google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 16, 2017

DIRA YA MAFANIKIO; Ujumbe Wetu Kwako Katika Siku Hii Ya Pasaka.

No comments :
Habari za muda huu mpendwa msomaji wetu wa blog hii ya DIRA YA MAFANIKIO, ni matumaini yetu u mzima na unaendelea vyema na pilikapilika za hapa ili kuhakikisha mkono unaenda kinywani.
Ikiwa leo ni siku ya tarehe 16/04/017, siku hii ni muhimu sana duniani kote kwani ni siku ambayo tunasherehekea sikukuu ya pasaka. Siku hii kwa mujibu wa mandiko katika biblia ni siku ambayo tunaadhimisha kufufuka kwa bwana yetu Yesu kristo.
Kwa kulitambua hilo uongozi mzima wa blog hii, unapenda kuchukua nafasi hii adhimu kuweza kukutakia siku njema katika kusheherekea siku hii, huku tukuzidi kukumbusha siku hii ifanye ni siku ya kumuomba na kumshukuru mwenyezi Mungu kwa uzima na mafanikio ambayo amaekujalia. Usifanye siku hii kama ruksa au sehemu ya kutenda dhambi.

Kwani tumekuwa tukishuhudia baadhi ya watu siku kama hii ya leo, wamekuwa wakieguza kama sehemu ya kuanguka dhambini. Hivyo tunachokudisitiza ni kwamba epuka mambo ambayo yatakufanya uanguke katika mambo ambayo ni chukizo mbele ya Mungu.
Mwisho kabisa tunashukuru kwa namna mmoja ama nyingine kuwa mdau wetu mzuri, katika kufuatilia makala mbalimbali ambazo zimekuwa zikiwekwa katika mahala hapa, ni imani yetu zinakusaidia kwa kiwango kikubwa sana, kwa falsafa yetu inasema Badili maisha yako kwa kuwa na fikra sahihi kwa kila kitu huanza katika fikra.
Endelea kuwa sehemu yetu kwa kusoma makala mbalimbali mahala hapa, nasi tutaendelea kuwa sehemu yako kwa kukuleta elimu zitakazo kusaidia kupata mafanikio zaidi. Pia kwa maoni na ushauri wowote usisite kuwasiliana nasi.
"Tunakutakia pasaka njema na siku njema kwako"
Asante.
Imeandaliwa na uongozi mzima wa blog ya Dira Ya Mafanikio.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.