google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 29, 2016

Unachokiamini Ndicho Unachopokea Na Kufanya.

No comments :
Mwanafalsafa mmoja aliwahi sema  “You cannot do beyond what you know and you cannot know beyond what you believe...therefore what you believe determines what you know and do”
Huwezi kufanya nje ya unavyojua na huwezi kujua nje ya unavyoamini...kwa hiyo unachoamini kinapelekea kujua kwako na kufanya kwako.
Hebu sisi tuchambue haya maneno muhimu matatu:-
Unachoamini.
Watu huamini tofautitofauti juu ya sababu za wao kuwa vile walivyo.Mwingine atakwambia yupo katika hali ya kushindwa kufanya vizuri kwa sababu ya mtu fulani,au jambo fulani lililowahi kutokea maishani mwake.
Mwingine anaamini kuwa ni kwa sababu tu bado hajachukua hatua ya kubadili hali yake. Huyu wa pili ana kheri ingawa wote wawili wapo sahihi kufikiria hivyo kwa sababu ndivyo wanavyoamini.
Kwa mujibu wa mwandishi Orison Swett Marden "What we sincerely believe regarding ourselves is true for us". Tunachokiamini kuhusiana na sisi wenyewe ni sahihi kwetu.
Unachokijua.
Kwa kawaida mwanadamu yeyote hawezi kufanya jambo bila kutafuta maana(they search for meaning) bila kujali chanzo cha hiyo maana na kama maana hiyo ni sahihi au sio sahihi...hutaka tu kuona anachofanya kina msaidia kwa namna fulani.
Maana yangu hapa ni kwamba ni muhimu kutumia asili hiyohiyo kutanua uwezo wa kujua ZAIDI ili kupata maana kubwa zaidi kuliko kuishia kung'ang'ania maana moja uliyoipata juu ya jambo husika.Kusoma vitabu,kuuliza na kusikiliza wengine kwa makini huongeza uwezo wa mtu kujua zaidi.
Unachofanya.
Mtu yeyote timamu lazima afanye jambo kwa kuangalia maslahi yanayotokana na kuwekeza nguvu yake hapo.Vinginevyo ataachana nalo na kuangalia ustaarabu mwingine.

Kwa hiyo kwa mtu mwenye lengo la kufanya vizuri iwe katika masomo, biashara, kilimo, michezo, mahusiano, ufundi nk ni muhimu kuzingatia ngazi hizo tatu muhimu zinazotegemeana LAKINI mlango mkuu ni kubadilisha UNACHOKIJUA.
Jenga tabia ya kutamani kujua vitu vipya, mbinu mpya na mwelekeo mpya ili uweze kufika unapotamani kufika siku moja.
Imeandikwa na Moses Mkemwa
(Uncle Moses)
0757717572


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.