google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 15, 2015

Njia 6 Muhimu Za Kukusaidia Kuitawala Hofu Inayokukabili Katika Maisha Yako.

No comments :
Habari za leo mpenzi msomaji wa mtandao huu wa DIRAYA MAFANIKIO, ni matarajio yangu ya kuwa umzima na upo tayari  kwa siku nyingine tena kwa ajili ya kujifunza kitu kipya cha kuweza kubadili maisha yako. Katika makala yetu ya leo tutaangalia namna tunavyoweza kuzitawala hofu zetu  zinazotukabili mara kwa mara katika maisha.  
Mara nyingi katika maisha yetu hofu huwa inaonekana ni kama kitu cha kawaida kwa binadamu kwa sababu tu, kila mtu inampata. Wengi wetu bila kujijua huwa tuna hofu za aina mbalimbali ambazo huwa zinatukabili. Hofu hizi huwa zinatofautiana kulingana na mtu mmoja na mwingine. Hofu hizi kwa wengine huwa ni kubwa zaidi na kwa wengine  ni za kawaida tu.
Wapo ambao huwa ni watu wa kuogopa sana juu ya kesho yao wakiwa hawaelewi nini hatima ya maisha yao ya kesho, wapo ambao huhofia sana kazi zao wakiwa hawana uhakika wa ajira zao na wapo pia ambao huhofia juu ya kifo na mengineyo mengi. Ukichunguza utagundua hizi ni baadhi ya hofu chache, kati ya nyingi ambazo wengi huweza kuwa nazo katika maisha yao.
Lakini hata hivyo ikumbukwe pia hofu hizi mara nyingi huwa zinasababishwa ama kuzalishwa na jamii yetu tunamoishi. Kwenye jamii ukiangalia  zipo hofu nyingi ambazo huwa tunapewa kama ‘wewe hufai katika hili,’ huwezi kufanikiwa’ na nyingine chungu nzima na matokeo yake tunajikuta ni watu wa hofu kila kukicha.
Sasa tunawezaje kuzitawala hofu hizi na kuishi maisha ya amani?
1. Kuwa makini na mambo yanayokupa hofu.
Ni muhimu sana kuwa na makini na yale mambo yote yanayokupa hofu sana. Jaribu kufakari na kujiuliza ni kipi kinachokufanya wewe kuwa na hofu zaidi. Na pia jiulize tena ikiwa utaachana na hofu hizo nini ambacho utakipoteza? Kwa kifupi, utagundua hofu nyingi ulizonazo ni wewe mwenyewe umeamua kuzishikiria na zinakutesa bure.

SOMA; Mambo MuhimuYa kukusaidia Kukupa Furaha Katika Maisha Yako.



2. Tambua kila mtu ana hofu zake.
Unaweza ukawa unahofu kwa sababu ya kuogopa kushindwa kitu ulani . Hiyo inaweza ikawa ni sawa lakini kitu cha kutambua kwako ni kuwa kila mtu kwa namna moja ama nyingine huwa anashindwa kwa sehemu yake. Kama ni hivyo ni lazima kwako wewe kuweza kumudu hofu zako na kuacha kuogopa kila kitu bila sababu ya msingi.
3. Jifunze zaidi mambo chanya.
Hii ni njia mojawapo rahisi ya kuweza kukabiliana na hofu kwa urahisi. Unapojifunza vitu chanya utajikuta ule woga uliokuwa nao unapungua siku hadi siku. Unaweza kujifunza kupitia nukuu za mafanikio ama vitabu au blog nzuri zinazohamisisha kama DIRA YA MAFANIKIO na AMKA MTANZANIA. Kwa kufanya hivyo utajikuta hofu ulizonazo unakuwa sasa unauwezo wa kuzitawala. 

SOMA; Mambo 5 Unayoyapoteza Katika Maisha Yako Kwa Sababu Ya Kuwa Na Hofu.

4. Jaribu kufanya mambo mapya.
Inawezekana mfumo wa maisha unaoishi nao wa kufanya mambo yale siku hadi siku ndiyo unaokupa hofu. Jifunze kufanya mambo mengine mapya ambayo yataweza kukuongeza ujasiri na nguvu ya kuweza kuikabili hofu uliyonayo. Kwa kufanya hivyo utajikuta unaitawala hofu yako na kuwa na maisha ya tofauti na ambayo unayo sasa.
5. Sikiliza mziki unaokupa matumaini.
Ni vizuri kusikiliza muziki ambao unakupa matumaini na faraja katika maisha yako ya kesho. Acha kusikiliza mziki tu kwa sababu upo kwenye kifaa cha kusikilizia. Kwa kusikiliza miziki hii itakupa nguvu kubwa ya wewe kuweza kusonga mbele pale unapokuwa na hofu na kumudu kuzitawala hofu hizo kwa sehemu kubwa katika maisha yako.

SOMA; Hivi Ndivyo UnavyowezaKuongeza Thamani Zaidi Katika Maisha Yako.
6. Kuwa mtu wa matumaini.
Ishi maisha kwa kuamini kuwa hofu ulizonazo unaweza kuzishinda. Acha kuwa mwoga sana kupitiliza hiyo kwa vyovyote haitakuweza kukusaidia wewe zaidi ya kukupotezea kwenye njia ya mafanikio. Unapokuwa unaishi kwa matumaini inakuwa ni njia rahisi kwako ya kuweza kutawala hofu zinazokukabili.
Hizo ndizo njia muhimu unazoweza kuzitumia kuweza kuiondoa hofu inayokukabili katika maisha yako. Kwa makala nyingine zaidi endelea kufuatilia DIRA YA MAFANIKIO kujifunza zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,
dirayamafanikio@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.