google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 23, 2017

MAMBO MUHIMU YAKUYAJUA KABLA YA KUINGIA KWENYE UFUGAJI.

No comments :
Habari za leo rafiki, karibu sana katika kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu ufugaji bora wa kuku, lengo kuu la makala haya kukupa elimu iliyosahihi kuhusu ufugaji , Na mambo yote ninayoyaandika yanatoka kwenye uzoefu wangu mwenyewe katika ufugaji karibu sana katika somo letu la leo.

Moja ya changamoto kubwa kwa watu wengi tunajiwekea malengo makubwa kila mwaka kwamba nataka kufanya kile na kile ndani ya mwaka huu lakini kila siku bado unashindwa kuanza hii inatokana na changamoto mbalimbali za hapa na pale.

Pia wengi hushindwa kuanza kwa sababu kubwa ya kokosa hamasa ya ndani juu ya kile walichokiwejiwekea malengo na hii inapelekea kila mwaka kuwa na malengo yaleyale bila kupiga hatua na kwenye upande wa ufugaji mambo ni hayo hayo kila siku.

Utakuta tunajisemea natamani kufuga huku tukiendea kuimba wimbo usiokuwa na vitendo, nini ninachotaka kukwambia rafiki siku hii ya leo  unahitaji kuchukua hatua chukua hatua sasa nasiyo kusubili subili utachelewa sana kufanikisha ndoto yako.


Unapochelewa kuchukua hatua ukumbuke siku zinaenda na majukumu yanazidi kuongezeka huku umri nao unakimbia, ila rafiki yako nina jambo zuri ninalotaka kukwambia na unatakiwa uchukue mara moja.

Jambo hili ambalo nakwambie uchukue hatua sasa ni juu ya wazo la ufugaji.  Unajua kwanini nakwambia ni sasa, kwa sababu hakuna wakati mwingine mzuri wa kuanza zaidi ya sasa, anza kufanya na kuweka mipango yako mapema juu ya ufugaji wako.

Hapa  hapa nimekuandikia mambo ambayo unatakiwa kuyajuwa kwanza na kuyafanyia kazi unapotaka kufanya shughuli ya ufugaji za ufugaji ili uweze kufanikiwa katika ndoto yako ya ufugaji, najua unafahamu kuwa ufugaji kwasasa ni moja ya kazi yenye faida.


1. ELIMU NA MAARIFA SAHIHI KUHUSU UFUGAJI.

Hii imekuwa kama sehemu ya kujifichia kwa watu wengi wanaposhindwa kuanza jambo lllote hasa la ufugaji unakuta wanaibuka na sababu kuwa nashindwa kuanza kwasababu sina elimu sahihi juu ya ufugaji sasa sijui una subiri nini kuitafuta hiyo elimu na maarifa sahihi unajichelewesha rafiki, chukua hatua.

2. TAMBUA UNATAKA KUFUGA KUKU KWA MALENGO GANI. 

Nimuhimu kujua kwa nini unataka kufuga kuku kwa sababu ukijua kwanini unataka kufuga kuku itakupa picha halisi juu ya kuku unaotaka kufuga ili uweze kutafuta taarifa sahihi juu ya ufugaji wako  kwasababu kuna aina nyingi za kuku na kila kuku ana sifa zake na mahitaji yake hivyo ukijua malengo yako kuhusu ufugaji wako itakusaidia sana katika kufanya maamuzi na kutafuta taarifa sahihi kuhusu ufugaji wako.

3. ENEO UNALOTAKA KUFUGIA. 

Unapojua tayari malengo uliyonayo katika ufugaji na kujua aina ya kuku unaotaka kuwafuga sasa utakuwa na picha nzuri juu ya ufugaji wako, baada ya hapo unahitaji kujuwa ENEO GANI UNALOTAKA KUFANYIA UFUGAJI hii itakusaidia kujuwa mali ghafi ambayo itatumia katika banda lako, ni muhimu sana kuandaa eneo la kufugia mapema mara tu ya kuweka malengo yako ya ufugaji, jua eneo la kufugia mifugo yako.

4. GHARAMA ZINAZOHITAJIKA KATIKA KUFANYA UFUGAJI  WAKO.

Baada yakujuwa malengo eneo unalotaka kufanyia shughuli zako za ufugaji ni muhimu sana kuchanganua gharama zitakozotumika katika kuanza ufugaji gharama hizo ni pamoja na banda, chakula, chanjo na tiba, hii itakusaidia kuweka mipango yako sasa ili uweze kufanya ufugaji wako kwa ufanisi mzuri

5. ANZA NA ULICHONACHO.

Hii ni jambo la muhumu sana katika kutimiza malengo ya aina yeyote, ni muhimu kuanza na kile ulichonacho usisubiri hadi uweze kujipanga vizuri sana kwasababu unapoanza inakupa hamasa ya kuendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhusu ufugaji. Anza na kuku idadi yoyote, kama ni kumi, hamsini au hata mia mbili kulingana na uwezo ulionao, kikubwa anza na ulichonacho. 

Naomba niishie hapa kwa leo,

Endelea kunifatitia nina mengi mazuri yakukwambia kuhusu ufugaji naamini yatakusaidia sana.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,

Ni Mimi rafiki yako katika ufugaji,
Frank Mapunda, 
0758918243/0656918243
Karibu sana, 



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.