google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 17, 2017

HEKIMA ZA MAISHA NA MAFANIKIO; Hakuna Mkate, Pasipo Kazi.

No comments :
Naamini leo yako iko poa na unaendelea kuimalizia wikiendi yako kabla ya kesho hujatua kazini kuanza kukamilisha majukumu ya Juma zima. Kama iko hivyo, shukrani za pekee zimwendee Mola wetu.
Ni wakati na jumapili njema kabisa nami na kualika katika jamvi letu la Hekima za maisha na mafanikio. Kumbuka hizi ni hekima ambazo zilitolewa kitambo na babu zetu au wahenga, sasa pia nasi ni muhimu tujifunze.
Na kwa nini tunajifunza misemo au maneno ya wahenga wetu ni kwa sababu, wengi wetu enzi hizo kwanza hatukuwepo, kwa hiyo kwa kujifunza hapa kupitia ukurasa huu, vipo vitu vizuri vya maisha na kimafanikio ambavyo vitatusaidia sote kutujenga kifikra na kimaisha.
Kwa kuwa na mimi si mchoyo, na sipendi kukunyima kitu, naomba nikukaribishe moja kwa moja na twende tujifunze hekima na mafanikio ambazo nimekuandalia siku ya leo. Kikubwa kaa mkao wa darasa na karibu sana.

Hekima ya 1; Hakuna mkate, pasipo kazi.
Hekima hii inajipambanua na iko wazi ikiwa na maana kwamba pasipo kazi, usitegemee mafanikio. Kama utakuwa umekaa tu na huweki juhudi za makusudi za kukusaidia kuweza kupata mafanikio yako, sahau kuhusu mafanikio. Mafanikio yanakuja kwa kazi, na kazi ndio inatupatia mkate au ridhiki ya kila siku.
Hata vitabu vya dini vimeweza kuandika hili ‘asiyefanya kazi na asile’ na hicho ndicho kitu unachopaswa kuzingatia. Kama unataka mavuno ya aina fulani, jiulize ni kazi ipi ambayo umeifanya. Kumbuka wahenga wetu kutokana na hekima zao  wanasema wazi, hakuna mkate, pasipo kazi na hio ndio kweli halisi huwezi kupinga.
Hekima ya 2; Unapokwenda kununua kitu, tumia macho na usitumie masikio tu.
Ni mara nyingi sana wengi wetu tunapokwenda kununua vitu iwe dukani au sokoni, huwa tuna tabia ya kuwasikiliza sana wale wanaotuuzia na kusahau kabisa kuangalia ubora wa kitu. Matokeo yake sasa, tunajikuta ni watu wa kuingia hasara kwa kuchukua vitu vibovu. Utakuta mtu anasikiliza sana maelezo bila hata na yeye kuangalia ukweli uko wapi.
Tabia hii wanayo wengi sana, miongoni mwao inaweza ikawa ni hata wewe, lakini hapa leo hekima hii inatukumbusha hivi, unapokwenda kununua kitu, tumia macho pia na usitumie masikio peke yake. Hiyo ikiwa inaonyesha kwamba ni vyema kujiridhisha kwa macho yako na si kusikiliza peke yako. Kusikiliza peke yake ni sawa na kuamua kuingia hasara.
Hekima ya 3;  Ushauri mzuri, ni bora kuliko dhahabu.
Hii ni hekima  ambayo msingi wake umejikita katika kuonyesha kwamba ushauri mzuri siku zote ni bora kuliko dhahabu. Unaweza ukapata dhahabu leo au mafanikio makubwa leo, lakini kama huna ushauri mzuri hiyo ni sawa na bure, kwani ni rahisi hata kuweza kuipoteza hiyo dhahabu au kitu cha thamani ulichokipata kama huna ushauri wa maana.
Kwa hiyo hapa tunaonywa kuwa ni bora kupata ushauri mzuri kwanza, na kisha ushauri huo mzuri utakusaidia kuweza kutumika katika kupata mafanikio makubwa ambayo yanafananishwa na dhahabu. Mifano hai tunayo, waangalie watu wote ambao walipata ushauri mbovu na maisha yao pia yapo hovyo pia.
Hekima ya 4; Usijilinde sana kwa kutumia fensi, jilinde kwa kutumia marafiki.
Wapo watu ambao katika maisha wanaamua kujilinda sana kwa kutumia kuta za nyumba, wanajilinda sana kwa kutumia fensi na vitu vingine kama hivyo, na kusahau kuwa kujilinda huko kunaweza kukawa kwa bure kama usipojua kwamba hata marafiki ulionao pia nao ni walinzi wazuri tu.
Katika hekima hii inatuonyesha kwamba ulinzi mzuri na wa maana upo kwa marafiki zetu pia. Marafiki zetu ndio watakaotuambia kipi kizuri na kipi kibaya. Pia marafiki zetu ni rahisi wao kutuonyesha  marafiki wengine wabaya na wepi ni wazuri. Kupitia hekima hii ya maisha na mafanikio ni wajibu wetu kutafuta marafiki bora ili wawe walinzi kwetu.
Naamini mpaka hapo kutokana na hekima ulizojifunza kuna kitu cha kipekee ambacho umejifunza. Nikutakie wakati mwema na tukutane wiki ijayo kwa hekima zingine kama hizi za maisha na mafanikio. Kila la kheri.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,









No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.