google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 2, 2016

Namna Bora Ya Kuendelea Kuishi Hata Ukiwa Umekufa.

No comments :
Pamoja na malengo mengi uliyonayo katika miasha yako, lipo kusudi na lengo moja kubwa sana katika maisha ambalo hutakiwi kulisahau kabisa. Lengo hilo ni kufanya maisha ya wengine kuwa ya maana na furaha.
Siku zote katika maisha yako, jitahidi sana kufanya maisha ya wengine kuwa ya maana, bora na furaha kwa sababu yako wewe. Uwezo wa kutekeleza hilo najua unao na hakuna cha kukuzuia.
Kwa chochote kile unachofanya iwe kwa kusema au kwa kutenda, hakikisha unafanya maisha ya wengine kuendelea kuwa bora. Epuka kabisa kuumiza watu katika maisha yako kwa jinsi yoyote ile.
Ifanye dunia iwe na furaha kwa sababu yako wewe, wafanye watu wale wanaokuzunguka wawe pia na furaha na mafanikio kwa sababu yako wewe, ukifanya hivyo unajitengenezea njia bora ya kuishi hata ukiwa umekufa.
Katika maisha kitakachokufanya ukumbukwe siku ukifa si kwa sababu ya pesa ulizonazo au umeishi miaka mingi sana duniani, bali ni kwa namna gani jinsi ulivyogusa maisha ya watu ikiwa ni pamoja na kuwapa furaha.

Unapofanya maisha ya wengine kuwa ya furaha, bora na yenye maana unakuwa unajenga kumbukumbu kubwa sana mioyoni mwao ambayo sio rahisi kusahaulika, na inakuwa ni njia bora kwako ya kuishi mara mbili wakati upo hai na hata ukiwa umekufa.
Naamini unawajua watu vizuri ambao majina yao hayaachwi kutajwa pamoja na kwamba kwa sasa hatunao katika hii dunia. Kilichowafanya wawe hivyo ni kwa sababu ya kufanya maisha ya watu wengine kuwa ya maana na furaha.
Bila shaka tunakubaliana hakuna asiyewajua watu kama Nelson Mandela, Nkwame Nkruma, Samora Machel na wengineo wengi ambao walipigania ukombozi wa nchi zao.
Siri kubwa ya watu hwa kuweza kukumbukwa kama nilivyosema ni ile kufanya maisha ya watu wengine kujengwa katika msingi wa furaha, amani, matumaini na mafanikio makubwa.
Suala la kufanya maisha ya wengine yawe ya furaha na ya maana, lifanye kama kuwa jukumu lako. Anzia hapo ulipo ulipo kufanya maisha ya wengine kuwa na furaha na yenye maana kubwa.
Acha kujiuliza sana utafanikishaje hili au utaanzaje? hutakiwi kuwa na wasiwasi sana kwani ni jambo ambalo halihitaji  pesa, bali ni uamuzi wako wewe mwenyewe wa kuanza.
Yapo mambo ya msingi ambayo unatakiwa uyazingatie ii kufanye maisha ya wengine yawe na maana na furaha. Mambo hayo ni kama haya hapa yafuatayo.
Kwa kile unachokisema, sema kwa maneno ya kutia moyo na sio kuumiza hapo utakuwa umefanya maisha ya wengine yawe ya furaha na maana kubwa sana duniani.
kwa kile unachoandika, jitahidi sana kuandika mambo ambayo yatatoa tumaini na nuru kubwa kwa maisha ya wengine leo na hata miaka mitano, kumi au hata miaka mia moja ijayo.
Kwa mitazamo uliyonayo, hakikisha unakuwa na mitazamo ambayo inakusaidia wewe na wengine kuwajengea faraja na matumaini makubwa ya mafanikio yao.
Pia hata nguvu na juhudi zako za kusaidia jamii ni lazima ziweze kuonekana za maana sana ambazo zinalenga si kukusaidia wewe tu, bali hata na kuwasaidia na wengine kufikia malengo yao.
Kila wakati ishi maisha ya kutoa maana kwa maisha ya watu wengine. Unapoishi maisha ya kutoa maana kwa watu wengine na kuepuka ubinafsi wa kila aina hapo unakuwa unajitengenezea njia ya ukika ya kufikia mafanikio makubwa.
Tunakutakia kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafikio.blogspot.com kila siku.
Napenda pia kukaribisha wewe rafiki yangu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja. Kujiunga tuma neno MAFANIKIO YANGU, kisha ikifutia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe. Hakuna gharama na karibu sana.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.