google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 21, 2015

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuishi Kwa Mafanikio Kazini Kwako.

No comments :
Watu wenye uwezo mkubwa wa kijamii, wanaweza kuishi karibu na kila mtu, na ikiwa unataka kufanikiwa katika fani yako, unatakiwa kuwafanya watu wajisikie vizuri. Jaribu kuchunguza ni kitu gani kinachowaudhi, nini kinawafurahisha na baadae utumie vifaa hivyo wakati unaposhirikana nao kila siku.
Nguzo kuu ya kupendwa ni kuweza kujinasibisha na hali tofauti. Hii haina maana kwamba, unalazimika kuwa mtu ambaye wewe sivyo ulivyo. Kila mmoja wetu ana matatizo yake, anaweza kubadilika na ni mwenye utashi tofauti. Unahitaji kujitambua wewe mwenyewe kiasi cha kutosha na kufahamu ni kwa namna gani tofauti unaweza kujitokeza kwa kundi fulani la watu.
Fani ya saikolojia inayoelekea kwenye suala hili ni Saikolojia ya jamii. Na kwa bahati nzuri tunazo kumbukumbu nyingi sana kutoka kwenye tafiti za kidaktari zinazotueleza namna mawazo, hisia na tabia za watu zinavyotawaliwa na uhalisia, fikara na matarajio ya watu wengine. Tumia utafiti huu kuwa mtu ambaye kila mtu atapenda kufanya nawe kazi.
Lakini waweza kugundua katika nafsi yako  zinazoweza kushirikiana  na kila mtu, ikiwa ni mwangalifu kwa nafsi yako na zile za wengine. Wanasaikolojia ya jamii huwaita watu wanaochunguza hali za kijamii na kujaribu kutafuta vile watakavyoweza kuishi na jamii kulingana na wao walivyo kuwa ni ‘ wafuatiliaji wa juu ya nafsi’.

Wafuatiliaji wa nafsi ni mabingwa wa kutambua kile watu watu walio mbali mbele yao wanachotarajia kwa wakati waliopo. Na watu hawa wana hisia za juu katika ufundi na mbinu za kuvutia, hutazama watu wengine wanavyotumia mbinu fulani, hujizoeza na baadaye kuzitumia wao.
Kwa baadhi ya watu, ujuzi huu wa kufuatilia wengine ndani ya kundi, huja wenyewe, wao ni kama kinyonga wanaoweza kusoma hisia za watu wengine.
Vinyonga hawa hujua nini cha kusema kwa wakubwa wao wa kazi ili kuwafurahisha wakati pengine ng’ombe wa wakubwa hawa nyumbani wanapokufa. Watu wengine ni wafuatiliaji wa nafsi.  Watu hawa hujaribu kubadili ili kuweza kwenda mbele kama wanavyotaka wao.
Watu hawa wanachojua ni hali moja tu ya kujiendesha kama wanaweza kubadilika kwa kufuata hali ilivyo. Hawa ni watu unaoweza kukuta wakifanya mizaha kwenye mkutano muhimu wa kikazi ama kuonekana wasio na mzaha kwenye tafrija ama pikiniki ya kampuni.
Mara nyingi vinyonga huonwa kuwa wapuuzi na hawa wafuatiliaji wa chini wa nafsi, lakini ukweli ni kwamba vinyonga huwa hawapotezi nafasi kutokana na uwezo wao wa kufanya kazi ns watu wa kila aina.
Ikiwa utaweza kufanya kazi na watu wenye tabia tofauti, si kwamba utapendwa zaidi kwenye nafsi yako ya kazi tu bali utaweza kutimiza malengo yako binafsi.
Watu wanaoweza kujenga urafiki na watu wa aina tofauti kwa wingi, wanakuwa na uwezo kubadilikaa vile wanavyofikiri wao ndivyo walivyo, kwa mujibu wa Profesa Tracy McLaughlin-Volpe, mhadhiri wa Saikolojia kwenye Chuo kikuu cha Vermont.
Tofati na kuwa na marafiki wenye tabia za aina moja, kuwa na marafiki wenye tabia tofauti kunakupa uwezo zaidi za aina moja, kuwa na marafikki wenye tabia tofauti kunakupa uwezo zaidi wa kujijengea picha nzuri zaidi yako, unakuwa una nafsi ya kuweza kubadilika na kuwa tu unayetaka kuwa.
Unahitaji kuwa mtu unayebadilika pale inapobidi, kwa sababu wanasaikolojia wa jamii pia wamegundua kwamba watu hukumbuka kirahisi mabaya kliko mema.
Hivyo, ukimweleza mfanyakazi mwenzako mgeni kwamba mkubwa wenu ni mtanashati , muwazi asiye na mwelekeo, ni wazi mfanyakazi huyo mpya atamchukulia zaidi mkubwa wenu huyo kama mtu asiye na mweleko kabisa,
Kumbukumbu zako mbaya huweza kunasa zaid kwenye akili yako kuliko kumbukumbu nzuri. Ikiwa unataka kupendwa, kubaliana na udhaifu wako na uwa tayari kuubadili. Wale wanaojaribu kwa katia hali zao bora wasikivu, wenye kuweza kujieleza, wanaopenda wengine bila wao wenyewe kujua watafanya mambo mazuri ofisini mwao.
Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya ujasiriamli na endelea kutembelea DIRA YAMAFANIKIO kujifunza na kuhamasika zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.