google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 4, 2016

Siri Kubwa Ya Mafanikio Yako Ndio Hii.

No comments :
Maisha ni muunganiko wa mambo mengi sana, yapo yale mambo ambayo hujenga na ambayo hayajengi. Mambo hayo ya kukujenga wewe katika ulimwengu huu yapo machache sana, lakini mambo ambayo hayakujengi haya yapo mengi sana.

Kwa kutokujua hili na hapo ndipo ambapo wengi huangukia. Na katika mambo hayo ni yale ambayo ni ya kukutatisha tamaa mara zote. Lakini kwa kuwa wewe ni mpiginaji wa kimaisha siku ya leo nataka nikwambie ya kwamba siri kubwa ya mafanikio yako ni ipo kwenye kubadili ratiba ya utendaji wako wa kazi.

Siri kubwa ya kuweza kufanikiwa ni kuweza kubadili namna ya utendaji kazi wako. Unashindwa kufanikiwa kwa kiwango cha juu kwa sababu umeshazoea kuishi kimazoea. Watu wengi tumelelewa katika maisha ya kimazoea.

Tunaishi maisha yaleyale  ambayo tumekwisha yazoea kiasi kwamba hatuwezi kufanya vitu vingine, lakini kama ambavyo nimezoea kusema ya kwamba maisha hubadilika yenyewe kama endapo utaamua leo kubadili namna ya utendaji kazi wako.

Badili utendaji wako wa kazi.

 Kunielewa vizuri katika hili ninalosema nitakupa  kisa ambacho kilimkuta rafiki yangu wa karibu sana.

Yupo rafiki yangu mmoja  alinipigia simu siku moja na kuniambia ya kwanza biashara yake imekuwa ngumu sana, na kila malengo ambayo hupanga huwa hafikii, hivyo alipenda nimshauri jinsi ya kuweza kufikia malengo yake.

Nikaamuliza huwa unafungua na kufunga biashara yako saa ngapi? ndipo akanijibu ya kwamba huwa anafungua saa mbili asubuhi na kufunga biashara yake mida ya saa mbili usiku.

Hapo ndipo nikagundua ya kwamba alishazoea kufanya biashara kimazoea, ndipo nilipomwambia ya kwamba abadili muda wa kufungua biashara na pia aongeze muda  kufunga biashara yake.

Nikamwambia afanye tathimini kwa muda wa miezi miwili kisha anipe majibu, baada ya miezi miwili kupita akanitafuta tena akanipa tathimini ya kwamba ananishukuru kwani ushauri wangu umemsaidia sana. Ndipo nikamwambia aendelee kufanya hivyo.

Nimekupa ushuhuda huu, ili uweze kukujenga na pia uweze kutafakari juu ya utendaji wako wa kazi. Siku zote siri kubwa ya mafanikio ya mtu binafsi upo katika kuheshimu matumizi sahihi ya muda.

Ni lazima ujue ya kwamba mtunza muda ni wewe hivyo ni vyema ukazingatia ile kauli ambayo husema ya kwamba muda ni mali. Pia uweze kujijengea ile tabia ya kuwa kwanza kuamka na pia mtu wa mwisho kulala.

Hata hivyo ni vyema ukautumia vyema muda ambao unao kuweza kufanya vitu vya msingi ambavyo vitakufanya kila siku uweze kutimiza lile kusudio lako la kuja hapa dunia.

Fanya muunganisho wa kile ambacho unakifamu na kukiweka katika matendo, hapa maana yangu ni kwamba kwa kila jambo ambalo unajifunza kupitia makala mbalimbali ziweke katika matendo, kwani endapo utafanya kinyume chake itakuwa ni bure.

Mwisho niweke nukata kwa kusema ya kwamba hakuna mtu atakayezuia mafanikio yako usipokuwa wewe mwenyewe.

Na: Afisa mipango Benson Chonya.


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.