google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 28, 2015

Hii Ndiyo Sababu Inayowafanya wengi Wawe Na Kisirani Asubuhi.

No comments :
Mara nyingi imeshawahi kukutokea wewe binafsi ama kuona kwa watu wengine mara wanapoamka asubuhi huwa ni watu wa kisirani sana tofauti na muda mwingine. Umeshawahi kujiuliza nini chanzo au sababu yake hasa? Kwa nini asubuhi mtu anapotoka usingizini, kisirani kinaweza kuzuka kirahisi zaidi kuliko wakati mwingine? Huenda jibu hulifahamu. Lakini, wataalamu wasiolala, wakichunguza matukio ya kila siku ya maisha ya binadamu wana majibu.

Kwa kawaida, mtu anapokuwa ameamka kutoka usingizini, akili yake inakuwa ina mawenge na kushindwa kufikiri vizuri. Inahitaji muda kidogo, ili mtu ambaye ametoka usingizini karibuni, kuweza kumudu kufikiri vizuri kwa utaratibu ule wa kawaida. Inaelezwa kwamba, uwezo wa kufanya uamuzi wa hekima unajengwa baada ya mtu aliyetoka usingizini, kupata muda wa kutafakari kwanza.

Kama mtu anatakiwa kufanya uamuzi wa haraka, mara baada ya kushtuka au kuamka kutoka usingizini, inaweza kumwia vigumu sana. Mara nyingi, akili ya mtu ambaye ndiyo ametoka usingizini muda huohuo, inakuwa na aina ya ukungu unaomzuia kufikiri vizuri na kwa haraka.

Inaelezwa kwamba, akili ya mtu ambaye ndio kwanza ametoka usingizini, inakuwa na ukungu kuliko ile ya mtu aliyekosa usingizi kwa saa 26. Hii inakuonesha ni kwa kiwango gani, mtu anapotoka usingizini, anakuwa na hali mbaya katika kufikiri.


Hata hivyo, wataalamu walioshughulikia kujua ukweli unaohusiana na kisirani cha asubuhi kwamba, huchukua kiasi cha dakika kumi hadi ukungu kuondoka akilini, ambapo mtu anaweza kuanza kufikiri vizuri. Lakini hata hivyo, imebainika kwamba, kwa watu wengine huchukua hadi saa mbili tangu kuamka, kabla ukungu wa akili haujatoka.

Utafiti huo bado unaendelea katika kutaka kujua muda hasa ambao akili inachukua kujirudisha katika hali ya kawaida baada ya mtu kuamka. Lakini pia kuangalia athari za watu kama madaktari ambao huamshwa usingizini kwenda kufanya uamuzi mkubwa unaohusu maisha ya mtu. Je, hali hii haiwezi kuwafanya madaktari kufanya makosa ya wazi yanayoweza kusababisha maafa kwa wagonjwa?

Ni juu yako sasa kujua namna ya kuwasiliana na mtu ambaye ndiyo kwanza ametoka usingizini. Kama kuna jambo linaweza kusubiri angalau kwa dakika ishirini baada ya mtu kuamka, ndiyo likasemwa, ni hekima kwa mtu kufanya hivyo. Kuchokoza hisia za mtu ambaye ndiyo kwanza ametoka usingizini kunaweza kuzaa kisirani ambacho vinginevyo kisingeweza kuzuka.

Kwa watu wanaojua jambo hili, huwa hawazungumzi jambo lolote wanapokuwa wametoka usingizini, labda kama ni muhimu sana. Wako wale ambao pia, wanapokuwa na jambo mbalo ni muhimu hawaambii wahusika wahusika, kama ndiyo kwanza wametoka usingizini. Husubiri ‘wachangamke’ kama inavyofahamika.

Unapolazimisha kuzungumza na mtu ambaye katoka usingizi muda sio mrefu kinachotokea mara nyingi ukijibiwa vibaya  au usipojliwa usishangae pia hii ndio huwa hali inayotokea. Na ndio ukweli wenyewe akili inakuwa bado ina maluweluwe. Kwa mujibu wa wataalamu hawa wanadai kuwa mara nyingi unpotoka usingizini hiki ndio huwa kipindi ambacho akili yako yako haifanyi kazi vizuri sana, kwa sababu inakuwa haijachanga sana.

Nakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa elimu na maarifa bora yatakayoboresha maisha yako.

IMANI NGWANGWALU,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.