google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 19, 2017

Changomoto Kubwa Zinazojitokeza Katika Ufugaji Wa Kuku.

No comments :
Habari rafiki, karibu katika makala ya siku hii ya leo, makala ambayo itakuwa inakufikia mara kwa mara kwa lengo la kukupa elimu bora ya ufugaji wa kuku kutoka hatua y akwanza hadi ya mwisho karibu sana

Kwanini ufugaji wa kuku?                    
        
Ufugaji wa kuku ni sekta ambayo inakuwa kwa kasi sana hapa nchini na sasa imekuwa ni sehemu ya ajira kwa watu wengi, ufugaji kwa sasa umekuwa ukifanya vizuri sana kwa kuwa na soko zuri kwa ndani ya nchi yetu na hata nje ya nchi.

 Ufugaji umekuwa sehemu nzuri ya ajira kwa watu wengi na imekuwa kazi rasmi kwa watu wengi, ufugaji umekuwa ni sehemu nzuri ya uwekezaji unaompatia mtu kipato na kumtimizia malengo yake katika maisha.

Pia ufugaji umekuwa ni rahisi kufanya na unafanyika katika maeneo yeyote mjini au vijijini, licha ya kuwa ufugaji wa kuku kuwa na faida nyingi pia ufugaji wa kuku umekuwa na changamoto zake ambazo zinawafanya wafugaji wengi kukata tamaa katika Ufugaji huu wa kuku.


 Jambo lililokuwa zuri ni kwamba changamoto nyingi zilizopo kwenye ufugaji ni aina changamoto ambazo inawezekana kabisa kuzipunguza ilimradi  tu tukiwa makini na kupata elimu bora na sahihi katika sekta hii ya ufugaji wa kuku.

Changamoto hizi zinatokana na  wafugaji wengi wanaingia kwenye Ufugaji bila kuwa na elimu sahihi ambayo itawapa mwongozo bora katika kufikia malengo waliyojiwekea katika ufugaji wa kuku kulingana na eneo husika.

Kwa kukosa huko kujua mambo muhimu yanayohusu ufugaji inawapelekea kupata hasara kubwa na kushindwa kutimiza malengo ambayo walikuwa wamejiwekea katika maisha yao ya kila siku.

Mimi kwa kuliona hili nimeona bora nikuletee elimu hii ili uweze kuwa na elimu sahihi katika uwekezaji wako katika sekta hii ya ufugaji. Mara baada ya utangulizi huo, naomba kwa leo tuanze somo letu moja kwa moja, linalohusu changomoto zinazojitokeza katika ufugaji wa kuku.

MAGONJWA.                                                    

Magonjwa yamekuwa ni changamoto kubwa kwa wafugaji wengi hasa wanaoanza kuingia katika ufugaji na hii inasababisha wafugaji wengi wakate tamaa ya kufuga na kuona kufuga hakuna faida yeyote kwasababu inawapa hasara kubwa sana.

Jambo lakuvutia nikuwa katika mfululizo huu wa makala zangu nitaeleza mbinu ambazo kama utatumia utaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa cha magonjwa ya kuku kwa kifupi nimekuja na majibu juu ya changamoto hii.

GHARAMA KUWA KUBWA ZA CHAKULA.

Hii ni moja ya changamoto kubwa kwa wafugaji wengi wa sasa kwa sababu wanapenda kufuga lakini wanajikuta wanashindwa kwasababu ya kukosa mitaji ambayo itaweza kuwa saidia katika kuwapa chakula mifugo yao. 

Kutokana na changamoto kuwa kubwa kwa upande wa chakula watu wengi wameshindwa kuendelea na ufugaji wa kuku kwa wingi na wamekuwa wakifuga kwa idadi ndogo sana au kuacha kabisa kwa sababu yakushindwa kupata chakula.

 WIZI.

Hii ni moja ya changamoto ambayo zinawakuta wafugaji wengi wa kuku hasa maaneo ya mijini, wezi wamekuwa wakibomoa mabanda na kuingia kuiba kuku wengi nakupelekea hasara kubwa kwa wafugaji.

Jibu la changamoto hii kama unafuga kuku wengi ni bora ukaweka mlinzi anaweza akawa mbwa au mlinzi kwa maana ya binadamu. Ukiweka mlinzi hapo itakuwa imekusaidia kwa kiasi kikubwa kutatua chagamoto hii.

Kwa leo naomba niishie hapa tutaendelea siku nyingine kwa llimu bora ya ufugaji wakuku. Endelea kutufatilia......

Kwa mahitaji ya vifaranga bora kabisa kwa ajiri ya ufugaji karibu sana vinapatikana, 
pia kwa mahitaji ya MASHINE  bora za kutotoleshea vifaranga zinapatika na
bila kusahau mayai kwa ajiri ya kutotoresha, kula yanapatika kwa bei nafuu sana yanasafirishwa popote pale. Mayai na vifaranga vinavyopatikana ni yakuku chotara aina ya kuroiler.
                                                
Karibu sana na wote mnakaribishwa. 

Kwa mawasiliano zaidi, 
0758918243/0656918243.
Ni mimi rafiki yako, 
FRANK MAPUNDA .
KARIBU KATIKA UFUGAJI BORA WAKUKU TUKUZE UCHUMI WA NCHI YETU.



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.