google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 13, 2016

Siri 6 Za Kuishi Maisha Ya Ushindi.

No comments :
Kwa kawaida zipo siri na mbinu nyingi sana za kukusaidia kuishi maisha ya ushindi wakati wote. Hakuna haja ya kulaumu au kulalamika  maisha ni magumu, zipo siri za kukusaidia kukabiliana na changamoto zako.
Leo kwa kifupi, naomba nikushirikishe mbinu au siri chache za mafanikio ambazo zitakusaidia kukupa hamasa na nguvu ya kuishi kwa ushindi na mafanikio makubwa sana.
1. Kila wakati, pambana na mambo magumu, wakati mambo hayo bado ni rahisi. Pambana na changamoto zako, wakati changamoto hizo bado ni kidogo. Pambana na kuitunza afya yako, wakati bado umzima. Pambana na umaskini, wakati bado ukijana mwenye nguvu.
Kila changamoto unayokutana nayo kwenye maisha, unaweza kuishinda ikiwa utakabiliana nayo mapema. Acha kusubiri mambo yameharibika ndio uanze kukomaa na changamoto yako. Acha kusubiri nyumba imeungua ndio utafute maji ya kuzimia moto.
Jifunze kutokuishi maisha ya zima moto. Ishi kwa mipango sahihi, ambayo mipango hiyo mwisho wa siku itakuongoza wewe kuweza kufikia katika mafanikio yako makubwa. Wengi wanashindwa katika maisha kwa sababu ya kuchelewa kuthibiti mambo ambayo walitakiwa wayathibiti mwanzoni.
Jiulize ni mara ngapi umekwama, kwa sababu ya kushindwa kuithibiti hali fulani ambayo ulitakiwa kuithibiti mapema? Acha kuendelea kuharibu maisha yako kwa kusubiri eti mpaka mambo yameharibika ndio utafute dawa yake. Changamka sasa na anza kutekeleza majukumu yako mapema.
7
Tunza na kuilea ndoto yako kwa uangalifu, ili ikupe mafanikio.
2. Siku zote katika safari ya mafanikio, kuwa makini sana na jinsi unavyoitunza na kuilea ndoto yako. Kama ndoto yako unaitunza na kuilea katika hali ya hofu na mashaka sana basi, utavuna magugu na hautaweza kufanikiwa.
Na pia kama ndoto yako unatitunza na kuilea katika matumaini makubwa ya kufanikiwa, imani ya mafanikio na kujiamini, uwe na uhakika ni lazima utafanikiwa. Wapo wengi wanaoshindwa kufikia ndoto zao kwa sababu ya kuzielea ndoto zao katika mazingira mabovu.
Kama ulivyo mmea ili ukue ni lazima umwagaliwe maji safi, halikadhalika ndoto  yako iko hivyo hivyo. Ni lazima ndoto yako ituzwe kwa matumaini na imani ya mafanikio na sio kuitunza katika hofu na woga ambapo mwisho wa siku ni lazima utakwama.
Najua hapo ulipo una ndoto ya iaina fulani, jiulize unailea ndoto yako katika mazingira yapi? Je, unajiamini utafanikisha? Au au upo kwenye mazingira ya mashaka na hofu? Mazingira yoyote yale unayoyatumia kuilelea ndoto yako yanakupa jibu kama utafanikiwa au hautafanikiwa kuifanikisha ndoto yako.
3. Ili kufikia mafanikio zaidi ya hapo ulipo, ipo haja na ulazima wa wewe kujituma na kufanya kazi kwa bidii sana nje ya yale mazoea uliyojiwekea. Kwa mfano, kama umezoea kufanya kazi kwa saa 8, ongeza masaa mengine manne ya ziada. Kama umezoea kuamka sa 12, anza kuamka saa 11 alfajiri. Fanya kitu ambacho kitakutoa nje ya mazoea yako yaani ‘comfort zone’. Kwa chochote kile unachokifanya, fanya nje ya mazoea yako. Hiyo itakusaidia sana kujenga misuri mikubwa ya kukuwezesha kufika mabali kimafanikio.
4. Kwa hali yoyote ile ambayo inatokea nje ya wewe haina mchango mkubwa sana wa kuweza kukukwamisha au kukufanya ushindwe kufikia mafanikio yako. Kitu ambacho kitakufanya ushindwe kufanikiwa ni ile hali inayotokea ndani mwako tu.
Hali hiyo inayotokea ndani mwako, ndiyo ina nguvu kubwa sana ya kubadillisha maisha yako na kuwa ya mafanikio kabisa. Hebu jiulize kila unapowaza mafanikio, ndani mwako unajionaje? Unajiona ni kwamba utafanikiwa au utashindwa? Kipi unachokiona ndani mwako?
Haijalishi watu wanasemaje au watasema nini juu yako, hata watu dunia nzima waseme kwamba utafanikiwa, lakini kama ndani yako huoni hivyo ni wazi huwezi kufanikiwa, pia hata dunia nzima iseme kwamba wewe ni wa kushindwa, lakini ikiwa ndani yako unajiona wewe ni mtu wa mafanikio, utafanikiwa.
Kiti kikubwa hapa, jifunze kutokulaumu hali yoyote ile, inayotokea nje katika maisha yako kwamba ndio imekukwamisha. Anayejizuia na kujikwamisha sio mwingine bali ni wewe mwenyewe na hali hasi nyingi ulizozibeba. Kuanzia leo amua kujenga hali bora ndani mwako itakayokupa mafanikio makubwa.
5. Kuna wakati unaweza ukajikuta unaumia sana kwenye maisha yako, hiyo yote kwa sababu ya maoni hasi ya watu wanayokutolea wewe. Sasa ili usiendelea kuumia kwa jambo hilo, kumbuka hivi, hicho ambacho kinaongelewa juu yako ni kwa mujibu wa maoni yao wao wenyewe. Uhalisia wa wewe jinsi ulivyo unaujua wewe.
Hivyo, acha kuchukua maoni ya watu na ukaamua kuyatumia kuendesha maisha yako. Alooo! Ukifanya hivyo utamuia sana na utaiona dunia chungu. Ishi wewe kama wewe kwa kufata kile ambacho moyo wako unakutuma na hiyo itakufanya uishi maisha ya ushindi na mafanikio makubwa.
6. Kitu pekee kitakacho kufanikisha si wingi wa maarifa ya mafanikio unayoyapata kila siku. Mafanikio yako utayapata kwa wewe kuamua kuyatumia maarifa hayo tena kwa uhakika.
Jiulize leo hivi, tokea uanze kujifunza juu ya mafanikio, umechukua hatua kiasi gani? Au umebakia kuwa ni mtu wa kushangilia na kuwaacha wengine wachukue hatua za kimafanikio?
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.

TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.

Ni wako rafiki,

IMANI NGWANGWALU,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.