google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 6, 2017

Mbinu Ziletazo Mafanikio Kwa Kasi Zaidi.

No comments :
Tatizo la Mafanikio limekuwa kilio kubwa, najua linawatesa wengi, ila afisa mipango ni zaidi ya suluhisho, endelea kusoma makala zake kupitia Dira ya Mafanikio. Naamini utaipenda.

Ni matumaini yangu u mzima wa afya na unaendelea na  kuimalika zaidi kupitia makala hizi za kimafanikio. Katika makala yetu ya leo tutakwenda kujikita zaidi katika kuangalia ni mbinu zipi ambazo ukiamua kuzitumia leo zitakwenda kubadilisha maisha yako. Mabadiliko ambayo nayazungumzia ni yale ya kiuchumi ambayo yamekuwa ni kilio kikubwa kwa watu wengi.

Tumekuwa walalamikaji wazuri juu ya maisha haya na kuona hatusongi mbele hii ni kutokana hatujui ni jinsi gani ya kuzitazama fursa ambazo zipo na zinatuzunguka. Na ukitazama kwa umakini utagundua ya kwamba nchini kwetu pana fursa nzingi sana ila tatizo kubwa linakuja katika uhusiano uliopo kati ya macho na ubongo katika kuziona fursa hizo kisha kuzifanyia kazi hatimaye kuweza kuondokana na sakata hili la umaskini.

Zifuatazo ndizo mbinu ambazo unapaswa kuzitumia ili kuweza kupata mafanikio kwa kasi zaidi;

1. Tengeneza fursa.

Kama utakuwa mfutialiaji mzuri wa makala zangu nilishawahi kuandika juu ya makala ambayo ilikuwa na kichwa kinachosema je unataka fursa nzuri maishani? Leo tena nitakueleza ambavyo   unavyoweza kujitengenezea fursa katika maisha yako. Huu ni ukweli usiofichika ya kwamba katika mazingira tunayoishi kuna fursa nyingi ila watu wengi bado hatuja stuka mapema.

Namkumbuka sana mwalimu wako wa masuala ya ‘problem solving’ hasa pale alipokuwa anatufundisha somo la fursa, kwani kila akitupa kazi za kufanya alikuwa anasema twende maeneo ambayo tunaishi tuangalie fursa kwani ndiko ziliko fursa za kimaendeleo. Kwa mara ya kwanza nilikuwa sielewi ana maanisha nini ila baada ya kufuatilia nikagundua ni kweli maeneo tunayoishi yana fursa nyingi sana.
Tengeneza fursa, zitakazokupa pesa ya kutosha.
Huo ndio ukweli ambao hauitaji hata mwanga wa tochi katika kuzitazama fursa katika mtaa ambao unaishi. Katika kuzitazama fursa angalia mtaani kwako kwa kufanya uchunguzi wa kina kuna changamoto gani baada ya hapo tafutia majibu ya changamoto hizo. Katika kuzitazama fursa wanasema ya kwamba kila changamoto ni fursa. Hivyo jambo la msingi la kufanya ni kwamba usizitazame changamoto kama tatizo, ila zitazame changamoto kama fursa kwako. Kuanzia leo ukifanya hivyo utakuwa ni miongoni mwa watu watakaokuwa na mafanikio makubwa kwa muda mfupi.

2. Kuwa na lengo mahususi.

Baada ya kujua ni changamoto zipi ambazo zinawakabili wanajamii mahali unapoishi na wewe ukazifanya kama fursa. Jambo la pili ni kuwa na lengo moja ambalo unalitaka kulifanya. Baada ya hapo ni lazima ujiulize je utatekelezaje fursa hiyo. Inawezekana baada ya kuona fursa uliziona nyingi basi ni muda wako muafaka wa kuchagua fursa ambayo utekelezaji wake haitakuwa ni mgumu na uanze kutekeleza mara moja na kwa haraka zaidi kabla watu wengine hawajaanza kuifanya kazi fursa hiyo. Kama umeamua fursa yako ni ya kibiashara , elimu, usafi, na nyinginezo nyingi chagua moja na weka juhudi za kutosha za kiutendaji.

Ni matumaini yangu makubwa umenielewa vizuri sana, kilichobakili ni kile ulichokisoma hapa kukiweka katika matendo. Pia inawezekana unaziona fursa na wewe huna pesa katika makala ijayo nitakwenda kukueleza ni kwa jinsi gani unaweza kuwapata wawekezaji kutoka nchi za nje ambazo watakusadia kuzitekeleza fursa. Usikosee hii nadhani muhimu zaidi.

Mwandishi; Afisa mipango Benson Chonya
Simu; 0757;909942
E-mail;
 
bensonchonya23@gmail.com



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.