google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 11, 2017

Ili Kuepuka Makosa Ambayo Uliyoyafanya Mwaka Huu, Katika Mwaka Ujao Unatakiwa kuwa hivi:

No comments :
Siku ya leo nimejikuta nakumbuka sana enzi ambazo nilikuwa nasoma shule ya msingi, nimekumbuka kwa sababu kila nikifanya mtihani nikumpa mzazi alikuwa haangilia zile tiki ambazo nilikuwa nimepata bali alikuwa anaangalia maswali niliyokosa, kisha alikuwa ananihoji mwanangu kwanini umekosa hizi, hapo ilikuwa haijalishi nimepata alama kubwa kiasi gani? Mara baada ya kukosa majibu ni kwanini nimefeli basi nilikuwa nakula mboko zangu za kutosha.
Kwa kipindi kile niliona mzazi  ananionea kwa sababu binafsi  nilijiona nimefaulu sana, lakini kadri siku zinavyozidi kwenda nimekuja kutambua kumbe mzazi alivyokuwa anafanya vile alikuwa sawa kabisa, unajua ni kwanini alikuwa sawa? Nakusihi twende sawa mwanzo mpaka mwisho wa makala haya.
Ziliwa zimebakia siku kadhaa kuamaliza mwaka huu, siku ya leo naomba ufanye tafakari kwa kutazama malengo yako ambayo uliyapanga, angalia malengo hayo yamefikia wapi, kwa sababu yawezekana kabisa ulikuwa umepanga kufanya jambo fulani na mpaka dakika hii ukawa hujafikia lengo lako au umefanikiwa katika lengo hilo.

Endapo kama umefikia lengo lako kwa asilimia zote piga kifua chako mara tatu huku ukisema “asante Mungu kwa kunifanikisha jambo hili”.
Na endapo kama hujafikia lengo lako ninachotaka kusema ni kwamba hizo ndizo alama ambazo umekosa ambazo unatakiwa uzingalie, kuliko kuangalia zile alama ambazo umezipata (malengo uliyoyatimiza).
Kuangalia jambo ambalo hujalikamilisha, humfanya mtu atafakari ni wapi ambapo umekosea na kuanza upya kulitekeleza, lakini jambo hili hufanywa na watu makini tu, bali watu ambao sio makini wao hukata tamaa mapema na kujiona hawawezi tena.
Hivyo kwa kuwa mwako ujao hutaki kufanya tena makosa, na pia kwa kuwa unataka kuona unatekeleza jambo lako kwa wakati ambao umejipangia hivyo ni lazima uhakikishe unafanya maamuzi magumu.
Nasema ufanye maamuzi magumu kwa sababu, yeyote yule ambaye unamuona amefanikiwa katika dunia hii ni kwamba ni lazima ipo siku moja mtu huyo alifanya maamuzi magumu.
Msomaji mwingine atanyoosha kidole  na kusema afisa mipango maamuzi magumu ni yapi?
Nami bila hiana namwambia  maamuzi magumu ni yale ambayo yatafamfanya mtu asiwe wa kawaida hata vitu anavyofanya asifanye kwa kawaida na alivyozoea kwani akifanya kwa kawaida na alivyozea basi hata matokea ya jambo hilo litakuwa ni ya kawaida.
Lakini pia kufanya maamuzi magumu ni lazima ujikane mwenyewe, kwa sababu mafanikio ni gharama lakini pia ni lazima ukubali kuwapoteza marafiki ambao hawana msaada wowote katika maisha yako.
Hayo ni baadhi tu ya maamuzi magumu ambayo unatakiwa kuyachukua siku ya leo ili uepuke makosa ambayo uliyafanya mwaka huu.
Na mwisho nimalize kwa kusema ya kwamba ili uweze kufika mbali zaidi katika kutimiza malengo yako kwa mwako ujao hakikisha ya kwamba unafanya maamuzi yasiyo ya kawaida.
Ndimi afisa Mipango wa Mafanikio Benson Chonya,
0757-909942.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.