google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 11, 2015

Kama Unaendekeza Tabia Hizi, Umaskini Kwako Utakuwa Ni lazima.

No comments :
Tabia tulizonazo mara nyingi ndizo zinajenga maisha yetu na kuweza kukutambulisha au kutupa ishara halisi ya kuwa sisi tunaweza tukawa akina nani baada ya muda fulani. Zipo tabia ambazo tukiwa nazo zinatupa uhakika wa sisi kuwa na mafanikio na zingine tukiwa nazo zinaturudisha nyuma kabisa hadi kwenye umaskini.
Je, umeshawahi kujiuliza kwa nini mara kwa mara huwa inatokea unajikuta huna pesa na hata pia ‘account’ yako nayo inakuwa haina kitu? Pengine umekuwa ukiuumiza kichwa na kujiuliza ni wapi ulipokosea hasa? Kitu ambacho umekuwa hujui unakuwa katika hali hiyo wakati mwingine kutokana na tabia ulizonazo.
Tabia ulizonazo zina nguvu ya kuweza kubadili au kutengeneza maisha yako kwa kadri jinsi unavyozitumia. Katika makala hii tutaaangalia tabia mbaya ambazo nyingi ya hizo ukiwa nazo uwe na uhakikia huwezi kufanikiwa katika lolote zaidi ya kuwa maskini. Ni tabia ambazo zimewaathiri wengi bila kujijua.
Fuatana nasi katika makala hii kuzijua zaidi:-
1. Tabia ya kutumia pesa zaidi ya kipato ulichonacho.
Kama unatumia pesa hizo kwa kuwekeza upo sawa. Lakini kama unafanya matumizi makubwa zaidi ya kipato chako, tambua na elewa kabisa upo kwenye mstari mwekundu wa kuelekea kwenye umaskini tena wakujitakia. Wengi wenye tabia hii huwa ni watu wa kuishi kwa madeni kila wakati na hali zao kifedha daima huwa ni mbaya siku zote na maisha yao huishia pabaya.
Nini cha kufanya?
Ili uweze kuondokana na hali hiyo jiwekee kiapo cha kutotumia pesa zaidi ya zile unazopata. Kaa chini kisha tafakari, na amua kuwa na matumizi tu ya kawaida ambayo hayataweza kukugharimu na kukuharibia maisha yako kwa ujumla.

SOMA; Tabia 8 Muhimu Unazotakiwa Kuwa Nazo, Ili Kujenga Maisha Ya Mafanikio Makubwa.


 2. Tabia ya kushidwa kujiwekea akiba.
Kinaweza kuwa ni kitu cha kawaida kwako lakini ni hatari kwa afya ya mafanikio yako. Kama utaendelea kuwa na maisha ya kuwa unapokea tu pesa halafu unashindwa kujiwekea angalau kiasi kidogo ambacho kinaweza kukusaidia kwa baadae uwe na uhakika pia kufanikiwa kwako itakuwa kugumu kidogo hata kama hutaki kukubali ukweli huu.
Nini unachotakiwa kufanya sasa?
Anza kujiwekea utaratibu wa kujiwekea pesa zako wewe mwenyewe. Kiasi chochote cha pesa unachopata tenga asilimia fulani ambayo utaiweka. Inaweza ikawa asilimia kumi ambayo itakusaidia katika shughuli nzima ya kuwekeza kwa hapo baadae pesa hizo zitakapokuwa nyingi tayari.
3. Tabia ya kutokujiwekea kumbukumbu.
Wengi wetu mara nyingi huwa tunatabia ya kutokuweka kumbukumbu hususani kwa pesa tunazozitumia. Huwa ni watu makini kwa baadhi ya matumizi lakini ukweli unakuja palepale kuwa matumizi mengine ya pesa hasa yale madogo madogo huwa hatupo makini nayo hali ambayo huweza kutupelekea kupoteza pesa nyingi bila sababu.
Nini cha kufanya?
Ili kuweza kuondokana na tabia ya kupoteza pesa hovyo ni vizuri tukajiwekea utaratibu ambao utakuwa unaweka kumbukumbu kwa kila shilingi unayoitumia. Kwa kuweka kumbukumbu hizo itakusaidia kuweza kuepuka matumizi yasiyoyalazima kwako.

SOMA; Ili uweze Kufanikiwa, Una Haja Ya Kujifunza Zaidi Juu Ya Kitu Hiki Katika Maisha Yako.

4. Tabia ya kutokujiwekea bajeti.
Pesa yoyote ambayo inatumika bila kuwa na bajeti maalumu siku zote huwa inatumika hovyo tu. Watu ambao wanaishi maisha ya kutojiwekea bajeti huwa ni watu wa kutumia pesa kiasi cha kwamba huwa inafika mahali hawaelewi hizo pesa zao zimekwenda wapi. Kutokana na hali hiyo huwa ni sababu tosha ya kuwapeleka kwenye njia ya kuelekea kwenye umaskini bila hata wao kujitambua.
Kitu gani cha kufanya?
Kitu pekee cha kufanya hapa ni kuhakikisha unatengeneza utaratibu wa kujiwekea bajeti na kuhakikisha ni lazima unaifata. Kwa kufuata bajeti hiyo ni lazima utafanikiwa na utaondokana na matumizi ya hovyo ambayo ni rahisi kwako kuweza kukurudsha kwenye umaskini.

SOMA; Kama Unataka Kufanikiwa Na Kuwa Tajiri, Acha tabia Hizi.

5. Tabia ya kutokujali sana mambo ya leo.
Ili uweze kujihakikishia mafanikio yako ya kesho unahitaji kufanya mambo yako kwa ubora zaidi kila siku. Kama leo utafanya vizuri zaidi ya jana na kesho ukafanya vizuri zaidi ya leo uwe na uhakika hakuna mtu wala kitu kitakachoweza kukuzuia kwenye njia kuelekea ya mafanikio. Wengi huwa wanashindwa kufanikiwa kutokana na kutokujali hilo.
Wengi ni watu wakijikuta ni wa kusema kuwa  nitafanya hiki na kile kesho ama siku nyingine na kujisahau kabisa kuwa leo ni siku muhimu kwa mafanikio yao kuliko wanavyofikiri. Kwa kutokujali leo hivyo hujikuta ni watu wasio na mafanikio katika maisha yao kwa sehemu kubwa sana.
Kitu cha kufanya ni nini?
Ni muhimu kutambua kuwa leo ni msingi wa mafanikio yako makubwa ya kesho. Kwa kulitambua hilo fanya kazi kwa bidii zote kama leo ndiyo siku yako ya mwisho. Acha kukata tamaa na wala usichoke, ongeza na kuchochea bidii zote. Kwa kutekeleza hayo uwe na uhakika ni alazima utafanikiwa.
Tunakutakia kila la kheri katika safari ya mafanikio, endelea kuwashirikisha wengine kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kila siku kwa kujifunza na kuhamasika zaidi.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
§  0713 04 80 35,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.