google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 9, 2016

Mbinu Bora Ya Kuishi Maisha Ya Ushindi Na Mafanikio.

No comments :
Kwa mwanamichezo yeyote yule, anajua vyema ili aweze kushinda ni lazima atambue mbinu sahihi ya kumwezesha kushinda. Hivyo, kutokana na kujua hilo mara nyingi wanamichezo wengi huwa wanaweka mikakati na kutafuta mbinu bora kila siku za kuwawezesha kuwa washindi.
Na mwisho wa siku kutokana na kutumia mbinu hizo ni kweli hujikuta ni washindi wa ndoto zao. Kama kwenye michezo iko hivyo, halikadhalika kwenye maisha ipo hivyo. Ili uweze kufanikiwa, inakulazimu ujue mbinu sahihi za kukuwezesha kufanikiwa.
Wale wote wanaojua maisha pia yanahitaji mbinu, daima hufanikiwa na kuwa washindi. Moja ya mbinu bora ambayo wale waliofanikiwa huitumia sana kuweza kufanikisha ndoto zao ni kule kuishi kwa kufuata ndoto zao.  Hii ni mbinu bora sana ambayo hata wewe unahitaji kuitumia.
Ikumbukwe mafanikio makubwa wakati wote yanaanza kwa kuishi kwa kufuata ndoto zako. Hutaweza kufikia ndoto zako hata kidogo, ikiwa utaishi maisha ya kutokufuata ndoto zako. Ni lazima ujue hasa ni kitu gani unachokitaka  hasa kwenye maisha yako ili uweze kufanikiwa.

Fuata ndoto yako mpaka ufanikiwe.
Katika kuifuta ndoto yako, ni lazima sana ujue ni kitu gani unakipenda. Ukishajua kitu hicho hakuna namna nyingine zaidi ya kujitoa na kuhakikisha unakifanikisha kwa gharama yoyote ile. Watu wenye mafanikio makubwa wanafuta ndoto zao kila siku.
Sasa ili uweze kuishi kwa kufuata ndoto zako, ni lazima ufanye mambo matatu muhimu. Jambo la kwanza unalotakiwa kulifanya ni kwa wewe kuhakikisha unaweka nguvu zako nyingi za uzingativu kwenye ndoto zako. Unapoweka nguvu zako kwenye ndoto yako kwa muda mrefu ni lazima utaifuata tu, hata kama hutaki.
Haijalishi una matatizo ya aina gani yanayokukabili wakati unaelekea kutimiza ndoto zako, lakini kitu unachotakiwa kufanya ni kuweka nguvu za uzingativu kwenye ndoto zako. Usipoteze muda wako kuwaza juu ya matatizo, waza jinsi utakavyofikia ndoto na malengo yako.
Ikiwa utatumia ngvu zako kufikiria juu ya changamoto unazokutana nazo utajikuta unakata tamaa. Lakini unapoweka nguvu ya uzingativu kwenye ndoto zako inakusaidia kukupa nguvu na kuona fursa nyingine zaidi. Usikubali kushindwa eti kwa sababu umekosa pesa, weka nguvu za uzingativu na kuamua kuifuata ndoto yako mpaka ufanikiwe.
Jambo la pili la kukusaidia ili kuweza kuishi kwa kufuata ndoto yako, ni lazima ujifunze kuandika ndoto yako na kuipitia tena na tena mpaka uone matokeo chanya.
Kwa uzoefu nilionao, washindi wote wanaandika malengo  yao na kuyapitia tena na tena kila siku. Na wengine huchukua jukumu la kuyasoma malengo yao kila wanapoamka, na hata pale wanapokwenda kitandani huyasoma tena.
Ikiwa utakuwa unayasoma malengo yako mara kwa mara au iwe umeyabandika ukutani, kwa kawaida unaongeza nguvu za kuweza kukusaidia kutumiza malengo yako na kuishi kwenye ndoto yako. Unaweza ukaanza leo kuyapitia malengo yako kila siku, ili ifike mahali uwe mshindi wa mafanikio.
Jambo la tatu la kufanya ili uweze kuishi kwa kuifuata ndoto yako ni kwa wewe kujiamini. Watu wote wenye mafanikio wana sifa kubwa ya kufanya mambo yao kwa kujiamini. Haijalishi jambo hilo ni kubwa vipi, ila hufanya mambo yao kwa kujiamini sana hadi kufanikisha.
Kujiamini ni nguzo kubwa sana ya mafanikio. Leo hii, ukitaka ufikie mafanikio makubwa anza kujiamini. Katika hali ya kawaida unapojiamini, unakuwa unaongeza nguvu na uwezo mkubwa wa kufikia mafanikio yako.
Ni lazima uanze kujiamini kwanza ili ufanikiwe. Ni lazima kwanza uwe mshindi kwenye akili yako, ili ufanikiwe kwa nje. Hii ni mbinu mojawapo nzuri inayokuwezesha kuishi maisha ya ushindi na mafanikio makubwa sana hasa pale unapoelekea kuifuta ndoto yako.
Kumbuka mbinu bora ya kukuweza kuishi maisha ya ushindi na mafanikio makubwa ni kwa wewe kuamua kuishi kwa kufuata ndoto zako. Kama ulikuwa bado huishi kwa kufuata ndoto zako, kumbuka kila kitu kinawezekana, na chukua hatua.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku. Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili uweze kujifunza. Kujiunga tuma neno MAFANIKIO YANGU, kisha ikifutia na namba yako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.