google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 29, 2017

Ukiruka Mfumo Huu…Umeshindwa Tayari.

No comments :
Kama wewe ni msikilizaji mzuri wa muziki, utakubaliana nami kwamba CD nyingi zimetengenezwa kwa mfumo ambao kama hutaki kusikiliza wimbo unaochezwa basi una uwezo wa kurusha mbele na kusikiliza wimbo mwingine unaotaka.
Kwa hiyo utakuta CD moja yenye urefu wa saa moja , unaweza ukaisikiliza hata kwa dakika ishirini tu, hiyoni kutokana na kuruka ruka huko na pia kuchagua vile vipande muhimu ambavyo wewe unavitaka na unaviona vya muhimu kwako.
Kwa wengi wetu tumekuwa tukitaka kujaribu kuishi maisha yetu kwa mfumo kama huo. Tumekuwa ni watu wa kutaka kuruka vitu vingi au kuishi maisha yaliyopita na kusahau kuishi sasa na kufanya yanayotuhusu kwa sasa.
Unatakiwa kuishi maisha yako kama pumzi. Kwa mfano, huwezi ukasema ukavuta pumzi nyingi leo ili kesho usivute na eti ukabaki unaishi, hicho ni kitu ambacho hakiwezekani hata kidogo katika maisha yote, ni lazima utumie pumzi yako sasa. Hakuna pumzi ya akiba.

Na yale tunayofanya au kwa jinsi unavyoishi, inatakiwa tuishi sasa na si kuishi jana au kesho. Ukimua kuishi leo na kukazana kufanya ya leo basi uwe na uhakika utajijengea uwezo wa kutengeneza mafanikio yako moja kwa moja na unakuwa unaishi kwenye mfumo sahihi  jinsi maisha yanavyotaka.
Wengi wetu wana shindwa kwa sababu ya kuamua kuishi maisha yao kwa kuyarusha. Utakuta mtu yupo leo, lakini anaishi kesho. Kuishi maisha kwa namna hiyo huko ni kujipotezea maisha yako moja kwa moja. Kuruka mfumo unavyotaka, ni sawa na kuamua kushindwa kabisa.
Unatakiwa ukumbuke kila wakati, maisha yetu yametengenezwa kuishi kwa mfumo. Kuishi kwa mfumo sahihi pasipo kuuruka huko ndiko kunapokupa mafanikio. Ila kama utaishi kwa kuruka mfumo wa aina fulani huko ndiko kujitengenezea anguko kubwa la kushindwa kwenye maisha yako.
Leo ni siku yako ya kufanya mambo makubwa. Kesho itakuja kwa wakati wake, kikubwa kwako fanya mambo yako  leo kwa uhakika mkubwa. Ishi kwa mfumo kama unavyotaka hapo utakuwa unatengeneza mafanikio yako mwenyewe.
Unachotakiwa uelewe hapa, hutakiwi kuruka kitu. Fanya mambo kwa mpangilio kama yanavyotakiwa kufanyika. Usijadanganye kwa kuahirisha au kuacha vitu bila sababu ya msingi, ukifanya hivyo utakuwa unaishi nje ya mfumo na utashindwa tu.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.