google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 9, 2016

Watoto Wenye Uzito Mdogo Hawaji Kuoa.

No comments :
Kwa mujibu wa tafiti, imethibitika kwamba watoto wa kiume wanaozaliwa wakiwa na maumbo madogo na uzito mdogo, uwezo wao wa kuoa hupungua ukilinganisha na wenzao wenye maumbo makubwa na uzito mkubwa.
Kulingana na moja ya ripoti iliyotolewa na watafiti wa kiingereza kupitia kwenye jarida la la British Medical, imegundulika kuwa wanaume ambao waliozaliwa wakiwa na maumbo na uzito mdogo, ukubwani huchelewa sana kuoa au hushindwa kabisa kuoa.
Hata hivyo, kulingana na matokeo ya uchunguzi huo, imebainika kwamba kuna mambo mengi yanayosababishwa wanaume waoe ikiwa ni pamoja na yale ya kibaiolojia na kijamii.
Na pia imefahamika kwamba, kasoro zinazojitokeza wakati wa kuzaliwa hasa kwa upande wa watoto wa kiume, zinaweza zikapelekea mtu kuwa matatizo makubwa ukubwani.

Matatizo hayo ni pamoja na ugumu wa kujumuika na watu wengine, kupungua kwa uwezo wa kujamiiana, matatizo ya kitabia na hasa kihisia na mengineyo.
Tatizo kubwa liko kwa watoto wakiume wachanga wanaozaliwa wakiwa na uzito unaopungua kilo tatu na nusu. Ukweli ni kwamba watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito pungufu na huo, wako katika uwezekano mkubwa wa kushindwa kuoa wanapokuwa watu wazima.
Watafiti hao wamethibitisha kwamba, kati ya watoto 100 wanaozaliwa wakiwa na upungufu wa uzito huo, 80 huja kuoa na 20 wanaobaki hushindwa kabisa kuoa. Hii si idadi ndogo hata kidogo. Kwa ujumla katika kila watoto watano wa aina hii, mtoto mmoja hatooa anapofikia umri wa utu uzima.
Watafiti hao wanaongezea kusema kwamba, hali hii haichagui iwapo watoto hao ni njiti, umri wa mama zao, kipato chao wanapokuwa watu wazima na hata daraja lao katika jamii.
Kwa ujumla matokeo na utafiti huo yanaonesha kwamba, wanaume ambao wameshindwa kuoa ni wafupi kwa robo tatu ya inchi, wana uzito pungufu kwa takribani kilo 2.5, na kwa ujumla ni wembamba sana ukilinganisha na wenzao.
Hata hivo, tunachokisema hapa ni kuwa,umbo na uzito wakati wa kuzaliwa, vina mchango mkubwa katika kuwafanya wanaume wasioe wanapokuwa watu wazima. Lakini hio sio sababu peke yake inayopelekea baadhi ya wanaume washindwe kuoa.
Endelea kujifunza kupitia diraamafanikio.blogspot.com kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.