google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 7, 2016

Zijue Sifa Hizi Kwa Hakikisho La Mafanikio Yako.

No comments :
Katika tafiti ambazo zimewahi kufanyika katika chuo fulani nchini marekani, waligundua ya kwamba kuna tabia za watu ambazo huwa zinafanana. Tabia hizo ni zile za kimafanikio, lakini zipo tabia ambazo hazifanani kwa watu hao hao tena. Lakini katika tabia za watu ambao wamefanikiwa idadi na takwimu wa mfanano huo upo kwa asilimia ndogo sana. 

Na kuwepo kwa asilimia ndogo hizo zinatengeneza orodha ndogo sana za watu wenye mafanikio. Kama ndivyo hivyo ili kuongezaka kwa idadi ya watu wenye mafanikio hatuna budi kujifunza kwa watu ambao wamefanikiwa kwa kuangalia wao wana siri gani ambayo imewafanya waweze kufanikiwa? Na suala si kujua tu bali kuweza kuyachukua yale mambo mazuri ambayo wao huyatumia hadi kuwasababisha kuwa katika maisha mazuri.

Unaweza ukajiuliza labda ni kwanini tujifunze kwa watu ambao wamefanikiwa, ili nasi tuweze kufanikiwa? wala usipate tabu maana  majibu ya maswali yako kuhusiana na watu ambao wamefanikiwa tutakwenda kuyaangalia, kwa kuangalia sifa walizonazo ambazo zimewafanya wao weweze kufanikiwa.

Zifuatazo ndizo sifa za watu wenye mafanikio;

a) Watu wenye mafanikio huwa ni watu wenye kiu na shauku ya mabadiliko hususani katika upande wa mafanikio. Pia huwa ni watu ambao kimsingi pamoja na mafanikio ambayo wamekwisha yapata huwa hawaridhiki kwa hali waliyonayo japo tayari wamekwisha fanikiwa, kwani wao huamini ya kwamba mafanikio hayana ukomo.


 b) Hujali sana muda husasani katika masuala ya ufanyaji wa kazi. Pia aina hii ya watu wenye mafanikio hawako tayari  kupoteza muda katika mambo ambayo hayaleti faida. Lakini kubwa kuliko yote katika suala la kujali muda wao huamini ya kwamba mafanikio ni leo, huku wakiendelea nini kifanyike leo na kama watataka kifanyike kesho, huendelea kujihoji  ni kwani kifanyike kesho? Kwa misingi hiyo na wewe mwenzangu huna budi kujitenenezea utaratibu huo ambao utakusaidia kuweza kuwa bora katika maisha yako.

c) Watu wenye mafanikio huugozwa kwa malengo yao ambao wamejiwekea na kuyafuata na si kinyume chake. Msukumo wa utekelezaji wa malengo ndio ambao umewawezesha kufika katika kilele cha mafanikio. Hivyo hata wewe ili uweze kufanikiwa  ni lazima uweze kuishi ndani ya melengo yako ambayo umejipangia. kama utaamua kuishi kinyume na malengo yako mafanikio itakuwa ni ndoto.

d)  Wapo tayari kuwapoteza ndugu, jamaa na marafiki ambao hawana msaada wowote katika mambo ambayo huwa wanayafanya kila siku. Hufanya hivyo kwa sababu idadi kubwa ya watu  katika ulimwengu huu ni wakatishaji wa tamaa wa mambo ya watu wengine, lakini idadi ndogo sana ya watu ndio ambao wanaweza kukusaidia katika mambo yako ya kimafanikio. Hivyo ni vyema ukafanya uchaguzi sahihi kwa kuangalia ni mtu gani ni sahihi. 

Hizo ni baadhi ya sifa chache kati ya nyingi ambazo watu ambao wamefanikiwa na  wamekuwa wakiziishi na kusabibisha wao kuendelea kufanikiwa. Mpaka kufikia hapo sina la ziada na pia nikusihi ya kwamba badili maisha yako kwa kuwa na fikra sahihi.

Ndimi: Afisa mipango Benson Chonya


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.