google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 5, 2017

Jinsi Ambavyo Mazoezi Yanaweza Kukuongezea Afya Ya Mwili Na Akili Yako.

No comments :
Si wengi sana ambao wanaona umuhimu wa mazoezi katika suala zima la kuboresha afya zao. Wengi huyaona mazoezi ni kitu cha kawaida na hawayachukulii katika ule uzito wake.
Kutokana na wengi kuupuza mazoezi hapo ndipo hujikuta wapo katika matatizo mengine ya kiafya ambayo kumbe wangeyaepuka kama wangekuwa ni watu wa mazoezi.
Kwa mtu yeyote anayezingatia mazoezi ni rahisi sana kujenga afya ya mwili na akili, katika maisha yake. Inatokea hivyo kwa sababu, pia uimara wa mwili wako unategemea mazoezi.
Hebu tuangalie ni kwa jinsi gani mazoezi yanaweza kuongeza afya ya mwili na akili yako kwa ujumla?
1. Mazoezi yanakufanya ujiamini.
Kwa mujibu wa tafiti nyingi zinaonyesha kwamba ni kitu cha kawaida sana kwamba mazoezi mara nyingi yanakufanya ujisikie vizuri. Na kwa jinsi unavyojisikia vizuri na kujiamini kunakuwa kunaongezeka ndani mwako.
Waangalie watu wote ambao ni watu wa mazoezi, utawaona ni watu ambao  wa kujiamini sana. Ni mara chache sana kukuta mtu ambaye anafanya mazoezi halafu tena akawa ni mtu wa kutojiamini, wengi wanajiamini.
\
Mazoezi ni afya ya mwili wako.
2. Mazoezi yanaifanya akili yako iwe ya ubunifu.
Hili linaweza kunekana ni jambo la kushangaza kidogo kwako, lakini mazoezi yana uwezo huo wa kuifanya akili yako ikawa na ubunifu wa hali ya juu sana kuliko ambavyo unaweza ukadhani.
Katika moja za tafiti zilizofanyika, zinaonyesha kwa kadri mtu anavyofanya mazoezi, anazalisha seli nyingi sana kwenye ubongo wake, matokeo yake seli hizo huongeza ubunifu. Hutaki kuamini katika hili, anza kufanya mazoezi leo uone.
3. Mazoezi yanaipa akili yako uwezo wa kukabiliana na changamoto.
Mbali na mazoezi kuifanya akili yako ikawa na ubunifu lakini pia, ni ukweli ulio wazi mazoezi yanauwezo wa kuifanya akili yako ikawa na uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto.
Akili yako inakuwa imekaa katika mkao wa kupambana na kila aina ya changamo inayojitokeza. Uwezo huu wa akili kuweza kupambana na changamoto hauji hivi hivi tu bali ni kwa kufanya mazoezi.  
4. Mazoezi yanakupunguzia msongo wa mawazo.
Kila mtu kwa namna fulani anakuwa ana msongo wa mawazo hata kwa kidogo. Kuna ambao msongo wao wa mawazo unatokana na maisha magumu na kuna wengine unatokana na mapenzi.
Haijalishi msongo wako wa mawazo chanzo chake ni nini, lakini dawa kubwa ya kutoka kwenye msongo wa mawazo ni kufanya mazoezi. Wengi wanaofanya mazoezi kwa sehemu hupunguza sana msongo wa mawazo.
5. Mazoezi yanakupa nguvu.
Bila shaka umeshawahi kuliona hili sana na kutambua kwamba kwa wote wanaofanya mazoezi miili yao huonekana ina nguvu sana yaani ikiwa imekakamaa na huku ikiwa shupavu.
Kinachotokea kwenye mwili unapofanya mazoezi hupelekea kukujengea misuli mingi sana ndani yako. Kwa hali hiyo ni lazima mwili wako unaonekana wenye nguvu na afya ya kutosha.
6. Mazoezi yanakufanya ulale usingizi mzuri.
Kwa wale wote wanaofanya mazoezi sana, tatizo la kukosa usingizi huwa si kubwa sana kwao. Hiyo yote ni kwa sababu mara nyingi wanakuwa wamechoka na miili huhitaji kumpumzika.
Ni mara chache sana kukutana na mtu ayefanya mazoezi ya kutosha halafu akawa na tatizo la kukosa usingizi. Hicho ni kitu kigumu sana, ndio maana tunasema mazoezi ni muhimu kwa afya na akili yako pia.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku na washirikishe na wengine pia waweze kujifunza na kupata maarifa bora kabisa.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 628 929 816, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.