google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 18, 2017

Bila Kujali Kitu Gani Kinatokea, Taka Matokeo.

No comments :
Ugunduzi mkubwa duniani, ulianza au ulitokana na watu ambao walikuwa wana matatizo sana. Kwa mfano, kuna eneo fulani duniani ambapo watu walikuwa wakitembea kwa miguu, kutokana na kuchoka huko kutembea kwa miguu ndio utakaja ugunduzi wa magari na hata ndege ili kurahisha.
Ubunifu mkubwa duniani pia ulitokana na watu ambao walikuwa hawajaridhishwa na huduma zinazotolewa. Kwa mfano, watu baada ya kuchoshwa na mabasi yenye ‘keria’ juu hapo ndipo yakaja mabasi yenye ‘buti’ ili kuepusha hata upotevu wa mizigo na inakuwa salama wakati wote.
Mafanikio makubwa duniani pia yanazaliwa na watu ambao walikutana na changamoto nyingi sana. Kuna watu baada ya kuchoshwa na umaskini, basi waliamua kupigana usiku na mchana mpaka kuhakikisha wanaupa umaskini mkono wa kwaheri, hakuna umaskini uliotolewa kwa njia ya lelemama.

Hii yote inadhihirisha kuwa, mafanikio makubwa hayaendi kwa watu ambao wanasema siku nikipata muda au siku nikipata pesa za kutosha basi nitawekeza kwenye mradi wa aina fulani, bali mafanikio makubwa yanaenda kwa watu wote ambao wako tayari kuchukua hatua hata kama rasilimali zao kwa akili na macho zinaonekana ni kidogo sana.
Hebu jiulize aliyegundua ndege au aliyegundua meli ni pesa au rasilimali gani za kutosha alikuwa nazo? Ukiangalia elimu, hawakuwa nazo za kutosha, ukiangalia ni pesa hawakunazo za kutosha, kila kitu kilikuwa hakitoshi kwao, lakini kilichowasukuma ni kutaka matokeo wanayoyataka bila kujali wana rasililmali chache kiasi gani.
Lakini tunaona mwisho wa siku, kutokana na ung’ang’anizi wao huo wakaja na kitu kikubwa, endapo kama wangekaa na kuanza kulia lia kama wewe unavyolia kwamba ‘ooh sina mtaji na siwezi kufanya biashara,’ basi inawezekana kabisa leo hii tungekuwa labda tunatembea kwa miguu.
Maisha ya mafanikio yanataka utayari. Upo tayari kutoa nini? Kwa chochote kile ulichonacho mkononi mwako hata kiwe kidogo sana kina uwezo wa kukufanikisha ikiwa kitu hicho utakilea na kukitunza vizuri. Haijalishi iwe ni kazi ya mshahara kidogo au una biashara ndogo lakini unaweza kupiga hatua na kufika mbali sana kimafanikio.
Kwa nini uendelee kuteseka na kuamini kwamba huwezi kufanikiwa, wakati uwezo huo unao. Kipi kinachokurudisha nyuma, je umeamua kukwama kwa sababu unaamini kwamba wewe si kitu na hutaweza kipiga hatua kwa sababu ya rasilimali ulizonazo ni chache sana, hiyo tu ni kwambie si kweli hata kidogo.
Kuanzia leo, acha kabisa kusubiri kuwa kamili, fanya kila ufanyalo kuhakikisha unapata matokeo unayoyataka. Kama unataka kwekeza kwenye mradi wa aina fulani, wekeza pasipo kutafuta sababu yoyote ile. Sababu hazina nafasi kwenye mafanikio yako, unatakiwa kufanikiwa tu.
Vizuizi au vikwazo vipo tu katika maisha yako. ukitafuta sababu kwamba ipo siku utavikimbia vizuizi hivyo hapo utakuwa unajidanganya sana. Tafuta njia ya kuweza kuondokana na vizuizi hivo ili uweze kuwa mshindi wa maisha yako.  Kwa namna yoyote ile, bila kujali nini kitatokea, taka matokeo ya mafanikio yako.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,






No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.