google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 20, 2016

Mfumo Unaotengeneza Maisha Yako.

No comments :
Upo mfumo unaotengeneza maisha yako na kuyafanya yawe hivyo kama yalivyo. Hapo ulipo upo hivyo kimaisha si kwa bahati mbaya, mkosi au laana kama ambavyo unajifikiria kila wakati, bali upo hivyo ni kwa sababu ya mfumo.
Kwa  bahati mbaya au nzuri mfumo huu mara nyingi unautengeneza wewe iwe kwa kujua au kutokujua. Habari njema kubwa kwako ni kwamba, kwa vyovyote vile iwavyo, mfumo huo unao uwezo wa kuutawala hata kama umejitengenezea mfumo mbovu.
Mfumo huu ambao ninauzungumzia hapa na ambao unatengeneza maisha yako upo kwenye mawazo yako. Mawazo yako ni kila kitu ikiwa utajua namna ya kuyatawala na kuyatumia vizuri ili yakupe mafanikio.
Tatizo kubwa la sasa ni kwamba, ulimwengu umejazwa na watu wengi ambao hawajui jinsi ya  kutawala mawazo yao. Kwa sababu hiyo hujikuta ni watu wa kuishi tu kwa kupoteza muda bila ya kuwa na mafanikio makubwa.

Kila wakati fikiria kile unachokitaka kwenye maisha yako.
Na kitendo cha kutokutawala mawazo yao kinasababishwa na watu wengi kushindwa kuelewa kile kinachoweza kutawala maisha yao. Nikiwa na maana ule mfumo ambao unaweza ukatawala maisha ya mtu.
Mfumo huu unaotengeneza maisha yako umefundishwa tokea miaka mingi sana na umefundishwa pia karibu  na dini zote. Kwa mfano tukisoma bibilia mithali 23;07 inatuambia “maana aonavyo mtu nafsini mwake, ndivyo alivyo…”
Andiko hilo linatuthibitishia na kutuonyesha kwamba mfumo unaoendesha maisha ya binadamu upo kwanza kwenye mawazo yake. Kipi unachokifikiri? Kipi unachoendelea kukiwaza kila wakati hicho ndicho kinaunda maisha yako.
Wanasaikolojia pia wanatufundisha kwamba kila mtu ana kitu anachokiwaza au kile anachokiweka akilini kwa muda mrefu.  Kitu hicho ambacho kinakuwa kipo akilini au picha ambazo unaziweka ndizo zinazo tengeneza maisha yako.
Ukichunguza utaelewa hicho kinachozungumzwa kipo na tunakiishi. Hiyo ikiwa na maana mfumo unaoendesha maisha ya mwanadamu upo kwenye kile anachokifikira kia wakati. Hakuna ubishi juu ya hili, ushahidi upo karibu kila kona.
Kwa mfano tunaona, watu maskini wanaendelea kuwa maskini zaidi kwa sababu ya mawazo au picha zile wanazoziweka kwenye akili zao. Kila wanachokiwaza au kikiona ni umaskini na mwisho wa siku huushia kuupata huo umaskini.
Pia watu matajiri wanaendelea kuwa matajii zaidi, lakini hiyo yote inatokana na kile wanachokiwaza kwa muda mrefu. Watu hawa kila wakati huwaza mafanikio, hivyo kwa sababu hiyo huvuta mafanikio na utajiri maishani mwao.
Kama kila wakati unaona umaskini, ni wazi utakuwa maskini. Kama kila wakati unawaza utajiri na kuweka picha za utajirii nalo hilo utalifanikisha bila shida yoyote. Mfumo unaotengeneza maisha yako yawe ya kushindwa au mafanikio haudanganyi, unakupa kile unachokizingatia akilini mwako.
Kwa kuwa mfumo huu upo, kila mmoja wetu anatakiwa kujua namna ya kujifunza kutumia na katawala mawazo yake kwa ufasaha ili yaweze kumpa mafanikio makubwa.
Lakini ikiwa endapo utaacha mawazo yako yakutawale, hutaweza kufanikiwa zaidi utabaki na utaendelea kuishi maisha ya kuwasindikiza wengine kwenye maisha na utashangaa huoni mafanikio yoyote yale.
Ili sasa uanze kuufaidi mfumo unaoutengeneza maisha yako na ukafikia mafanikio makubwa kama wengine, kila wakati unatakiwa kuwaza kile unachokitaka. Acha kuwaza na kinyume unachokitaka.
Jaza picha za kule unakokwenda. Jaza picha za kile unachotaka kukifanikisha. Jaza picha za kiwango cha pesa unachokitaka mwaka huu. Ukifanya hivyo kila wakati huku ukichukua hatua za utendaji UTAFANIKIWA.
Kwa kifupi hivyo, ndivyo ambavyo mfumo unaotengeneza maisha yako jinsi unavyofanya kazi. Kumbuka kila wakati hakuna bahati, muujiza wala mkosi katika maisha bali upo mfumo unaotengeneza maisha yako.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Napenda pia kuchukua fursa hii kukukaribisha wewe rafiki yangu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja na kwa ukaribu zaidi. Kujiunga tuma neno MAFANIKIO YANGU, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 04 80 35 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.