google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 24, 2015

Jinsi Unavyoweza Kushinda Tatizo Ulilonalo Na Kuishi Maisha Ya Ushindi Na Furaha.

No comments :
Kila mmoja wetu katika maisha yake huwa anakabiliana na matatizo ya aina fulani, ambayo katika hali ya kawaida huwa siyo rahisi kuyakwepa. Matatizo haya mara nyingi huwa yanajitokeza katika biashara zetu, familia na wakati mwingine ni matatizo ya mtu binafsi ambayo huwa nayo. Wakati mwingine matatizo haya, huwa yanaonekana ni makubwa sana kwetu kama mlima kiasi kwamba tunaanza kufikiri tunashindwa kuyamudu.  

Kutokana na matatizo haya wapo ambao hufikiri na kujiona wanamkosi na wapo ambao hufikiri kuwa wamerithi kwa namna fulani matatizo. Kila mtu huja na mtazamo wake kutokana na matatizo yanayomkabili. Kitu wasichokijua kumbe ndani yao wanauwezo mkubwa wa kushinda matatizo waliyonayo na kuishi kwa ushindi ili mradi tu waitambue siri hiyo na kuweza kuitumia vizuri.
Katika makala hii utajifunza njia, mbinu na mikakati ya kukusaidia kushinda tatizo ulilonalo na kuishi maisha ya ushindi. Utatambua jinsi unavyoweza kuhamasika na kujiamini wewe mwenyewe binafsi kuwa unaweza kutatua tatizo lako na kufanikiwa kusonga mbele bila shida yoyote. Ieleweke kuwa kila tatizo ndani yake huwa lina njia ya kulitatua hata liwe kubwa vipi.
Inaweza isiwe rahisi sana kwako kunielewa lakini, kwa vyovyote vile iwavyo kama una tatizo linalokukabili huo si mwisho wa kufanikiwa kwako. Bali ni dalili tosha ya kukupeleka kwenye mafanikio unayoyataka. Unaweza ukajiuliza kwa nini hiyo iko hivyo? Ni kwa sababu matatizo yanakuwa yanakupa ukomavu ambao hukuwa nao hapo mwanzo ikiwa utajifunza kupitia matatizo hayo.
Unawezaje kushinda matatizo uliyonayo na kuishi maisha ya furaha na ushindi?  
1. Amini inawezekana kulitatua tatizo ulilonalo.
Siku zote ushindi wa mambo yote huwa unaanzia kwenye kuamini. Kuamini ndiyo nguzo kuu ya mafanikio. Unapokuwa na imani inakusaidia kuweza kutatua tatizo ulilonalo hata liwe kubwa vipi. Kitendo cha kuwa na imani kinakupa ujasiri wa kukabiliana na tatizo lako bila woga. Watu wenye imani kubwa mara nyingi huwa ni washindi katika mambo yao.
Hata ukiangalia dini nyingi duniani msingi wake mkubwa umejikita kwenye imani. Watu mbalimbali waliopata matatizo kipindi hicho walitumia imani kama nguzo kuu na kuamini kuwa wanaweza kufanikiwa kutoka katika matatizo waliyonayo na ni kweli waliweza kutoka. Hivyo ili uweze kutoka katika tatizo ulinalo ni muhimu kuwa na imani ya kukusaidia kutoka hapo.

2. Lijue tatizo lako vizuri.
Kuamini tu peke yake hakutoshi, ili kuweza kutoka kwenye tatizo ulinalo ni muhimu pia kulijua tatizo lako vizuri. Kwa nini ninasema ni muhimu kulijua tatizo lako? Unapolijua tatizo lako hiyo inakusaidia kuweza kulikabili vizuri bila woga  na hatimaye kulishinda. Kama tatizo lako hulijui vizuri itakuwa ngumu kulishinda.
Hata unapokwenda kwa daktari kwa ajili ya kutibiwa pamoja na kuwa unajua kuwa unaumwa na umemweleza daktari kuwa pengine kichwa kinauma, lakini daktari huyu atalazimika kukupima kabla ya kukupa dawa. Anachofanya daktari hapa, nikuhakikisha anajua tatizo lako vizuri kabla hajakupa dawa ambazo hazihusiki. Ili utoke kwenye tatizo ulinalo ni muhimu ulijue vizuri ili upate njia sahihi za kulikabili.
3. Acha kuchanganyikiwa na tatizo lako.
Hata kama ikitokea tatizo lako limekuwa kubwa kiasi gani gani kitu cha msingi acha kuchanganyikiwa na tatizo lako. Unaweza ukasema ‘aah hili haliwezekani’, lakini ninachotaka kukwambia inawezekana. Unapokuwa unakuja juu ama unajihisi kuchanganyikiwa mara nyingi kinachokutokea unakuwa hauna uwezo wa kulikabili hilo tatizo na badala yake unalikuza.
Watu wengi huwa wanashindwa kukabili vizuri matatizo yao kutokana na kuhisi kuchanganyikiwa. Linapotokea tatizo kaa chini kwanza tulia kwa muda kisha tambua njia sahihi ya kulikabili. Mara nyingi huwa linaonekana kubwa ni kutokana na jinsi tunavyolipokea. Tuchukulie kweli hata kama ni kubwa hata ukija juu kiasi gani au uhisi kuchanganyikiwa utafanyaje? ndio limeshatokea. Kitu cha msingi tuliza kwanza sana akili yako unapopata tatizo, ili upate njia sahihi za kulitatua.
4. Acha kufikiria sana juu ya tatizo hilo.
Usipoteze muda sana kufikiria juu ya tatizo lako. Si maanishi hapo unakuwa unalipuuza hapana, ila badala ya kulifikiria tatizo hilo sana weka nguvu zako nyingi katika kulitatua tatizo hilo na kulishinda. Kama utaendelea kulifikiria tatizo hilo kwa muda mrefu usishangae kama itatokea hutapata suluhisho la kulitatua.
Weka nguvu nyingi chanya katika kutatua tatizo lako. Ikitokea umeshindwa kwa namna moja au nyingine tafuta msaada wa kukusaidia kutoka kwenye tatizo hilo na acha kung’ang’ania kulifikiria. Inawezekana tatizo linalokusumbua linaweza lisiwe kubwa sana kama unavyolifikiria, zaidi unajiumiza bure kwa kulifikiria sana.
 5. Acha kuzungumzia kushindwa.
Inaweza ikawa inaonekana kweli upo katika hali ngumu ambayo inapelekea kushindwa hiyo ni sawa, lakini acha kuzungumia juu ya kushindwa kwenye tatizo lako. Kwa kadri unavyokuwa unazungumzia kushindwa ndivyo ambavyo unakuwa unakosa ujasiri wa kukabiliana na tatizo ulinalo na mwisho wa siku unajikuta unashindwa kabisa kulitatua.
Kumbuka tatizo lolote ulinalo unaweza kukabiliana nalo. Haijalishi ukubwa uliopo kwenye hilo tatizo, kwa vyovyote vile iwavyo mwisho wake upo. Jipe moyo inawezekana na hakuna marefu yasiyo ya ncha, kama ni hivyo na tatizo lako litaisha hivyohivyo bila wasiwasi.
Nakutakia kila la kheri katika safari ya kufikia mafanikio makubwa. Karibu sana kwenye mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika kila siku na endelea kuwashirikisha wengine kuweza kujifunza zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048 035,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.