google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 2, 2015

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuongeza Thamani Zaidi Katika Maisha Yako.

No comments :
Je,  unathaminiwa  na   watu  katika  jamii? Kama  unathaminiwa  ni  mambo  gani  yanayokufanya uone  kuwa   unathiminiwa?.    Kama   unathaminiwa    ni mambo  gani  yanayokufanya  uhisi   hivyo? Moja   katika    mahitaji  muhimu   ya  binadamu   baada ya  chakula,  mavazi na  malazi  ni  kuheshimiwa  na  kuthaminiwa  na  jamii.

Binadamu  ni  kiumbe   pekee  aliye na  daraja  kuliko  viumbe   wengine  wote.   Kinachompandisha   hadhi   kuliko  viumbe   wengine  ni  uwezo  wake  wa   kufikiri,  ambao   umemwezesha   kuyatawala  mazingira  yake  na  kuyatumia  ili  kuboresha  maisha  yake.

Maendeleo  yetu  na  maisha  yetu  kwa  jumla  yanawategemea    watu.   Tunachohitaji  kutoka  kwao   ni  kututhamini,  kutujali  na  kutupenda.  Watu   watutathamini   kutokana  na  matendo  yetu  na  jinsi   tunavyoonekana  kwao.   Hii  ni   kwa  sababu  imethibitishwa  kuwa  watu  wenye     muonekano  wa  hali  ya  juu  mara nyingi    huwa   ndiyo  mwenye  mafanikio   katika maisha.

Licha    ya  muonekano   wetu  kufanya  kuthaminiwe  na  watu,   unadhifu  pia  huwa  na  uhusiano  na   fikra  zetu.   Ndiyo   maana  viongozi   wa  dini,  mashehe, mapadri, makasisi na  wachungaji  huvaa  mavazi  maalum    ambayo  huwafanya  wapate  hisia  fulani  za  mamlaka   katika  nafsi  zao.    Inasemwa   kuwa  hata askari   anapokuwa     anavaa   sare  za   jeshi heshima yake huwa juu zaidi.


Niliwahi    kusikia   kisa  cha  Ofisa  na   dereva  wake  waliokwenda  kwenye  sherehe.   Walipofika  waliegesha  gari    mbali na  ukumbi.    Hivyo  watu   hawakuwaona   jinsi  walivyokaa  kwenye  gari.    Kwenye  ukumbi  kulikuwa  na  msichana   aliyeandaliwa  kumvisha  mgeni  shada  la  maua.


 Ofisa   na  dereva   walipofika    mlangoni  yule  msichana   alikwenda  kumvisha   shada  la  maua   dereva  badala  ya  Ofisa  na  huku  watu  wakimshangilia  dereva   alivishwa  shada  la  maua  kutokana na  jinsi  alivyoonekana.  Alikuwa    amependeza  na  kuonekana  na  hadhi  kuliko  bosi  wake.

Kwa  hakika   siyo  sahihi  kumthamini   mtu  kwa  mavazi  na  muonekano  wake  pekee  kwa  sababu   kuna  mambo  mengine  muhimu  kama  vile  akili,    ujuzi  na  tabia.

Lakini  pia  tukumbuke  kuwa siku  zote   watu  hutupangia  thamani  kutokana  na  jinsi  tunavyoonekana    kwao  hasa  wanapotuona  mara  ya  kwanza.   Mwonekano   ndicho  kitu  cha  kwanza   ambacho   hudumu  zaidi  katika  fikra  za  mtu  anayetuona  mara ya kwanza.

Aidha hata hivyo  muonekano   huo   huweza kuwa na taswira   hata  katika  sifa   zetu  nyingine  ambazo  mtu  huweza  kuzigundua  baada  ya  kutuona  kwa mara  ya kwanza. Mara  ngapi  tumewahi    kuwasikia   watu  wakisema  “Mtu  kama  yule  hawezi   kutenda  jambo   la  kijinga  kama  hili”  kipimo     wanachokitumia  hapa   huwa   siyo   kingine  isipokuwa  anavyoonekana.

Je,   umewahi   kuchunguza   ni  watu  wa  aina  gani  ambao   huonekana   wanaheshimika  sana  kwenye   mkusanyiko   wa  watu  kama  vile  kwenye  kituo  cha  basi  sokoni  au  mkutanoni.   Utagundua  kuwa   wanaoheshimika   zaidi  ni  wake    walio  nadhifu. 


Kwa  kawaida   watu  huamini   kuwa  mtu  aliye  nadhifu  ni  mtu  wa  maana,  aliye  mwenye  akili,  msomi,   anaye  aminika  na  aliyefanikiwa  katika maisha.   Mtu  asiye  nadhifu  anayeonekana  mchafu  watu  humchukulia  kama  mtu  asiye  na  maana,  siyo   mwerevu,   siyo   makini  na  hajaendelea  kimaisha.

Lakini  mtu  mwingine   anaweza  kukata  tama  kuwa  hawezi  kuonekana  nadhifu   kwa  kuwa  hana  fedha   za  kuweza  kununulia  mavazi  ya  thamani.    Hata  hivyo,  ikumbukwe   kuwa    ili  mtu  aonekane  nadhifu  sio   lazima  avae    nguo   ghali.    Unadhifu    ni  kuvaa  nguo   safi    na  kuutunza  mwili  mzima  katika   hali   ya  usafi.

Hakika    ili  tuwe  nadhifu   tunahitaji   nguo  nyingi   zitakazotuwezesha   kuwa   nadhifu   kila  siku.   Tukinunua  nguo   za  bei  nafuu   tunaweza  kupata   nyingi   na  kuonekana  nadhifu  siku  zote.

Hatuna   budi    kukumbuka  kuwa   unadhifu   haushii  tu  katika  manufaa    ya  kuwavutia  watu  wanaokutazama  bali   hata  kwako  wewe  mwenyewe.  Kadri    unavyojishughulisha    kujiweka  katika  ya  unadhafu  ndivyo    kadri  unavyojijengea  hali   ya  kujithamini  wewe  mwenyewe.

Unapojithamini    wewe  mwenyewe  ndipo  na  watu  wengine     wanapokuthamini.  Kwa   hakika  unapojifikiria  kuwa  wewe  ni  duni  na  mtu  wa  hali  ya  chini   utaonekana   vivyo  hivyo  kwa  watu  na   utajipunguzia  nafasi  ya  kuthaminiwa.

Kulikuwa  na  kijana  mmoja   ambaye   hakusoma   shule  lakini     hakupenda  kabisa  watu wajue    hakusoma.     Hivyo   alikuwa   akijiweka   kalamu  mbili  hadi  tatu  kwenye  mfuko  wa  shati  lake.    Alipotembea  katika  mkono    mmoja  alishika  gazeti     na  upande  mwingine   alibeba   mkoba   wa  mkononi.

Siku  moja   aliingia   posta  kumsalimu    rafiki  yake  anayefanya   kazi  hapo.   Alipoingia  tu  alikutana   na  mzee  mmoja   kutoka  mtaani  kwao  aliyemuomba   amjazie  fomu.

Kijana  aliona  huo  ni  mtihani   mkubwa  ambao   ungefichua   siri  yake.   Lakini   alifikiri  haraka  akaweza  kuvuka  mtihani   huo,   alimwambia  mzee  ana  haraka  ana  kisha    akachukuwa  kalamu  moja  katika  mfuko   wa  shati  akampatia  mzee  na kumuomba   atafute  mtu   amjazie  fomu  yake. 

Kila   ninapoikumbuka   hadithi    hii   huzidi   kuamini  kuwa   mtu  anaweza   kujitengenezea  yeye   mwenyewe   hadhi   anayoipenda  na  kuwafanya  watu  wamthamini.    Hata  hivyo,  pamoja  na  kuwa  nadhifu   bado  kuna  mambo  mengine   ambayo  mtu   anapaswa   kufanya  ili  watu   wakuthamini  kikamilifu.   Watu  wanakuthamini kikamilifu  iwapo   utaishi   nao  kwa  maelewano  ushirikiano staha  na  adabu.     Huna   budi  kuwatendea  matendo   mema  uwe  mwaminifu   na  mvumilivu.

Uepuke   maneno  ya  karaha,  jeuri  wala  usiwe   na  choyo,  chuki  na   hasira  pamoja  na  yote  ni  lazima   wewe   pia   uwathamini.

Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika.  

MAKALA HII IMEANDIKWA NA ABEID SAKARA (Dar es salaam)





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.