google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 10, 2017

HEKIMA ZA MAISHA NA MAFANIKIO; Ukipanda Nyasi, Usitegemee Kuvuna Mchele.

No comments :
Karibu rafiki na mpenzi msomaji wa matandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO katika siku ya leo, kuweza kujifunza hekima za maisha na mafanikio. Inawezekana unajiuliza kwa nini tunajifunza hekima za maisha na mafanikio na hekima hizi ni zipi?
Kupitia makala hizi za hekima za maisha na mafanikio utakuwa ukijufunza, misemo au mithali ambazo zilitolewa na wahenga zamani, lakini lengo lake likiwa ni kufunza juu ya maisha na mafanikio kwa ujumla.
Yapo mambo mengi ya kujifunza sana kupitia hekima za maisha na mafanikio. Ni jukumu lako wewe kufanyia kazi hekima hizi ili ziweze kukubadilisha na kukutoa ulipo na kukupeleka sehemu nyingine kimaisha.
Karibu rafiki yangu tuweze kujifunza pamoja, juu ya hekima hizi za mafanikio ambazo nimekuandalia kwa siku ya leo.

1. Kujua njia sahihi ya unakotaka kwenda, waulize wanaorudi na njia hiyo.
Hekima hii ina maana kwamba, ukitaka kujua wapi unaokoelekea kwenye maisha na hata mafanikio yako, ni vyema ukawauliza wale ambao wanafanya kitu hicho ambacho unakifanya kuliko kukaa kimya tu ambako hakuwezi kukusaidia.
Kwa mfano, kama unafanya  biashara ya viatu, ni vizuri ukawauliza watu pia wanaofanya biashara ya viatu ili wakupe mwangaza wa kipi ambacho unatakiwa kufanya kuliko kwenda kuwauliza watu wengine wanaofanya biashara tofauti, hapo utakwama.
2. Usiogope kama unakua kidogo kidogo, ogopa sana kama hukui kabisa.
Katika hekima hii iko wazi inaonyesha kwamba kama kuna mabadiliko unayafanya hata kama ni kidogo, wewe upo sahihi sana kuliko yule mtu ambaye hafanyi mabadiliko yoyote yupo yupo tu  na ameganda, mtu huyo ndio hatari sana.
Kwa hiyo kama kuna hatua unapiga hata kama ni kidogo sana, endelea kupiga hatua hizo maana zitakusaidia kwenda mbele kuliko kama utakuwa hupigi hatua. Ukumbuke hatua ni hatua hata kama ni kidogo vipi.
3. Ukipanda nyasi, usitegemee kuvuna mchele.
Msingi wa hekima hii imejikita kwamba kwa chochote kile unachokipanda kwenye maisha yako uwe na uhakika utakivuna tu. Pasipo kujalisha unapanda nini, jiandae kuvuna kile unachokipanda na usitegemee kuvuna kinyume cha hapo.
Kama unapanda wema, jiandae kuvuna wema. Kama unapanda ubaya pia jiandae kuvuna ubaya huo. Hakuna ambacho utaweza kukivuna kinyume na kile unachokipanda kwenye maisha yako. Kuwa mwangalifu unapanda kitu gani, kwani utakivuna.
4. Fanya mambo mengi kwa busara, lakini si kwa kutumia nguvu peke yake.
Hekima hii pia inatuonyesha umuhimu wa kufanya mambo yetu mengi kwa kutumia busara zaidi kuliko nguvu yaani kwa kulazimisha. Unapofanya mambo yako kwa kutumia busara ni wazi mambo yako yataweza kufanikiwa.
Tambua wapo watu ambao kazi yao badala ya kutumia akili, bali wao ni kulazimisha mambo yaende kwa nguvu hata ndani yake busara haipo. Sasa hapa tunaonywa kutumia pia busara lakini si nguvu peke yake.
Kwa leo kutokana na hekima hizo za maisha na mafanikio tulizojifunza tunaishia hapa, naamini kuna kitu umejifunza na utakitendea kazi mara moja.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.