google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 19, 2015

Siri 6 Za Mafanikio Ya Mjasiriamali.

No comments :
Ili uweze kufanikiwa ukiwa kama mjasiriamali unahitaji kuzijua siri ama mbinu muhimu za kuweza kukupa mafanikio hayo. Mbinu hizi zitakusaidia kukuongezea maarifa  ambayo yatakupelekea kufanya shughuli zako kwa ufanisi  na kukupa mafanikio unayoyahitaji.
Ni mbinu ambazo ambazo zinatumiwa na wajasirimli wengi wenye mafanikio makubwa duniani kote. Kwa hiyo ni muhimu hata kwako wewe kuweza kuzitimia. Na mbinu au siri hzi zipo za aina mbalimbali ambazo mjasiriamali anatakiwa kuzitumia ili kujipatia uhakika wa mafanikio zaidi.
Zifuatazo Ni Siri 6 Za Mafanikio Ya Mjasiriamali.
1. Kauli nzuri za kumjali mteja.
Moja kati ya sumu kali katika biashara yoyote ile ni kutokumjali mteja. Kwani kwa kauli yako unaweza kumfanya mteja wako akawa ni wa kudumu katika biashara yako au kumfukuza kabisa mteja huyo.
Wengi hufikiri kuwa asipomridhisha mteja mmoja haina tatizo kubwa katika biashara yake. Lakini ukweli ni kwamba mteja huyo mmoja ana nafasi kubwa ya kukutangazia biashara yako, kwa kadri utakavyomhudumia vizuri ndivyo atakavyoshawishi wengine waje kwenye huduma yako.
Acha kutumia kauli za matusi badala yake tumia maneno mazuri, yenye mvuto mbayo yatamfanya mteja wako ashawishike kurudi kwako tena. Kujali mteja siyo lazima uwe mwongeaji sana, bali waweza kutumia maneno machache kama ‘karibu dada, au samahani’ na mengineyo. Hii ndiyo siri mojawapo ya mafanikio kwa mjasiriamali.

2. Uaminifu.
Uaminifu ni moja kati ya nguzo muhimu sana kwa mjasiriamali yoyote Yule. Inabidi mjasiriamali awe mwaminifu kwa wadau wote husika, yaani kwa wateja wake, anakochukulia bidhaa zake, wafanyabiashara wenzake, taasisi za fedha, serikali na washirika wake wote.
Unapokuwa mwaminifu unakuwa unazidi kushirikishwa mambo mengi ya kijasiriamali. Hata mafanikio ya wajasiriamali wengi wenye mafanikio yametokana na uaminfu. Uaminifu ni moja ya kati ya mambo yanayotangaza biashara kwa kiasi kikubwa sana. Hivyo matunda ya kesho katika ujasiriamali yanatokana na uaminifu unaounyesha kila siku.
3. Kujali muda.
Katika karne hii ya syansi na teknolojia watu wengi huzingatia sana muda ili waweze kukamilisha mipango yao katika muda unaohitajika. Hivyo kitendo cha kumpotezea mtu muda wake unamuuingizia hasara kubwa sana. Pengine hujui muda huo kidogo mtu huyo angeingiza kiasi gani cha pesa.
Kwa hiyo kwa mjasiriamali ni vyema akawa wa kisasa zaidi kwa kuzingatia muda katika shughuli zake za kila siku. Ni muhimu sana kuheshimu ahadi ulizopanga na wateja wako na hata wafanyabiashara wenzako. Muda unachukua nafasi kubwa katika maendeleo binafsi ya mjasiriamali.
4. Utafiti wa bei na masoko.
Moja kati ya mambo yanayoweza kupunguza kasi ya mauzo ya mjasiriamali ni bei ya bidhaa zake kutofautiana kwa kiasi kikubwa na jirani zake. Utakuta bei ni ileile lakini kila mtu amejipangia bei yenye tofauti kubwa na jirani zake. Wengine bila uoga hupanga bei mara mbili au tatu zaidi ya jirani zao.
Wateja wanapoanza kukimbia mtu hufikiri anamkosi, wenzake wanamfitini au amerogwa! Lakini kumbe sivyo. Bei zako mbaya ndizo zinaweza kuwa chanzo cha kukimbiza wateja. Kwa hiyo unapopanga bei ni muhimu kuangalia mambo kama tafiti za jirani zako wanauzaje au uimara wa bidhaa zako.
5. Kubana matumizi.
Ili upate faida nzuri katika biashara yako, suala la kubana matumizi ni muhimu sana. Yako maeneo mengi ambayo mjasiriamali anaweza kubana matumizi bila kuathiri mwenendo wa biashara yake.
Katika kubana matumizi hakikisha unabana matumizi bila kuharibu ubora wa bidhaa ila jalli sana matumizi ambayo siyo ya lazima kwako kuyafanya katika biashara yako. Na pia biashara yako ifanye isije ikabeba matumizi yako mengi binafsi, badala yake jipangie mshahara.
6. Usafi.
Moja kati ya vivutio muhimu kwa wateja ni usafi. Wateja hupendelea kununua bidhaa au kupata huduma katika sehemu na wahudumu walio safi. Hivyo, inatakiwa mjasiriamali azingatie usafi katika maeneo kama eneo la biashara, usafi binafsi na bidhaa ziuzazwo au zizalishwazo.
Lakini kama eneo lako la biashara litakuwa linaendelea kubaki chafu hadi kusubiri eti Bibi afya aje akague, tayari utakuwa umeshapoteza wateja wengi. Tambua kuwa unapoimarisha usafi katika biashara yako ndivyo unavyoongeza idadi ya wateja wako.
Kwa kadri mjasiamali anavyojua siri hizo, ndivyo hujikuta katika nafasi nzuri ya kufanikiwa.
Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya ujasiriamli na endelea kutembelea DIRA YAMAFANIKIO kujifunza na kuhamasika zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.