google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 16, 2017

Sababu 15 Zinazopelekea Kushindwa Katika Maisha Yako Wakati Wote.

No comments :
Kama wewe ni msomaji mzuri wa vitabu sina shaka na wewe, naamini umeshawahi kusoma kitabu cha ‘Think and Grow rich’ kilichoandikwa na Napoleon Hill miaka mingi ya nyuma.
Katika kitabu hiki mwandishi ameandika mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kukusaidia na  kukutoa kutoa kwenye umaskini hadi kuweza kufikia ngazi ya utajiri.
Hiyo haitoshi, Napoleon hill pia kupitia kitabu hiki, ameweza kuandika kwa ufasaha sababu 30 ambazo zinapelekea watu wengi kushindwa katika maisha wakati wote.
Kupitia makala yetu haya ya leo nataka nikushirikishe kwa ufupi baadhi ya sababu hizo muhimu ambazo hufanya maisha ya watu wengi kushindwa kufanikiwa na kuishi kwenye umaskini.
Zifuatazo Ndizo Sababu 15 Zinazopelekea Kushidwa Katika Maisha Wote.
1. Kukosa malengo maalumu.
Kama unaishi bila ya kuwa na malengo maalumu, hujui unapokwenda kwenye maisha ni sababu tosha itakayokufanya ushindwe katika maisha yako. Ishi kwa malengo ujenge mafanikio yako.
2. Kukosa nidhamu.
Hakuna mafanikio ambayo unaweza ukayapata bila ya kuwa na nidhamu. Inatakiwa uwe una nidhamu karibu katika kila eneo la maisha yako. Wengi wanaoshindwa katika maisha kiukweli hawana nidhamu.

3. Kuahirisha mambo.
Pia kuahirisha mambo inatajwa kama sababu ya kukufanya ushindwe katika maisha. Kama kuna jambo unataka kulifanya,hebu lifanye wakati huo huo. Acha kusubiri kesho utapotea.
4. Kukosa nguvu ya kushikiria.
Wengi nao wanashindwa kwa sababu hawawezi kunga’ng’ania. Ikiwa unataka kufanikiwa lakini huna maamuzi ya kuwa mbishi sahau mafanikio. Hii ni dunia inayotaka uwe mbishi kweli mpaka ufanikiwe kimafanikio.
5. Mtazamo hasi.
Hiki pia ni kikwazo kikubwa cha mafanikio kwa watu wengi. Kama wewe una mtazamo hasi, hauwezi kufanikiwa. Mafanikio yanajengwa kwa mtazamo chanya.
6. Kukosa maamuzi sahihi.
Ikiwa kila wakati huna maamuzi sahihi, kwa mfano, maamuzi ya kukusaidia kufanikiwa, tambua upo pia kwenye eneo la kushindwa kila wakati. Maamuzi bora ni nguzo au njia sahihi ya kukufanya ukafanikiwa wakati wote.
7. Woga.
Pia mwandishi ameeleza kwamba maisha ya wengi yamejawa na hofu sana. Sasa hiki nacho ni kikwazo kikubwa cha kuweza kufika mafanikio makubwa. Ni lazima kuishinda hofu ili kufikia mafanikio yoyote katika maisha yako.
8. Kujiwekea tahadhari sana.
Kuna watu ambao wao hawataki kukosea kabisa. Ni watu wanaotaka kuwa wako kamili kila wakati. Ili ufanikiwe ni muhimu ukajua kukosea pia ni ngazi ya kukusaidia kuweza kufanikiwa. Kosea, jifunze na songa mbele.
9. Kukosa nguvu ya uzingativu.
Inatakiwa mawazo yako yawe kwenye kile unachokifanya mpaka ufanikiwe. Kama mawazo yako unayapeleka sehemu tofauti huwezi kufanikiwa. Kwa kila unachokifanya, zingatia hapo kwanza.
10. Kukosa uvumilivu.
Maisha yanaenda sambamba na kuwa mvumilivu. Kuna wakati unaweza kukutana na magumu sana, lakini ukishindwa kuvumilia ndio basi tena huwezi kufanikiwa.
11. Kukosa ushirikianao na wengine.
Huwezi kufanikiwa kama huna ushirikinao mzuri na watu wengine. Mafanikio ni kutegemeana, hasa katika suala la kushirikiana. Ni muhimu sana kushirikiana na wengine ili kuweza kufanikiwa.
12. Kukosa mtaji.
Watu wengine pia wanashindwa kufanikiwa kwa sababu ya kukosa mtaji. Ingawa katika hili sio sababu kubwa sana kwa sababu unaweza ukajipanga na kisha ukapata mtaji baada ya muda fulani.
13. Kuishi kwa kuhisi sana.
Pia kuna wengine wanashindwa kufanikiwa kwa sababu ya kuishi kwa hisia. Utakuta badala ya kufanya jambo fulani kwa uhakika, mtu anawaza tu kwamba nitafanya kesho au hata nisipofanya hakuna shida.
14. Kuingia katika biashara isiyo sahihi.
Kama upo kwenye biashara ambayo haipo sahihi, pia ni rahisi kuweza kushindwa katika hilo jambo unalolifanya. Inatakiwa kuwa makini na kichagua biashara ambayo ni sahihi kwako na ambayo itakupa mafanikio.
15. Kuingia katika mahusianao mabovu.
Hakuna kitu kibaya kama kuingia katika mahusiano mabovu. Unapojiingiza katika mahusianao mabovu ni chanzo kingine kinachoweza kukufanya ukashindwa katika maisha yako.
Ukichunguza na kuangalia hizo ndizo sababu zinaweza kukufanya ukashindwa wakati wote, haijalishi unafanya nini kama una sababu hizo nyingi ni lazima utashindwa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.