google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 18, 2016

Mawazo Muhimu Unayotakiwa Kuwa Nayo Ili Kukuza Biashara Yako.

No comments :
Biashara shaka naongea na wewe katika siku hii ya leo ukiwa kwenye biashara yako au pengine ukitarajia kuanza biashara hivi punde. Kama uko kwenye biashara, pengine naongea na wewe ukiwa kwenye harakati za kutafuta wazo bora litakalo kusaidia kukuza biashara yako na kuwa ya mafanikio makubwa.
Kama uko kwenye hali ya kutafuta wazo bora litakalokusaidia kukuza biashara kwa kusoma makala haya itakusaidia sana. Ieleweke kwamba kuanzisha biashara na kuikuza biashara hadi ukaiona inaleta matunda ni vitu viwili tofauti. Wengi hujitahidi sana kuanzisha biashara lakini linapokuja suala la kukuza, hushindwa kwa sababu ya kukosa mawazo muhimu.
Kwa namna yoyote ile, mfanyabiashara anahitaji kuwa na mawazo muhimu yatakayomsaidia kukuza biashara yake  wakati wote. Haijalishi udogo au ukubwa wa biashara husika, lakini mawazo bora ni nguzo muhimu ya kuifanya biashara ikaendelea mbele na kutoa mafanikio makubwa.
Leo kupitia makala haya hebu tuangalie mambo gani muhimu unayatakiwa kuwa nayo ili kukuza biashara yako.
1. Tanua soko lako.
Biashara yako itaweza kukua ikiwa utakuwa una wazo la kutanua soko lako kila wakati. Kwa mfano, kama umekuwa ukiuza bidhaa zako ndani ya mtaa mmoja, ni vyema ukafikiri namna ya kuzipeleka na mtaa wa pili. Kwa wazo hilo litakusaidia sana  kukuza biashara yako kwa viwango vya juu.

Jenga mtandao wa kukuza biashara yako.
2. Pata maarifa ya biashara.
Kila wakati inabidi ujifunze kuunoa ubongo wako na kujifunza sana juu ya biashara unayoifanya. Maarifa ni muhimu sana katika kuikuza biashara yako, vinginevyo biashara hiyo ni lazima itadondoka. Hivyo, unatakiwa kujisomea vitabu au kuhudhuria semina mbalimbali za kibiashara ili kufanikisha hilo.
3. Toa huduma za ziada.
Unaweza ukaifanya biashara yako ikakuwa na kuwa ya mafanikio ikiwa utajifunza kutoa huduma za ziada. Kwa mfano, unaweza ukawapa wateja wako zawadi ndogo ndogo kila wanaponunua bidhaa. Hilo litawasaidia kuwavuta na kujikuta ukikuza biashara yako siku hadi siku.
4. Tengeneza mtandao wa kibiashara.
Huwezi ukasema unakuza biashara yako na kusahau kukuza mtandao wako wa kibiashara. Ni lazima kujitengenezea ‘netwek’ na wafanyabiashara wenzako ya kukusaidia kukufanikisha. Hilo litakusaidia katika kutatua changamoto na wakati mwingine hata kukuza bidhaa kwa urahisi.
5. Boresha bidhaa zako.
Mwisho, ili uweze kukuza biashara yako, kwa vyovyote vile unalazimika kuboresha bidhaa zako. Kila bidhaa unayoitoa ni lazima iwe ya viwango vya juu. Kwa hali hiyo itapelekea utapata wateja wengi kila kukicha  na kusababisha biashara yako kuweza kukua.
Ikumbukwe kwamba kutanua soko, kupata maarifa ya kibiashara, kutoa huduma za ziada, kutengeneza mtandao na kuboresha bidhaa kila wakati, ni moja ya mawazo muhimu ambayo unatakiwa kuwa nayo kila siku ili kukuza biashara yako.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku. Ila hakikisha unawashirikisha wengine waweze kujifunza zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.