google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 31, 2015

Tabia Tatu Muhimu Ambazo Watu Wenye Mafanikio Wanazitumia Kila Siku Kufikia Mafanikio Makubwa.

No comments :
Njia pekee na ya haraka kwa wewe kufikia mafanikio makubwa ni kuhakikisha unajijengea tabia kama walizonazo watu wenye mafanikio makubwa. Watu wenye mafanikio makubwa katika maisha yao wana tabia za aina fulani ambazo wanazifuata kila siku bila kuacha. Ni tabia hizo hizo ambazo zinawasaidia sana kuwafanikisha kwa kile wanachokifanya.
Ili uweze kufanikiwa na hatimaye kufikia viwango angalau vinavyofanana na wao, unalazimika kujifunza kujijengea tabia kama walizonazo. Hiki ndicho kitu cha lazima ambacho unatakiwa kufanya kila wakati. Bila kujijengea tabia hizo, suala la kuwa na mafanikio makubwa sahau katika maisha yako, zaidi  utaishia kuwa kama ulivyo sasa na maisha yako ya kawaida tu.
Usije ukafikiria nasema hivi kwa lengo la kukatisha tamaa au ukaona kwamba na kudharau huwezi kitu, hapana. Ninachotaka ujue hapa  huo ndio ukweli wa wazi ambao ninaotakiwa nikwambia uujue, sitaki kukudanganya kwa chochote, ni lazima kujijengea tabia hizo kwa faida zetu wenyewe na mafanikio yetu.
Na pia tambua kwamba tabia hizo ndizo zilizowasadia na kuwafikisha watu kama akina Bill Gates, Warren Buffet, Brian Tracy na wengineo wengi wenye mafanikio makubwa pale walipo sasa. Maisha ya watu hawa siku zote wanazitenda tabia hizi na kuzifuatilia bila kuacha. Unaweza ukawa ni mmoja watu kama hawa ikiwa utakuwa na tabia kama zao. Je, Unajua ni tabia zipi hasa walizonazo?
1. Kupangilia siku inayofuata mapema.
Unaweza ukafikiri ni kitu cha kitoto lakini huo ndiyo ukweli, watu wenye mafanikio siku zote wamejijengea utaratibu wa kupangilia siku zao mapema ikiwezekana kabla. Nakumbuka wakati ninajijengea tabia hii mwanzoni niliona ni kama kitu kinachopteza muda na wala hakina maana yoyote ile kwangu.
Lakini nilipouzoea utaratibu huu nilikuja kugundua unapopangilia siku yako mapema, mambo yako mengi unakuwa unayafnya kwa urahisi na ufanisi mkubwa.  Hii inakuwa hivi kwa sababu unapopangilia siku kila kitu kinakuwa kwenye utaratibu na ratiba ya utekelezaji. Hivyo inakuwa sio rahisi kupoteza muda kwa namna yoyote ile.
Kwa msingi huo, matokeo chanya utayaona ikiwa utafuata tabia kama hii. Kabla hujalala jizoeze kila siku kupanga mambo yako mapema na kujua kwa siku ya kesho unakwenda kufanya nini?. Kwa kadri siku zinavyosonga utazoea na utaona utaratibu ni wa kawaida. Ni muhimu sana kwako kujifunza tabia hii ya kupangilia siku yako mapema ili kufanikiwa zaidi.

2. Kuweka vipaumbele mapema.
Watu wenye mafanikio mbali na kuipangilia siku nzima ya kesho mapema, lakini  ni watu wenye utaratibu mzuri wa kujiwekea vipaumbele mapema kabla ya siku inayofuata haijaaanza. Wanakuwa ni watu wa kujua kesho wataanza kufanya kazi gani na itafuatia kazi gani tena. Hakuna ajali wala mshituko wa kiutendaji kwao. Kila kitu kimepangwa tayari katika utaratibu ambao ni rahisi kuweza kufuatwa.
Watu hawa wanajua bila vipaumbele hakuna kitakachoweza kufanikiwa zaidi ya kurukia hiki au kile katika kazi na kujikuta ni mtu wa kugusa na kuacha kazi. Kwa sababu hujiwekei vipaumbele unaweza ukawa unashangga siku nzima ya kazi hujafanya kazi ya maana zaidi ya kuruka ruka mara huku mara kule. Hiki ni kitu ambacho kinawatokea wengi.
Hata ukija kuangalia mazingira mengi ya kazi nyingi zinafanywa bila ufanisi kwa sababu ya kukosa vipumbele. Ukijifunza kuweka vipaumbele kazi zako nyingi utaweza kuzisukuma kwa mwendo mkubwa kuliko unavyofikiri. Kwa sababu ndani yako unakuwa na kitu kinachokwambia ni lazima nifanye kitu hiki. Ukichunguza siri kubwa mojawapo ya watu wenye mafanikio umejificha kwenye tabia hii ambayo siyo rahisi kwako kujua.
3. Kukamilisha kazi waliyoianza mpaka mwisho.
Kama unataka usifanikiwe katika maisha yako jiwekee utaratibu wa kuanza kazi nyingine kabla hujamaliza ile ya kwanza. Kwa maisha hayo ukiamua kuyachagua kwako, suala la kuwa na mafanikio litabaki kuwa kwako hadithi. Wapo watu ambao maisha yao yako hivi, ni watu wa mipango mingi hivyo kujikuta wanarukia mpango huu mara ule lakini yote ikiwa inatakiwa umaliziwaji.
Watu wenye mafanikio ni watu wa kulenga kitu kimoja na wanahakikisha kumekamilika na kufuata kingine tena. Hata siku moja hawarukii mambo, ni watulivu ndani ya mioyo yao lakini pia ni watu wa kujizuia kukurupuka. Hii ni moja ya tabia waliyojijengea na inawasidia kufikia mafanikio makubwa katika maisha yao siku zote.
Hitimisho
Ikiwa utaendeleza tabia hizi tatu katika maisha yako, uwe na uhakika ufanisi na utendaji wako wa kazi utaongezeka na kuwa wa kiwango cha juu.
Kwa makala nyingine nzuri zaidi endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza na kuboresha maisha yako kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048 035,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.