google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 28, 2016

Jinsi Ya Kutengeneza Chili Sauce.

2 comments :
Kama utakuwa ni mfutialiaji mzuri wa mtandao huu, siku chache zilizopita tuliweza kukulete makala ambayo ilikuwa inahusu ni jinsi gani unaweza kutengeneza tomato souce, namshukuru Mungu kuna watu wengi walichukua hatua na sasa wameanza kutengeneza pesa kupitia utalamu huo wa utengenezaji wa tomato souce.

Nakusihi hata wewe ambaye unasoma makala haya leo uweze kuchukua hatua mathubuti juu ya somo hili la leo na kuona ni wapi ambapo na wewe utatengeneza pesa kupitia somo hilo, maana somo hili si kwa ajili ya kukupa hamasa bali ni kwa ajili ya vitendo na kutengeneza pesa, nakuomba urudie kwa mara nyingine kusoma aya hii, maana kiukweli somo hili ni hili ni pesa mkononi. 

Afisa mipango kwa moyo wa ajasiri nimeamua kukuletea somo hili ili nikutoe katika kundi la watu ambao wanalalamika kwamba Maisha magumu, ajira hakuna, mara serikali ya awamu hii inabana na sababu nyinginezo kama hizo, ambazo kwa upande wangu huwa naziona ni stori nyoka tu.

Weka maandalizi yako mapema.
Pasipo kumung'unya maneno, wala kushika simu yangu kuangalia kama kuna meseji au kuna mtu kanipigia, wala bila ya wewe kukuchosha nadhani niende moja kwa moja kwenye maada amabayo siku majawabu tosha ya wewe kupata pesa. 

Yafutayo ndiyo mahitaji kwa ajili ya kutengenezea chili souce;

a) Pilipili mbuzi nyekundu robo 1/4 kilo.

b) Nyanya kilo moja.

c) Kitunguu swaumu kikubwa kimoja.

d) Mafuta ya kula vijiko 7 vya chakula.

e) sukari vijiko viwili vya chai.

f)  maji ya moto kikombe kimoja cha chai.

g) vinega vijiko 3 vya chai.

Baada ya kuandaa mahitaji hayo ya jinsi ya kutengeneza chili souce, twende kuona moja kwa moja jinsi ya kutengeneza chili souce

HATUA YA KWANZA.

-Kata Pilipili kuondoa mbegu.

-menya nyanya kuondoa mbegu pia.

-menya vitunguu swaumu kisha
 vikatekate viwe katika vipande vidogo vidogo.

Nb; baada ya kumaliza hatua hiyo ya maandalizi chukua Brenda, kisha saga mchanganyiko wote wa malighafi ambazo nimezianisha kwenye hatua ya kwanza. Saga mchanganyiko huu mpaka uone imetoka rojo laini.

HATUA YA PILI.

Ukishamaliza kusaga mchanganyiko huu hapo juu jambo ambalo unatakiwa kulifanya ni;

*Chukua sufuria yenye nafasi ya kutosha kwa ajili ya kupika mseto huu.

*Weka sufuria yako jikoni, iache kwa sekunde kadhaa ili ipate moto pia kama kuna maji katika sufuria yaweze kukauka.

*Baada ya kuona sufuria yako imekwisha kupata moto, chukua mafuta ya kula yaweke kwenye sufuria, yaache yachemke.

* mafuta yakichemka chukua mseto wako mwagia katika sufuria yako, koroga mseto huo kuelekea upande mmoja kwa dakika 30 huku mseto huo ukiendelea kuchemka.

* Baada ya dakika 30 epua mseto huo na uuache upoe, kisha funga katika vifungashio kwani mseto huo utakuwa umeshakuwa chili souce.

Mpaka kufikia hapo utakuwa umekwisha kutengeneza  chili souce ambayo inafaa kwa ajili ya matumizi ya binadamu kwani ni salama kwa ajili ya afya yetu.

Endelea kufuatilia mtandao huu Wa DIRA YA MAFANIKIO kwani uongozi wa mtandao huu umeandaa masomo mazuri kwa ajili yako, ambayo yatakufanya uweze kufanikiwa katika maisha yako. 

Ndimi; Afisa mipango; Benson chonya
0757909942

2 comments :

Note: Only a member of this blog may post a comment.