google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 13, 2017

Jinsi Ya Kufanya Mambo Magumu Kuwa Rahisi.

No comments :
Ni rahisi kufanikisha jambo lolote, ikiwa jambo hilo utataanza kulifanya mara moja na kuacha kusubiri.
Ni rahisi kujifunza kitu kipya kwenye maisha yako, ikiwa utaamua kweli kujifunza kila siku.
Ni rahisi kutoka kwenye kushindwa, ikiwa kama utachukua jukumu la kujaribu tena na tena.
Ni rahisi kusogea hapo ulipo kimaisha, ikiwa utaweka nia na juhudi kubwa ya kutaka kutoka hapo ulipo na kwenda ngazi nyingine kimafanikio.
Ni rahisi kuwa na watu wanaokutia moyo, ikiwa wewe utaamua kuwa wa kwanza kuwatia moyo wengine kufanikiwa.

Ni rahisi kuweka akiba na kuanza kukuza utajiri, ikiwa kuanzia leo utaamua kuanza utekelezaji.
Ni rahisi kukamilisha lile jukumu ambalo linasemwa sana kwamba, haliwezekani, ikiwa wewe utaligawa jukumu hilo na kuanza kulifanyia kazi.
Ni rahisi kuongeza kipato chako, ikiwa utajifunza kuwekeza hata kama ni kidogo katika maisha yako.
Ni rahisi kuyafanya maisha yako yakawa na maana, ikiwa kila siku utachukua jukumu la kufanya mabadiliko kidogo kidogo.
Maisha yako yanaweza kuwa kama unavyotaka yawe wewe, ikiwa wewe kwanza utachukua jukumu la kuyafanya maisha yako yakawa rahisi.
Acha kufanya mambo au maisha yako yakaonekana magumu sana hasa kwa zile hali ambazo ulikuwa unaweza kuzibadili kabisa.
Kumbuka, Ni rahisi kuanza jambo jipya, ni rahisi kujaribu tena pale uliposhindwa, ni rahisi kufikiri jinsi utakavyofanya maisha yako yakawa bora zaidi, sasa jiulize ni wapi unaposhindwa?
Kwa jinsi unavyofanya kidogo kidogo kwa yale mambo yanayoonekana magumu, siku hadi siku, kuna wakati utakamilisha mambo hayo magumu na hutaweza kuamini.
Kila wakati Jifunze kufanya mambo magumu kuwa rahisi.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,
dirayamafanikio.blogspot.com  

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.