google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 4, 2017

Mambo Ya Kuzingatia Unapokuwa Kazini Ili Usije Ukaishi Maisha Ya Majuto.

No comments :
Wengi wetu tunapokuwa makazini yapo maisha ambayo  tunakuwa tunaishi na yanapelekea majuto kwa baadae. Maisha haya wanayo wengi sana, hasa vijana wanaopata kazi mapema na kujikuta kujuta baadae.
Unachopaswa kujua au kuelewa, upo msingi wa maisha unatakiwa kuishi nao unapokuwa kazini ili baade usije ukaishi maisha ya majuto na kujilaumu sana hasa pale unapofikia uzeeni kwako.
Katika makala haya itafafanua mambo ya kuzingatia unapokuwa kazini ili maisha yako ya baade yawe ya uhakika na usije ukaishi maisha ya majuto. Sasa twende pamoja ili tuweze kujfunza mambo hayo.
1. Tumia pesa zako kwa busara.
Kwa namna yoyote ile unapokuwa kazini na unapata pesa zako wakati upo kazini, jitahidi sana usiishi maisha ya kujisahau. Watu wengi wanapopata pesa wanakuwa wanajisahau na kujua mshahara kwao ndio kila kitu.
Kwa mfano, utakuta pesa unazipata kweli lakini matumizi yako yanakuwa yako hovyo sana, kiasi kwamba unafika mahali huelewi hata hizo pesa zako unazitumiaje. Kuishi maisha haya ni kutafuta janga kubwa la kushindwa kwa baadae.
Ili kuepuka kuishi maisha ya majuto baade, ishi kwa mipango, pesa zako zipangilie vizuri na ishi kwa kusudi maalumu.

2. Kamilisha mambo yako ya msingi mapema.
Kama unajielewa wewe upo kazini na umeamua kufanya kazi kweli, hebu kamilisha mambo yako mapema. Yapo mambo ya msingi unayotakiwa kuyakamilisha mapema kama vile kusomesha watoto na kujenga nyumba.
Ni kosa kubwa sana, kuendelea kufanya kazi kwa muda mrefu pasipo kujiandaa kujenga nyumba yako na kusubiri hadi kustaafu kwako. Jenga nyumba mapema, maliza kusomesha watoto wako mapema na usiache jukumu hilo kwa watoto wengine wakajisomesha wao wenyewe.
Unapokamilisha majukumu yako mapema inakupa uhuru  wa kuishi maisha bora pale unapokuwa umestaafu.
Kwa kifupi, hayo ndiyo mamb unayopsw kuyazingatia has pale unapokuw kzaini na wakati huo unajiandaa kutengeneza maisha bora uyatakayo.
Nakutakia wakati mwema na uwe na siku njema, fanyia kazi haya na kila kheri katika kufikia mafanikio yako.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,







No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.