google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 13, 2015

Hii Ndiyo Sababu Kubwa Inayokufanya Uahirishe Mambo Yako.

No comments :
Kuna wakati ambapo Professa mmoja kutoka chuo kikuu cha Havard, Marekani aliwahi kufanya utafiti ambapo alitaka kujua ni kwa nini hasa watu wengi huwa wana tabia ya kuahirisha mambo yao mara kwa mara. Aliamua kufanya utafiti huo mara baada ya kutambua kuwa kuahirisha mambo ni moja kati ya tabia inayokwamisha wengi katika safari yao ya mafanikio.
Bila shaka hata wewe unaweza ukawa shahidi katika hili ni mara ngapi hasa umekuwa ukiona watu ama wewe mwenyewe binafsi ukiahirisha mambo yako mengi zaidi, ambayo yangeweza kukusaidia kusonga mbele? Najua ni mara nyingi umekuwa ukifanya hivyo na pengine bila kujiuliza  kwa nini iko hivyo.
Katika utafiti wake huo ilikuja kubainika kuwa binadamu kama binadamu huwa anatabia ya kuahirisha mambo inayotokana na kitu kimoja tu. Kitu hicho ni kupenda kuwa huru na kufurahia maisha ya sasa na kuweza kusahau mambo ya baadae. Kufurahia maisha ya sasa inaweza ikawa ni kupenda kulala sana, kuongea, kutembea, kuangalia tv au mpira na mengineyo. Lakini  hii ndiyo sababu inayofanya wengi wawe wanaahirisha mambo yao.

SOMA; Huyu Ndiye Mtu Pekee Anayekufanya Ushindwe Katika Maisha Yako.

Unaweza ukawa bado hujanielewa vizuri lakini iko hivi, kwa mfano unaweza kuwa una kazi ambayo unataka kuifanya sasa hivi lakini wakati huohuo unakuwa unapenda kuongea na rafiki yako kwenye simu au unataka kuperuzi kwenye mtandao. Kwa namna yoyote ile unaweza ukajikuta unaahirisha hiyo kazi unayotaka kufanya ambayo ni muhimu kwako na kuamua kuongea na huyo rafiki yako.

Kwa kufanya hivyo utakuwa moja kwa moja umependa kufurahia maisha ya sasa na kuweza kusahau kazi yako ambayo pengine ni muhimu sana kwa faida ya baadae katika maisha yako. Hivi ndivyo inavyotokea na wengi ndivyo huwa wanajikuta wanaarisha mipango na malengo yao mazuri waliojiwekea siku hadi siku.
Unaweza ukatambua ambavyo mtu kwake inaweza kuwa rahisi kuweza kutumia pesa zake hovyo kwa sababu ya starehe za leo na za muda mfupi na kusahau kujikita katika suala zima la uwekezaji. Hiyo yote inakuja kwa sababu ya kupenda kufurahia maisha ya sasa na kusahau kabisa maisha  ya kesho ambayo yanaweza kuwa ni msaada mkubwa kwake.
Hivyo, mtu kwa hali hiyo hujikuta akisema nitafanya hili kesho ama kesho kutwa na kupelekea siku nyingi kuweza kusonga mbele bila kufanya ama kubadili chochote katika maisha yake. Jaribu kuchunguza hili kwa makini utagundua ninachosema hapa, mara nyingi unapenda kuahirisha mambo kwa sababu ya starehe fulani fulani za leo au uvivu, huu ndiyo ukweli.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kukabiliana Na Changamoto Katika Maisha Yako.

Ili uweze kuondokana na hali hiyo unatakiwa utambue kuwa  uhuru unaotaka sasa au starehe, pengine unazozifanya na ambazo zinakupelekea wewe kuacha majukumu haziwezi kukufikisha popote. Elewa kabisa maisha yako unatakiwa kuyajenga wewe mwenyewe na siyo mtu mwingine. Jifunze kutokuharisha mambo yako kwa gharama yoyote ile.
Kama si hivyo jifunze kuangalia faida ya jambo hilo ikiwa hutaweza kuariahirisha. Angalia matokeo chanya ambayo utayapata kwa kutokuahirisha kitu unachokifanya. Kama utaendelea kuahirisha mambo yako utakuwa unajiwekea vikwazo wewe mwenyewe vya kufikia mafanikio yako.
Ansante kwa kwa kuwa msomaji mzuri wa DIRA YA MAFANIKIO, endelea kuwashirikisha wengine kuweza kujifunza zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 04 80 35,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.