google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 20, 2015

Jinsi Ya Kutambua Kipaji Cha Mtoto Wako Na Kukiendeleza

No comments :
Hujambo mpenzi msomaji wa DIRA YA MAFANIKIO na karibu sana katika siku ya leo kwa ajili ya kujifunza. Leo katika makala yetu tutajifunza namna unavyoweza kutambua kipaji cha mtoto wako na kukiendeleza. Na tunapozungumzia kipaji  huu ni uwezo anaokuwa nao mtu wa kufanya jambo fulani bila hata kwenda kujifunza shuleni. Najua unaelewa hili vizuri.
Mara nyingi mtu huzaliwa na uwezo huo na anapokwenda shule inakuwa ni rahisi kuweza kuuendeleza kipaji hicho na kufanya jambo hilo kwa ufanisi sana. Sasa wewe kama mzazi unawezaje kutambua kipaji cha mwanao na kukiendeleza? Ili kupata majibu hayo ya nini unachotakiwa kufanya fuatilia yafuatayo katika makala hii;-
Kama mtoto wako anaongea kupita kiasi; Kuna watoto ambao huongea kwa spidi sana na huwa hawachoki kuongea. Watoto hawa huongea mpaka anapokwenda kulala na wengine huwa wanaongea mpaka usingizini. Huwa na tabia ya kusimulia visa mbalimbali au kukueleza mzazi yote yaliyotokea mchana pengine wakati wewe umeenda kazini au kwenye shughuli zako.

KUZA KIPAJI CHA MTOTO WAKO.
Kwa mfano unapokutana na mtoto wa aina hii, hiyo hapo ni dalili nzuri sana kwa watoto hawa kama kipaji chao kitaendelezwa vizuri na kutokana na mwenendo huo wanaweza kuwa  wanasheria, waandishi wa habari, wanasiasa pamoja na Mc wa majukwaani.
 Jinsi ya kuwasaidia watoto wa aina hii;
1. Epuka kuwakatisha tamaa kwa yale wanayoongea na kama yanakera mfundishe kuongea yanayofurahisha.
2. Unaweza kumwambia akusimulie visa mbalimbali wakati wewe ukimrekodi na baada usikilize pamoja nae. Hii humjengea kujiamini na kuona kuwa anachofanya kinathaminiwa.
3. Msaidie pia aweze kuwa msikilizaji mzuri kwa wewe kumsimulia wakati yeye akikusikiliza ana kumwambia arudie ulichosema.
4. Mtengenezee tabia ya kujiamini kwa kuepuka kumfokea au kumpiga mara kwa mara hususani kutokana na kosa la yeye kuongea sana.
Asante sana mpenzi msomaji wakati mwingine tutaangalia kipaji cha mtoto ambae kila jambo anataka kulifanya yeye mwenyewe.
Makala hii imeandikwa na Deo Mukebezi Unaweza kuwasilina naye kwa 0654627227



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.