google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

May 22, 2017

Utajiri Wako Unacheleweshwa Hivi...

No comments :
Kwa jinsi binadamu tulivyo, tunaweza kuona vitu vyote ambavyo havionekani mbele ya macho yetu. Ukifuatilia kwa undani unagundua kuwa vitu ambavyo tunaambiwa na kuamini kuwa havionekani, kiuhalisia vitu vyote vyaweza kuonekana endapo ukiamua. Kwa mazoea, wengi tunafikiri kwamba kama kitu hakionekani mbele ya macho yetu ya kawaida, basi tunasema...
hakipo. 

Ajabu na kweli ni kwamba, mtu asipoona kitu kwa macho yake ya kawaida, basi udhani kwamba kitu hicho hakionekani na wengine ufikiri kwamba kitu hicho hakipo kabisa duniani. Kumbuka kuwa kuendelea kufikiri na kuamini kwamba kitu fulani hakionekani au hakipo haina maana kwamba hakionekani kwa wengine! Wewe usipoona wengine wanaona.

Tunapodhani kwamba kitu fulani hakipo duniani, wakati kipo, moja kwa moja tunapoteza uwezo wetu wa ndani na nje wa kukifanya kile kisichoonekana kionekane mbele ya macho ya wengi.

Kwa binadamu ni akiri yake pekee iliyo na uwezo wa kuona vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Unapofikiri kwa kutumia akiri (ubongo), hapo tunasema kuwa umeona kwa macho ya akiri au ubongo. Pia, kile uonacho kupitia fikra zako, ndicho ambacho ukusukuma wewe kutumia rasilimali zilizopo, ili kukiweka katika uhalisia.


Kitu kikishakuwa kwenye uhalisia, basi hapo tutasema “umefanya kwa vitendo au umetenda”. Ukisha tenda, maana yake ni kwamba, unakifanya kile ambacho kilikuwa hakionekani mbele ya macho yetu ya kawaida, kionekane sasa machoni mwa wengi. Endapo watu wataona kile ulichotenda, wasijidanganye kuwa “wameona BALI wajue wametazama”.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya “kuona” na “kutazama”. Kutazama siyo kuona, na kuona ni zaidi ya kutazama. Dhana nzima ya “KUONA” ni pale tunapoweza kutumia akiri kuota ndoto, halafu tukapiga picha, halafu tukapanga, tukaamini, na kisha tukatenda. 

Kwa maana nyingine ni kwamba, akiri (ubongo) ni kiwanda na karakana ya kuzalisha mambo mapya. Lakini pale tuonapo picha ya kitu kutokea nje (kwa macho ya kawaida), basi huko siyo “kuona” bali ni “KUTAZAMA”.

Binadamu wengi tunao uwezo wa kuona kila kitu endapo tunataka kufanya hivyo. Pamoja na uwezo mkubwa tuliopewa, bado hatuutumii katika kuona fursa za kujiondoa kwenye majanga ya umaskini. 

Watu waliofanikiwa mara nyingi wanatwambia kila siku kuwa popote tulipo Tanzania tumezungukwa na fursa nyingi. Kwanini sasa watu wengi ni maskini katika nchi iliyo na fursa nyingi? Jibu ni moja tu nalo ni watu wengi hawaoni fursa bali wanatazama fursa”.

Utajiri wa uhakika hautapatikana kutokana na watu wengi kutazama fursa BALI ni pale tu watu watakapoweza kutumia akiri zao kuona fursa na kisha kuanza kuchukua hatua za maksudi ili kuzifikia fursa hizo. 

Kumbe watu wengi tumekuwa ni watu wa “kutazama” fursa na siyo“kuona” fursa. Unapoona fursa unakuwa na ujasiri, nguvu na shauku ya kutenda ili kufaidi fursa husika. Lakini unapotazama fursa, mara nyingi unajawa sana na uoga, hofu inayotokana na wewe kukosa majibu muhafaka ya maswali unayojiuliza baada ya kuona kwa macho yako kile kilichofanywa na wenzako.

Unapotazama kitu kilicho mbele ya macho yako, mara nyingi utajiuliza maswali mengi bila majibu juu ya jinsi kilivyotengenezwa. Unapokosa majibu sahihi ya mswali yako, mara nyingi utapata hitimisho moja tu! Nalo ni “HAIWEZEKANI”. 

Ukishajiridhisha kuwa haiwezekani, basi unaamua kwenda kutazama fursa nyingine ambayo nayo utapata hofu na woga wa kuifanyia kazi. Mwisho wake unaishia kuwa ni mtu wa kutazama na kuongea tu! Huku ukizidi kuandamwa na maisha ya taabu na umaskini.

Watu wenye kuona fursa ndio wenye “maono”. Maono ni ndoto kujumlisha na ukweli wa mambo. Ukiwa na maono yafanyie kazi. Tumia macho ya akiri au ubongo kuona fursa. 

Ukitumia macho ya ubongo au akiri, utaweza kuona vinavyoonekana na visivyooekana. Fursa za uhakika hazionekani kwa macho ya kawaida. 

Usipoona fursa machoni mwako haina maana kwamba fursa hizo hazipo! ni uhamuzi wako tu! ukiamua zionekane na ziwepo basi, itakuwa hivyo. 

Lakini, ukiamua zisiwepo basi, hazitakuwepo wala hazitaonekana mbele ya macho yetu ya kawaida. Jambo hili aliwahi kulisisitiza mwanafalsafa wa Kifaransa aliyejulikana kama Henri Bergson kuwa “Jicho linaona kile ambacho akiri iko tayari kukiona au kuelewa”

Kutokana na maneno hayo ya Bwana “Henri Bergson”, tunajifunza kwamba fursa ambazo hazionekani machoni mwako, ni lazima uziite wewe mwenyewe ndipo zitakuja kwako na usipofanya hivyo watu wengine watafanya hivyo, mwisho wake fursa ulizotakiwa kuzifaidi wewe, utabakia KUZITAZAMA kwa jirani. Endapo jirani au watu wengine wasipoziita fursa hizo, basi zitaendelea kubakia katika hali yake hiyo ya kutoonekana, mpaka zitakapoitwa na vizazi vijavyo.

Leo hii Tanzania kama taifa tunaishi maisha duni kutokana na ukweli kwamba watu wengi wanaanzisha miradi ya biashara baada ya kutazamia kwa wengine. Ni bora ukaona mradi anaoufanya mwingine kuliko kuutazama. 

Watu wengi hasa Tanzania, huwa hawaoni miradi bali uitazama tu basi. Kwa maana nyingine ni kwamba, unapoona mwenzako akijishughulisha na mradi fulani wa kibiashara na wewe ukafanya kama anavyofanya bila kuongeza kitu chochote kipya, basi ujue kuwa mradi huo “haujauona”BADALA yake “umeutazama” tu!.

Ni nini faida za kufanya mradi ambao umeuona?
Kimsingi nchi inapokuwa na watu wengi ambao tunafanya miradi tunayoiona kwa macho ya ubongo au akiri zetu, ni wazi kwamba tutakuwa na uwezo mkubwa wa kutatua changamoto na kero nyingi ambazo zinasababisha maisha magumu kwa jamii tunayoishi nayo. 

Pili, tutaweza kutengeneza bidhaa na huduma za thamani kubwa kwa watu wa Tanzania na dunia kwa ujumla. Tatu, tutasaidia katika kuharakisha ukuaji wa uchumi wetu binafsi na taifa letu kwa ujumla.

Watu wengi tukiona na siyo kutazama miradi ya maendeleo, tutaweza kutegeneza bidhaa nyingi ambazo ni tofauti tofauti. Tukiwa na bidhaa nyingi zenye ubora wa hali ya juu, ni wazi kwamba tutaweza kuvuta pesa nyingi kutoka kwa watu wengine hasa nje ya nchi. Watu wenye pesa zao, watapenda watume pesa zao kwetu, ili kupata bidaa na huduma na hivyo kutufanya sote tuwe na pesa nyingi. 

Kwa ngazi ya kitaifa ni kwamba watu kutoka mataifa ya nje watapendelea kutuma pesa zao Tanzania ili kununua suruhisho tulizonazo juu ya changamoto walizonazo kwao – hali hii ndiyo itachangia uwepo wa ajira na hatimaye nchi kuwa na uchumi mkubwa.

Hili tuwe na uwezo wa kuona miradi tufanye nini?
Katika hili hakuna namna na hakuna njia muhafaka ZAIDI ya kuzidi kuwekeza sana kwenye fikra. Ninaposema kuwekeza kwenye fikra ni zaidi ya watu kusoma hadi vyuo vikuu au kubobea kwenye taaluma fulani.

Uwekezaji mzuri kwenye fikra ni ule ambao unajifunza kila siku kwa kutumia njia mbalimbali, kama vile kujenga tabia ya kuwa mdadisi wa kila jambo/kitu na hasa yale yanayohusu kile ambacho unakifanya au unatarajia kukifanya.

Kabla ya kuanzisha mradi wako hakikisha unafanya utafiti wa kero na changamoto zinazowakabili watu waliokuzunguka au wengine wa mbali --- kwa kawaida kero inayo wapata watu waliokuzunguka mara nyingi huwa inawapata pia watu wengi walioko mbali na wewe.

Uzuri wa uwekezaji katika fikra hauna usumbufu na wala hauitaji gharama kubwa. Kinachohitajika ni nidhamu ya kufanya kile ulichopanga kukifanya hata kama ni kigumu. Kwa hiyo, huu ni uwekezaji ambao unaweza kufanywa na karibu wa aina yoyote, ilimradi mtu awe anajua kusoma na kuandika.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.