google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 12, 2016

Mambo Muhimu Ambayo Hutakiwi Kuyapoteza Kwenye Maisha Yako.

No comments :
Katika safari ya mafanikio, kuna mambo ya msingi sana ambayo unatakiwa kuyalinda ili uweze kufanikiwa. Ikiwa utakuwa unaishi kiholela na kuyapoteza mambo hayo iwe kwa kujua au kutokujua ni wazi utashindwa kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kwenye maisha yako.
Je,  wewe binafsi ulishawahi kujiuliza ni mambo gani unayotakiwa kuyalinda kama mboni ya jicho lako ili yaweze kukusaidia kufaniwa? Kama hujawahi kujiuliza hivyo, tambua yapo mambo unayotakiwa kuyalinda sana ili yakusaidie kufanikiwa.
Bila kupoteza muda fuatana nami hatua kwa hatua katika makala haya ili kuweza kujifunza mambo muhimu ambayo hutakiwi kuyapoteza kwenye maisha yako kabisa.  
1. Hutakiwi kupoteza mwelekeo.
Ili uweze kuishi maisha ya mafanikio ni lazima uwe na mwelekeo maalumu. Ni lazima ujue wapi unatoka na wapi unakwenda. Kujua mwelekeo wako sahihi ni jambo la muhimu sana katika safari ya mafanikio yako.
Watu wengi huwa ni watu wa kupoteza mwelekeo wa maisha yao hata kwa mambo madogo. Kwa mfano, wapo ambao hupoteza mwelekeo wao kwa sababu ya kukosolewa, kushindwa sana au changamoto nyingine za maisha.

Ongeza ushirikiano na wengine ili ufanikiwe.
Kwa bahati mbaya, kila unapokosa mwelekeo kumbuka huwezi kukua kimafanikio na hakuna makubwa utakayoweza kufanya. Kukosa mwelekeo ni moja jambo muhimu sana la kimafanikio unalolipoteza kwenye maisha yako.
2. Hutakiwa kupoteza ushirikiano na wengine.
Mafanikio uliyonayo yanatokana pia na mchango wa wengine. Sasa ili ufanikiwe hiyo inamaanisha mchango wa wengine kwenye maisha yako ni muhimu sana.
Kama unaishi peke yako bila ushirikiano mkubwa na wengine sio rahisi sana kufika mbali kimafanikio. Unaweza kweli ukapata mafanikio lakini hayawezi kuwa makubwa sana kama ungekuwa na ushirikiano na wengine.
Hivyo, kati ya kitu ambacho hutakiwi kukipoteza kwenye maisha yako ni ule ushirikiano mkubwa na wengine. Kila inapoitwa leo jitahidi sana kujenga mahusiano bora na wengine ili ya kusaidie kujenga mafanikio makubwa.
3. Hutakiwi kupoteza kujitawala mwenyewe.
Kati ya kosa kubwa ambalo hutakiwi kulifanya kwenye maisha yako ni kule kupoteza au kushindwa kujitawala. Kwa vyovyote vile ni lazima ujue namna ya kujitawala wewe mwenyewe iwe uweze kufanikiwa.
Kwa mfano unatakiwa kutawala matumizi ya muda wako, pesa, tabia na wakati mwingine hata kutawala nidhamu binafsi. Haya ni mambo ya msingi sana kuweza kuyatawala ili kujihakikishia ushindi wa mafanikio.
Kwa wengi wanaoshindwa kujitawala, hujikuta maisha yamewatawala na matokeo yake huishia kuwa na maisha mabovu sana. Jenga msingi wako wa mafanikio kwa kuhakikisha ni lazima umeweza kujitawala.
4. Hutakiwi kupoteza matumaini.
Zipo changamoto nyingi sana ambazo tunakutana nazo kwenye maisha karibu kila siku. Kuna wakati changamoto hizo hupelekea sisi kukata tamaa kwa yale mambo ambayo tunayoyafanya.
Inapofika wakati ukakata tamaa kwa sababu ya changamoto hapo unakuwa upo kwenye wakati mgumu sana wa kutoka hapo. Kitu ambacho unatakiwa uzingatie, changamoto isiwe kizuizi kikubwa cha kukufanya ushindwe kufanikiwa.
Na wala usije ukakata tamaa kwa sababu ya changamoto yoyote ile. Kila wakati unatakiwa kuwa na tumaini la mafanikio yako, hata wakati unapoona mambo yako yamekuwa magumu na hayawezekani.
Kumbuka kama tulivyojifunza ni marufuku kupoteza mwelekeo, ushirikiano, kujitawala na ni marufuku kupoteza matumaini. Hayo ni mambo ambayo hutakiwi kuyapoteza hata kidogo bali unatakiwa uyalinde na kuyakumbatia kila wakati ili uweze kufanikiwa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Napenda pia kuchukua fursa hii kukukaribisha kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja na kwa ukaribu zaidi. Kujiunga tuma neno MAFANIKIO YANGU, kisha ikifuatia na namba yako kwenda 0713 04 80 35 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,







No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.