google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 25, 2016

Sheria Tatu (3) Za Mafanikio (3 Laws Of Success).

2 comments :
Uhali gani mpenzi wa makala haya, ni matumaini yangu makubwa umzima wa afya kabisa, katika makala hii natakaka tujikite zaidi katika kujua  sheria ambazo zitatufanya tuweze kutimiza ndoto zetu.

Mara kadhaa umekuwa ukizoea kuona ya kwamba mahali palipo na sheria lazima pawe chombo au mtu wa kuzisimamia ili sheria hizo ziweze kutekelezeka kirahisi.

Lakini katika sheria za ya mafaniko huwa ni kinyume kwa sababu haina haja ya kuwepo chombo au mtu wa kukuongoza isipo kuwa wewe mwenyewe ndiye nahodha wa Maisha yako.

Maana tunaambiwa ya kwamba hatima ya maisha yetu tunayo wenyewe. Hiyo ina maanisha kwamba sheria za mafanikio zipo, uwe unajua au hujui, ila unapovunja sheria hizo lazima uadhibiwe na ulimwengu.

Leo katika makala haya, Afisa mipango nataka nikushirikishe na wewe sheria tatu tu za mafanikio. Ikiwa ikatokea ukazitumia sheria hizo uwe na uhakika utafanikiwa.

Zifuatazo Ndizo Sheria Tatu Za Mafanikio.

1. Fikiri (think).

Kila mwanadamu ana uwezo binafsi ambao amezaliwa nao kwa ajili ya kufiri, lakini fikra hizo hizo hutofautiana baina ya mtu mmoja na mwingine, hata siku moja hakuna mtu ambaye atafanana uwezo wa kufikiri na mtu mwingine.

Hata hivyo kila kitu chochote ambacho unakiona leo hii  yupo mwazilishi wa kitu hicho. Hapa ina maana ya kwanza yupo yule mwanzilishi wa kitu na yupo yule ambaye ni mtaalamu kwa ajili ya kufanya marekebisho ya kitu hicho andapo kitukuwa hakipo sawa.  

Vilevile katika kufanya vitu ambavyo tunaviona leo vinazidi kuwa katika ubora huohuo hutuna budi kutazama vitu hivyo katika jicho la tofauti sana, inawezekana bado hujanielewa ila ukweli ni huu upo utofauti mkubwa kati ya kufikiri na kuwaza.


Mara kadhaa endapo utamsikia mtu anasema nilitaka kufanya hiki na kile lakini hakijaenda kama alivyokuwa amepaga ujue fika mtu huyo ni alikuwa anawaza tu. Lakini ukweli ni kwamba ukitaka kufika kilele cha mafanikio yako huna budi kuweza kufikiri mambo kwa hali juu sana na sio kuishia kuwaza tu.

Unajua ipo hivi hapa ulimwenguni hakuna kazi ngumu kama ya kufikiri vitu vipya, na kama nilivyosema hapo awali ya kwamba kila binadamu ana uwezo wake binafsi ambao amezakiwa nao kwa ajili ya kufikiri, hapo sasa inategemeana ya kwamba unafikiria nini ?

Je ni mawazo chanya au mawazo hasi? Tafakari kidogo kisha ugundue juu ya jambo hili .Hata hivyo wapo baadhi ambao wamefanikiwa kimtazamo hata kimaisha watu hawa wao walifikiri mambo ya msingi katika mtazamo chanya, ndivyo hivyo ambavyo leo inatupasa mimi na wewe kuweza kutazama katika mtazamo huo huo ili tuweze kufanikiwa zaidi.

Kwa kuongezea pasipo kumung'unya mdomo wala kuharibu silabi za matamshi, kila kitu ambacho unakifijiria ambacho kipo katika mtazamo chanya huna budi kukiandika katika sehemu ambayo mara kadhaa utakuwa unakiona, kufanya hivi kutakufanya uweze kufikiri kwa kina zaidi ni kwa jinsi gani ambavyo unaweza ukakitekeleza kitu hicho. Mara kadhaa ukitaka kufanikiwa zaidi kumbuka kufikiri tofauti.

2. Panga (plan).

Jambo la pili ndugu msomaji wa mada hii, ni kwamba baada ya kufanya tafakari juu ya jambo lako huna budi kukaa chini na kutengeneza mpango kazi kwa ajili ya utekelezaji wa jambo hilo. Katika kupanga mpango kazi wa kile ambacho umekifikiria kitakupa picha kamili juu ya kile ambacho unatamani kukifanya, hii ikiwa na maana ya kwamba kitakuwa na matokeo chanya au matokeo hasi.


Kwa mfano labda unataka kufanya biashara, ni lazima uwe na mpango wa kibiashara (business plan) ambayo itakupa picha kamali ya jinsi ya biashara yako itakavyokuwa, kufanya hivi ni chachu ya kufika mahali ambapo unatamani kufika.

Pia yamkini unatamani kufanya jambo fulani kwa hapo mbeleni hivyo tumia muda huu kupanga mambo ya msingi yatayokwenda kukufanikishia jambo lako. Maana kuna usemi ambao unasema ukikosea kupanga mambo ya msingi umekwisha kufeli mambo yako.

3. Fanya (do).

Baada ya kufanya tafakari ya kina, pia baada ya kupanga namna ya kutekeza, jambo la tatu huna budi kuanza kutenda jambo hilo, si kutenda tu! Bali kutenda kwa njia tofauti na ulivyozoea kutenda au watendavyo watu wengine.

Pia kwa jambo lolote ambalo unataka kulifanya, au umekwisha kuanza kulifanya ili uone ya kwamba jambo hilo lina matokeo kiasi gani ni lazima ukipende jambo hilo haijalishi lina changamoto kiasi gani. 

Kwa mfano  unafanya biashara  haina haja ya kutumia nguvu katika kutafuta wateja bali unachotakiwa ni kuongeza thamani katika bidhaa au huduma, kufanya hivi wateja watakuja wao wenyewe, kwa sababu moja ya tabia ya wateja wengi wana tabia ya kuambiana hasa ni wapi ambapo hutolewa huduma nzuri. Narudia kusema tena penda kutoka ndani ya dhamira yako kwa jambo lolote ambalo unalifanya, maana hapa ndipo mzizi wa mafanikio yako ulipo.

Ni matumaini yangu makubwa ya bila shaka tumeelewana vizuri, na nikuhakikishe tu kwamba endapo ulichokisoma hapo juu utakwenda kukiweka katika matendo basi mafanikio yanakuja kwako kwa asilimia zote.

"Naamini katika kujifunza" kama na wewe unaamini hilo tukutane tena siku nyingine katika makala ijayo.

Ndimi; Afisa Mipango; Benson Chonya.
Phone no; 0757909942


2 comments :

Note: Only a member of this blog may post a comment.