muhimu sana katika kupata mafanikio unayoyahitaji. Kwa hiyo watu wote wenye mafanikio, wamezama sana kwenye ubunifu ili kupata matokeo wanayoyataka.

6. Ni wenye ndoto.
Ili kuweza kuishi maisha yenye maana, binadamu hana budi kuishi maisha yenye ndoto katika mipango na malengo muhimu aliyojiwekea. Watu wengi wenye mafanikio, kwa kawaida wanakuwa wametumia muda mwingi wakifikiria ni aina gani ya ndoto waitimize katika maisha yao. Wanapokuwa wameipata huweza kuifanyia kazi kwa nguvu zote mpaka kuweza kufanikiwa kwa kile hasa ambacho wanakuwa wamelenga katika maisha yao.


7. Hupenda kujifunza.
Wat wenye mafanikio mara nyingi huwa wana sifa ambayo huwa ni ya pekee ambayo huwa inawatofautisha kabisa na watu ambao hawana mafanikio. Sifa hii muhimu ambayo huweza kuwa nayo ni sifa ya kupenda kujisomea. Watu wenye mafanikio mara nyingi huwa ni watu wa kujifunza siku zote na huwa hawaachi. Kutokana na kujifunza huku kupitia vitabu na semina mbalimbali hujikuta wana maarifa mengi sana ambayo huweza kuwasaidia na kuwafanikisha kwa kiasi kikubwa kusonga mbele.

8. Wana uwezo wa kubadilika.
Watu wapenda mafanikio huenda kufuatana na upepo. Kuwa king’ang’azi, bila kusoma hali za nyakati za upepo na maisha yanaendaje kwa wakati huo kuna wakati kunaweza kukupeleka kuzimu. Watu wenye mafanikio wanaweza kubadili mwelekeo muda wowote ule hata bila kutarajia, hii ni moja ya sifa muhimu ambayo hata wewe unatakiwa uwe nayo.

9. Hawaogopi kutoa maamuzi.
Wahenga walisema, uwe mwepesi kutoa maamuzi na nenda polepole katika kubadili maamuzi. Watu wenye mafanikio ndivyo walivyo. Wanafanya maamuzi ya haraka na kuangalia mbele zaidi katika maisha. Kuwa mtu wa kigugumizi sana huweza kupunguza nguvu ama mwendo wa kuelekea kwenye mafanikio yako.

10. Watulivu.
Ni ukweli usiopingika mafanikio huchukua muda kuweza kuyajenga. Matajiri huwa sio watu wa kupenda mafanikio ya haraka kama unavyofikiri bali huwa ni watu wa kujiwekea mipango na malengo hadi kufanikisha kile wanachokihitaji. Huwa ni watu ambao sio wa kulazimisha mambo katika maeneo ambayo hayawezekani hasa katika njia  za mkato huwa hawaamini hilo. Huwa ni watu wa subira kuhakikisha mambo yanaenda katika uhalisia wake.

11. Wanajifahamu.
Ili kuwa mtu mwenye mafanikio huna budi kujijua uwezo wako ulionao na hata mapungufu uliyonayo ili kama ni kujirekebisha uweze kujirekebisha na kuweza kusonga mbele. Watu wenye mafanikio mara nyingi hujijua undani mwao, wanataka nini na kitu hicho wakitakacho watakipataje. Wanajua viwango vyao na hawavipunguzi zaidi ya kuviboresha.

12. Wawazi.
Watu wenye mafanikio mara nyingi huwa wawazi katika mambo yao. Kile wanachoongea ndio huwa wanamaanisha na sio tofauti na hapo. Huwa hawaoko tayari kuuma maneno, kama jambo haliwezekani watakwambia haliwezekani tu. Lakini zaidi ya hapo watu hawa huwa wako tayari kupokea habari zozote ambazo zinaweza kusababisha kufanikisha ndoto zao zifanikiwe bila kinyongo.

13. Ni watu wa kawaida.
Watu matajiri ni watu wenye furaha sana katika maisha yao na huwa hawana makuu hata kidogo. Huwa ni watu ambao wapo karibu sana na familia zao na kupata muda wa kuburudika. Ni watu ambao unaweza kupishana nao mara kwa mara kadhaa kutwa usijue kwamba wanauwezo mkubwa ndani mwao. Ni watu wanaojua kujichanganya kirahisi na hawauoni utajiri wao kama kitu cha ajabu sana, hivyo hujikuta ni watu wa kujali sana wengine.

14. Watu wa kiroho.
Hawa mara nyingi huwa ni watu wenye mambo ya kiroho. Wanaamini kwamba maisha yao sio tu maumbile ya nje bali hata mambo ya ndani mwao. Wanaamini kuongozwa na roho. Kumbuka sizungumzii dini hapa, bali nazungumza maisha yaliyo juu ya uhitaji na utashi wa mwili, hisia na akili.

15. Ni watu pia wa kuburudika.
Kuishi maisha mazuri haina maana kuwa kwamba ni kazi..kazi..kazi.. haina maana hiyo hata kidogo. Matajiri wa kweli na wenye furaha mioyoni mwao huwa ni watu wenye furaha na ni watu wanaopata muda wa kupumzika, wakifurahia upande wa pili wa maisha yao.

Kwa kuishi maisha ya kuwa na sifa muhimu ambazo matajiri wa kweli wanazo ni njia bora kabisa itakayokufikisha kwenye mafanikio ya kweli ambayo dunia inayahitaji. Hizo ndizo sifa ambazo matajri wa kweli huwa nazo na kuweza kuzitumia katika maisha yao ya kila siku.

Kwa pamoja tunaweza kuyafikia mafanikio makubwa tuyoyahitaji katika maisha yetu, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa elimu na maaarifa bora yatakayoboresha maisha yako.

NAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YAKO YA MAFANIKIO.

IMANI NGWANGWALU,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.