google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 12, 2016

Maadili Yakufuata Ili Kufikia UTAJIRI.

No comments :
Kila kitu katika maisha ili uweze kukipata kina misingi na maadili yake. Hakuna kitu au mafanikio ambayo unaweza ukayapata kiholela, ni muhimu kwako kufuata maadili yake tena ikiwezekana kila siku ili uweze kufanikiwa.
Kwa mfano, yapo maadili ya msingi ya kufuata kwa mwanamichezo, mwanafunzi, mfanyabiashara au daktari hadi kufanikiwa. Ukiangalia kila eneo la maisha hadi lilete mafanikio linahitaji maadili ya aina fulani hivi.
Hata linapokuja suala la kutafuta mafanikio na utajiri kwa ujumla yapo maadili ya msingi ambayo ni lazima uyafuate ili ufanikiwe. Haya ndiyo maadili ambayo karibu kila mtu ambaye ni tajiri anayatumia.
Je, unataka kujua ni maadili yapi ya msingi ambayo unatakiwa kuyafuata ili uweze kufanikiwa na kuwa tajiri? Hilo lisikupe shida, fuatana nami katika makala haya na tujifunze pamoja.
1. Kufanya kazi kwa bidii.
Kati ya kitu muhimu ambacho kinauwezo wa kukutoa kwenye umaskini na kukufanya ukawa tajiri ni kufanya kazi kwa bidii zote. Hakuna ubishi katika hili, ikiwa utajitoa kufanya kazi kwa bidii ni lazima utafanikiwa tu.
Unaweza leo hii ukawa maskini wa kutupwa lakini kesho utakuwa tajiri kama utajitoa kufanya kazi kwa bidii sana. Haya ni maadili ya msingi sana kuyafuata  kila siku hasa kwa mtu yeyote anayetaka kufanikiwa na kuwa tajiri.

Jiwekee nidhamu binafsi, itakayokusaidia kutengeneza utajiri.
2. Ung’ang’anizi.
Ili ufanikiwe na kuwa tajiri, moja ya maadili ambayo unatakiwa kuwa nayo ni kwa wewe kukubali kuwa king’ang’anizi. Huwezi ukafanikiwa ikiwa hautakuwa king’angazi hasa kwa yale mambo unayoyafanya.
Ukiangalia sifa na maadili yaliyowafanya matajiri kupata utajiri wao ni kule kung’ang’ania kwao. Waliposhindwa jambo fulani, hawakuona kwamba hicho ndicho kikwazo bali waling’ang’ania hadi kufanikiwa.
3. Nidhamu binafsi.
Hutaweza kufanikiwa na kuwa tajiri katika maisha yako kama huna nidhamu binafsi. Maisha yako ya mafanikio yanajengwa hasa kwa wewe kujitengenezea nidhamu binafsi katika kila eneo.
Kwa mfano, unatakiwa kuwa na nidhamu binafsi kwenye kazi unayoifanya, matumizi yako yako ya pesa na hata nidhamu binafsi kwenye malengo uliyojiwekea.  Utafanikiwa na kujenga mafanikio makubwa kama una nidhamu binafsi.
4. Kujiamini.
Maadili mengine ya msingi ambayo unatakiwa kuwa nayo ni kujiamini kwako. kila wakati ni muhimu kujiamini ili ufanikiwe. Mara nyingi watu wanaojiamini ndio wanaofanikiwa sana.
Unapokuwa unajiamini inakusaidia sana hata katika changamoto nyingi uweze kukabiliana nazo na kuzishinda. Ikiwa nia yako ni kufikia utajiri mkubwa, hebu anza kwa kujiamini kwanza.
5. Kufanya kazi kwa mwendelezo.
Kile kitu ambacho umekichagua kukifanya ni muhimu sana kukifanya kwa mwendelezo kila siku. Hata kama ni kwa kidogo lakini kitu hicho ni lazima ufanye kila siku ili kikupe nguvu ya kukufanikisha.
Wanaofanikiwa si kwamba wanauwezo mkubwa sana kama unavyofikiri, bali mambo yao huyafanya kila siku. Weka nguvu zako kwa kile unachokifanya kila siku, ni lazima utapata matokeo ya kukusaidia kufanikiwa.
6. Simamia maamuzi yako.
Lazima uwe na maamuzi ambayo hayabadiliki badiliki. Ukisema mwaka huu nakwenda kufanya jambo hili ni vyema ukatekeleza jambo hilo na sio kuwa mtu wa kuacha acha.
Kwa jinsi unavyozidi kuwa na maamuzi imara ni msaada kwako wa kuweza kukusaidia kufikia malengo ya aina fulani ambayo unakuwa umejiwekea tena kwa wakati mwafaka.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.