google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 27, 2017

Malezi; Watoto Wasitumike Kama ‘Risasi’ Za Kushambuliana Sisi Wenyewe.

No comments :
Mfumo dume umekuwa na mwelekeo wa kuchochoea utoaji wa talaka kwa wana ndoa kirahisi sana. Utakuta wanaume huamua kuwapa talaka wake zao hata kwa makosa madogo madogo tu.
Na wanapofanya hivyo huhakikisha kuwa akina mama hao hawaondoki na kila kitu. Mara nyingi wamekuwa wakiondoka bila chochote, msaada wowote na hata bila watoto wao.
Wengi wetu tumekuwa hatushituki, tunapowaona wanandoa ambao walikuwa wakipendana wakipeana talaka. Na vile vile tukiwawekea utaratibu wa kuwasaidia wanandoa wanao achana, ili waweze kupona kihisia na kiakili.
Lakini, jambo la kukumbuka ni kwamba, unapompa talaka mwenzako, maana yake unamkana na kuondoa msamaha wako, upendo wako, na uaminifu wako kutoka kwake.

Pia, kuishi maisha ya useja ni jambo lililogumu hata zaidi. Iwapo wewe bado ni kijana na damu yako inachemka, kuishi maisha ya peke yako kunakufanya ukose usalama, uwe na hofu ya kukufanya upate maradhi yatokanayo na hisia. Lakini, pia upweke na kadhia zingine nyingine huwezi kuvikwepa.
Ni kweli kuwa, ndoa ni jambo jema na linalokubalika na jamii. Lakini iwapo ndoa itakuwa na matatizo au migogoro, wanandoa watapaswa wafanye nini? Ukweli ni kwamba, ni lazima pawepo na mlango wa nyuma wa kutokea. Tunapaswa tukumbuke kwamba, tunapoona kuna kitu kinachoitwa talaka, tujue tunapoelekea si pazuri.
Kuufahamu ukweli huu kutakusaidia tuepukana na matatizo, sisi na watoto wetu. Ingawa lengo si kutalakiana, lakini dunia yetu hii ni kubwa, na lolote lile linaweza kutokea.
Vilevile ukweli ni kwamba, wanandoa wanapotalikiana huendelea kubaki na maumivu au mateso kwa miaka mingine ipatayo kumi. Hali huwa mbaya zaidi kwa watoto.
Kwa mujibu wa kitabu kiitwacho Second chances kilichotungwa na kuandikwa na Sandra Blakeslee na Judith Wallerstein, ambao walifanya utafiti wa muda mrefu unaohusu madhara yanaotokana na talaka.
Katika utafiti wao wanasema kwamba, hata kama talaka itatolewa katika njia halali na ya haki, bado huo ni udanganyifu wa kihisia tu, kwani madhara yake huendelea kuwepo.
Pia wanasema kwamba, talaka ndiyo sehemu pekee katika maisha ambayo watoto hutumika kama risasi za kushambuliana sisi wenyewe, yaani mke na mume. Talaka ina maumivu makali kushinda matatizo  ambayo inajaribu kuyatatua.
Hata hivyo, jambo la kukumbuka ni kuwa, ndoa siyo kamilifu kwa sababu inaundwa na binadamu wasiokuwa wakamilifu. Licha ya ukweli huo, bado uwezekano upo kuboresha zetu. Na tutaweza kufanya hivyo, iwapo tutakuwa na uelewa wa kutosha unaohusu ndoa.
Ni Baraka ya aina yake ikiwa utaamua kusali na kujiandaa kwa ajili ya ndoa yako. Bila shaka kuna matatizo mbalimbali kwenye ndoa. Lakini iwapo kila mwanandoa atakubali kuwajibika kikamilifu, ndoa inaweza kuboreka kila mwaka, na kisha kuleta furaha, kuongeza na kukuza urafiki wa wanandoa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Tunakutakia kila la kheri,
Imani Ngwangwalu,
0713 04 80 35,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.