google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 22, 2017

Maeneo Unayotakiwa Kuwajibika Sana Ili Kujenga Mafanikio Makubwa.

No comments :
Kati ya kitu ambacho unatakiwa uelewe katika safari yako ya mafanikio ni kwamba, mafanikio yoyote unayoyatafuta yanaanza na wewe. Hiyo ikiwa na maana, hakuna mtu mwenye hamasa kubwa ya kufikia  mafanikio yako zaidi ya wewe.
Kwa hivyo, hiyo inatuonyesha kwamba ili ufanikiwe, unatakiwa kuwajibika katika maisha yako kwa nguvu zote na kwa asilimia zote. Ikiwa hutafanya hivyo utajiangusha mwenyewe, maana hutaweza kufanikiwa.
Kupitia makala haya nataka nikupe dondoo za kukusaidia kujua maeneo ambayo unatakiwa uwajibike kwa uhakika ili upate mafanikio unayoyahitaji. Bila kupoteza muda tufuatane pamoja katika makala haya kujifunza;-
1. Wajibika kufanya maamuzi sahihi.
Kabla hujafanya kitu chochote ni lazima ufanye maamuzi. Na kufanya maamuzi ya kuweza kubadili maisha yako kuna wakati huonekana ni kitu kigumu sana.
Lakini hakuna namna nyingine zaidi ya kujua unatakiwa ufanye maamuzi yatakayobadilisha maisha yako. Pia  inatakiwa ujue bila kufanya maamuzi bora ya kukufanikisha itafika mahali utakwama.

Wajibika katika kila eneo la maisha yako kwa ukamilifu.
2. Wajibika kuweka mipaka ya maisha yako.
Ikiwa unataka kufika kule unakotaka kufika kimafanikio lazima ujue jinsi ya kuweka mipaka kwenye maisha yako. usiruhusu maisha ako yaingiliwe na kila mtu anavyotaka. Weka mipaka maeneo muhimu.
Jifunze kuweka mipaka kwenye matumizi ya pesa zako, nguvu na hata muda wako pia. Usiogope kuweka mipaka yoyote ile, ni muhimu kufanya hivyo ili kupata mafanikio. Kama hutajiwekea mipaka itakusumbua sana kufanikiwa.
3. Wajibika kukabiliana na mabadiliko.
Tunaishi katika dunia inayobadiilika sana. Ili kuweza kwenda sawa na dunia hii inatakiwa ifike mahali ukakubali kuwajibika ili ikusaidie kwenda sambamba na mwendo kasi wa dunia.
Kama hutaweza kukabiliana na ushindani, elewa  kabisa utashindwa. Njia bora ya kuweza kukabiliana na ushindani ni kujifunza kila siku na kujua maisha yanataka nini kwa sasa.
4. Wajibika kuwa mkarimu.
Ni rahisi kufika ngazi ya juu kimafanikio ikiwa wewe mwenyewe utakuwa mkarimu. Unapokuwa mkarimu unajenga uaminifu mkubwa kwa watu na hiyo inakusaidia kushirikiana katika mambo mengi ikiwa pamoja na biashara.
Kiuhalisia hakuna mafanikio ambayo unaweza kuyapata kiurahisi kama ikiwa hutaweza kuwajibika katika hayo maeneo. Kila wakati hakikisha unawajibika vizuri katika maeneo hayo ili ujenge mafanikio makubwa na ya uhakika.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.