google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 23, 2016

Fahamu Kwanini Kesho Si Rafiki Wa Mafanikio Yako.

No comments :
Katika maisha yetu ya kila siku, neno "Kesho" linatumika sana kama njia pekee ya kuahirisha mambo mengi, ambayo kimsingi yalitakiwa yafanyike "leo" . 

Kesho ni miongoni mwa maneno yanayopendwa kutumiwa kama kinga ya kukataa kutimiza majukumu fulani ya leo. Badala ya mtu Kusema "HAPANA" Kitu hiki, utakuta mtu huyo anajibanza nyuma ya kesho, Huku akidhani Kuwa ataweza kufanya au kutimiza majukumu ya leo siku ya Kesho. 

Matokeo yake, kesho ikifika anasogeza tena mbele kwa sababu kuna kesho nyingi mbele yake. Kwa maneno mengine ni kwamba, tunahitaji kujiadhari sana na "kesho" kwani bila kufanya hivyo, tutajikuta kwenye hali ya umaskini mkubwa sana bila kujua.

Ni Ukweli usiopingika kuwa neno baya kuliko maneno mengine na linaloongoza kwa kuharibu maisha ya binadamu ni neno liitwalo "kesho". 

Watu wengi hasa maskini, watu ambao hawajafanikiwa, wasiokuwa na furaha, na wale wasiokuwa na afya njema ni kundi la watu ambao upendelea sana kutumia neno " Kesho" .


Anza siku yako leo, kama hakuna kesho.
Ndiyo maana watu wa namna hii, mara nyingi hupendelea kusema maneno kama"nitaanza uwekezaji kesho au " nitaanza kutumia lishe bora kesho " au nitaanza mazoezi ya kupunguza uzito Kesho! Wengine husikika wakisema" nitaanza kusoma labda kesho.

Ukichunguza kwa undani unagundua kuwa neno "Kesho" linatumika sana kumaanisha kuwa jambo fulani litaanza kufanyika siku ambayo siyo ya leo. Ndiyo maana utasikia nitaanza hiki siku Ya kesho, wiki, mwezi, mwaka kesho au wakati ujao.

Kwanini Watu hupendelea Kusema Kesho?

Sababu ni moja tu kwamba tunayo HULKA ya kupenda kufanya Vitu vingi kwa mara moja na ambavyo haviko hata kwenye mpango maalum. 

Tunapenda sana kufanya kazi kwa kufuata kasi ya matukio yanayoendelea kutokea. Kwahiyo, mambo au shughuli za leo zinapozidi uwezo unaamua kuzipeleka siku ya kesho. 

Kwa mfano unaweza kukuta kwamba kufika saa sita mchana ya leo, Tayari umekwisha kuahirisha shughuli nyingi za leo na kuzipeleka kesho. Lakini uzoefu unaonyesha kuwa unapoona kitu hujakifanya leo, basi ujue siyo muhimu.

Kuhusu kitu gani muhimu ufanye leo, hakiji hivi hivi, ni lazima shughuli zako nyingi za kila siku zifanyike kwa kulenga ndoto yako ya maisha yaweza kuwa ni miaka mitano, kumi au na zaidi.

Bila kuwa na ndoto au maono juu ya maisha unayotaka kuyaishi, Lazima utaendelea kufanya kazi zako nyingi kwa kufuata matukio ya siku husika. 

Mwisho wake kila utakapofanya Tathmini ya miaka 5 au 10 iliyopita unajikuta umezidi kurudi nyuma, hapo ndipo utaanza kutafuta wa kumlaumu. Kuchanganyikiwa kwa Watu Wengi ambako huambatana na msongo mkubwa wa Mawazo, mara nyingi huja kwa njia hii.  

Kwahiyo, ni muhimu sana kwetu tunaotaka maisha huru ya mafanikio kutambua kuwa vitu vyote muhimu kwa maisha yetu ni inatakiwa vinavyofanyika leo. 

Maisha yako siyo kesho, wiki, mwezi, mwaka au miaka kumi ijayo bali maisha halisi, ambayo una fursa ya kufanya kazi itakayo kuletea mafanikio makubwa siku za mbeleni ni leo.

Ni muhimu tukafanya yale yote yaliyo muhimu leo. Ukishatambua hilo, utakuwa wa kwanza kuona umuhimu wa kuianza siku yako mapema Alfajiri. 

Kushindwa katika maisha yako hakuji siku moja bali ni matokeo ya kushindwa kidogo kidogo kila siku. Ukiona umeshindwa au unakabiliwa na umaskini usifikiri ni jambo ambalo limetokea leo bali ni kutokana Na wewe kuchezea yale masaa ya kuanzia unapoamka hadi unapolala.

Kwa hiyo kwa maneno au lugha rahisi "LEO Ndiyo Dili" kubwa ya kubadili maisha yako. Hii ikiwa na maana kwamba tukifanya kazi sana leo tutapata ushindi au mafanikio kidogo na kesho tukifanya kama au zaidi ya leo tutapata mafanikio Kidogo.

Yale mafanikio kidogo kidogo tunayovuna kila siku ndiyo kwa ujumla wake yatatufanya kuwa na mafanikio makubwa miaka 5 au 10 ijayo na hapo ndipo Wengi watakapoanza kukutambua kwamba na wewe huwa upo!

Jitahidi kuipenda na kuikumbatia leo na uachane kuwa na mpenzi wa kesho kwasababu, neno Hili linaharibu sana maisha ya watu wengi kuliko maneno mengine.

Achana na neno "Kesho" kwasababu haitatokea uione kesho. Kesho huwa haipo. Kesho huwa ipo tu kwenye akili za watu waota ndoto bila vitendo na washindwaji.

Nimalizie kwa Kusema Kuwa sijawahi kuiona "Kesho" Kitu tulichonacho Pekee ni "Leo". LEO ni neno la washindi na Kesho ni neno la washindwa.

Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

Makala hii imeandikwa na  Cypridion Mushongi wa MAARIFA SHOP.





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.