google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 24, 2021

Jinsi Ya Kupata Wazo Bora La Biashara.

4 comments :
Kisaikolojia kila mtu ana mawazo bila kujali ni mazuri au mabaya. Wakati mwingine binadamu huwa na mawazo mazuri ambayo kama atayaendeleza na kuyafanyia kazi yanaweza kubadili kabisa maisha yake.

Mawazo humfanya mtu awe alivyo, aonekane vile anavyoonekana. Mwenye akili, mpole, mkorofi,mwema au mkatili. Haya yote ni matokeo ya mawazo aliyonayo mtu kichwani mwake.

Kila siku tunasikia watu wanasema nina pesa ila sijajua nifanye biashara au mradi gani. Wakati mwingine utasikia mtu akisema nina wazo zuri la kufungua biashara au mradi tatizo langu mtaji sina.

Katika kuwaza kwao watu hawa mwisho hujikuta muda umeenda, umri umesonga bila hata kutekeleza wazo moja alilopanga. Mwenye pesa amekaa na pesa hadi  imekwisha kwa kutatua matatizo ya aina mbalimbali.


Mwenye wazo kawaza mpaka kawazua mtaji hana na wazo limechina mwisho anakata tamaa na kuamua kufanya kazi asiyotaraji kuifanya ili kujikimu na mahitaji ya kila Siku katika maisha.

Ni Kitu gani kifanyike ili watu hawa waweze kufanikiwa? Mwenye wazo na mwenye pesa? usiumize kichwa Kisuda nitakupa siri yake leo. Kabla sijaeleza namna gani ufanye nikudokezee siri moja muhimu katika mafanikio.

Tafuta wazo sahihi la kukufanikisha.
Ili mtu yeyote iwe mimi au wewe uweze kufanikiwa unahitaji vitu vinne.

1. MAARIFA/UJUZI juu ya jambo unalotaka kufanya.

2. WAZO BORA NA  ZURI la kukuongoza hatua kwa hatua lenye taarifa sahihi juu ya mradi au biashara husika.

3. WATU WAZURI wa kushirikiana nao. Hakuna kazi au mradi unaoweza kuufanya peke yako ila kushirikiana na watu. Hivyo ni lazima upate watu makini na sahihi wa kushirikiana nao.

4. MTAJI /PESA ya kuanzishia mradi lakini zingatia kuwa pesa si chochote katika mradi au biashara hata uwe na mamilioni ya shilingi kama huna hivyo vitu vingine wazo,maarifa na watu sahihi sahau kuhusu MAFANIKIO utaangukia pua tu.
Kisaikolojia  pesa haileti mawazo, bali mawazo ndiyo huleta PESA. Na hii ndio Imani yangu na falsafa yangu Kisuda  katika maisha yangu ya mafanikio.


Sasa nitoe njia 5 za kuweza kukusaidia wewe rafiki yangu katika kupata wazo la biashara ili uweze kufanikiwa kirahisi kwa wewe mwenye pesa na mwenye wazo:-

1.Tafuta uhitaji wa watu/ tatizo linalowasibu watu kisha tafuta namna ya kuwatatulia shida /tatizo lao utapata pesa nyingi sana.

2. Boresha wazo la mwingine. Hapa ni kuangalia tu mapungufu ya mtu katika kazi au biashara halafu una boresha utendaji kazi na utaona mabadiliko makubwa katika kazi au biadhara yako. Kamwe usiige wafanyavyo wengine utapata matokeo yaleyale wapatao wao badili njia.

3. Hamisha wazo kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Hapa na maanisha ukiona mradi au biashara sehemu si lazima nawe ukafanyie pale unaweza anzisha wazo kama hilo sehemu tofauti na ukafanikiwa sana.

4. Rahisisha mchakato au upatikanaji wa huduma au bidhaa fulani badala ya watu kuifuata sokoni au mjini wapelekee wewe nyumbani kwao watakulipa pesa nyingi na gharama ya usafiri kwa nini wakulipe? Umewaokolea muda wao ili wafanye mambo mengine na pia wamepata wanachotaka kwa wakati.

5. Tengeneza uhitaji kwa watu. Hapa ni kubuni Kitu cha ziada ambacho watu wanakihitaji lakini kutokana na muda au umbali wanaona kama hakina umuhimu sana kwao. Mfano simu za mkononi zimekuja baada ya barua kuonekana kuchelewa kuwafikia wahusika leo hii taarifa ya dakika 10 imeshasambaa nchi nzima.

Haya sisi wataalamu tunaita ni kutengeneza mahitaji ya ziada kwa watu ili wakulipe pesa. UWEZO WAKO WA KUJA NA MBINU AU WAZO JIPYA TOFAUTI NA MAZOEA YA WATU NDIO CHANZO CHA MAFANIKIO YAKO.

Ansante kwa kutembelea DIRA YA MAFANIKIO na endelea kujifunza hapa bila kuchoka.

4 comments :

Note: Only a member of this blog may post a comment.