google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 11, 2016

Aina 5 Za Mafanikio Ambazo Ni Muhimu Kuzifahamu Na Kuziishi.

No comments :
Hongera sana kwa kuchukua uamuzi huu kuweza kusoma makala haya. Kimsingi ni kwamba siri kubwa ya mafanikio yako ambayo unayahitaji ipo katika maandishi, unashangaa! Usishangae huo ndio ukweli.

Kila kitu ambacho unataka katika dunia ya leo kipo katika maandishi, ndiyo maana mwanzoni nimesema hongera kwa kuchukua uamuzi huu ambao umeufanya katika kusoma makala hii.

Hivyo nakusihi uendelee kusoma makala haya mwanzo mpaka mwisho naamini utajifunza kitu ambacho kitakusaidia sana siku ya leo endapo utaamua kuchukua hatua kwa kile ambacho utajifunza katika safu hii.


Ukweli ambao hautaji mifano kutoka kwa wazungu, ni kwamba mwanadamu yeyote ambaye anahitaji kufikia kilele cha mafanikio yake anahitaji aina kumi za mafanikio ile kwa kuanza, nitaeleza aina tano tu.

Nimeamua kuleta maada hii kwa sababu wengi huamini ya kwamba kuwa na pesa ndio kufikia ndoto zao, lakini ukweli halisi haupo hivyo. Kwa msingi huo, leo nitakuongeza kitu katika kujua ukweli wa aina nyingine za mafanikio ambao mwanadamu yeyote yule ni lazima azifahamu.

Zifuatazo ndizo aina tano (5) za mafanikio ambazo ni lazima uziishi;

1. Mafanikio ya kiroho.

Haya ni mafanikio nambari moja kwa mwanadamu, watu wengi huwa wanasahanu ya kwamba mwanadamu yeyote yule ni lazima awe na malengo ya kiroho ili kukamilisha aina hii ya mafanikio. Watu wengi wamekuwa hawana ukaribu na aina hii ya mafanikio kwa sababu ambazo mimi ziwezi kuzielezea ila wao watakuwa wanafahamu kwa undani zaidi.

Na endapo utafanya uchunguzi katika kundi fulani la watu juu ya malengo yao ni asilimia chache sana ambao watakwambia kuhusu malengo yao hasa katika upande wa masuala ya kidini na kumuweka mwenyezi Mungu mbele, wengi tumekuwa tukiishi kama vile tumejiumba wenyewe. 

Ni muhimu pia kujenga mafanikio ya kiroho.
Ewe usomaye makala haya Maisha yako yanahitaji uwepo wa aina hii ya mafanikio ambao utakuweka karibu baina yako na Mungu. Kwani kuwepo na ukaribu na mahusiano bora baina ya mtu na Mungu humfanya mtu aweze kufikia ndoto zake.

Hivyo kama ufanyavyo katika kupanga malengo mengine ya mafanikio yako, vivyo hivyo ni lazima upange malengo yako juu ya aina hii ya mafanikio ya kiroho, hapa haijalishi itakadi yeyote ya kidini uliyonayo ila anachotakiwa ni kuamini ya kwamba Mungu ana nafasi kubwa sana katika maisha yako. 

Mwingine anaweza akaniuliza afisa mipango labda nawezaje kufikia aina hii ya mafanikio? Laa! Usipate tabu unachotakiwa kufanya ni; katika utaratibu wa mzunguko wa dunia katika kulizunguka jua kuna masaa 24 katika mzunguko huo kwa siku.

Sasa ili uweze kufanikiwa katika aina hii ya mafanikio ni lazima uyatenge masaa ya kumuomba Mungu. Lakini wengi tupo vizuri katika kumuomba mwenyezi Mungu pasipo kushukuru, lakinu nikwambie kuwa siri kubwa ya kupewa ipo katika kushukuru pia. 


Hivyo basi kama ufanyavyo katika suala la kutenga masaa  kumuomba Mungu, pia fanya hivyo hata katika kutenga muda kwa ajili ya kumshukuru Mungu . Pia yakumbuke yale maneno matumu yenye hamasa ambayo yanasema ombeni bila kuchoka, lakini na mimi naongezea ya kwamba shukuruni bila kukoma. 

Wakati huo pasipo kumung'unya maneno, wala kukuna kichwa huna budi kuhudhurua kwenye nyumba za ibada kila wakati, makongamano ya kidini na kama ulivyo na ukaribu na simu yako kuliko kitu kingine kile.

Mazingira hayohayo yajenge pia katika vitabu vya kidini. Kufanya hivyo kutakufanya uwe na dira na mwanga mpya kila mara na hatimaye kufikia aina nyingine za mafanikio zilizosalia.  

2. Mafanikio ya mahusiano.

Aina ya pili ambayo unatakiwa kuwa nayo ni aina ya mahusiano baina yako na watu wengine. Hakuna siri ambayo ipo katika maisha haya kama hautakuwaa na mahusiano bora na watu wengine.

Je unajua wewe ni daraja la mtu mwingine kuweza kufanikiwa, kama haujui basi nikwambie ya kwamba bila wewe kuna mtu hawezi kufanikiwa, kama wewe ambavyo unamtegemea mtu fulani ili uweze kukufikisha lengo fulani wapo baadhi ya watu ambao wanakutegemea sana watu.

Kuwa na mahusiano bora na watu wengine ni mbinu bora ya kupata taarifa, taarifa ambazo zitakufanya uweze kufika kule unapopataka. Hii ni aina muhimu sana ya mafanikio ambayo ni lazima unahitajika uwe nayo bila kuikosa.


Je, ni aina zipi nyingine za mafanikio unatakiwa kuendelea kuwa nazo, usikose kusoma wiki ijayo siku kama hii mwendelezo wa makala haya, ili ujue aina nyingine za mafanikio ambazo unatakiwa kuwa nazo katika ulimwengu huu.

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi, endelea kujifunza  kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

Napenda pia kuchukua fursa hii kukukaribisha kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja na kwa ukaribu zaidi. Kujiunga tuma neno MAFANIKIO YANGU, kisha ikifutia na namba yako kwenda 0713 04 80 35 ili uanganishwe.

TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.

Ni wako Afisa mipango,

BENSON CHONYA,
dirayamafanikio.blogspot.com  

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.