google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

May 30, 2015

Haya Ndiyo Mambo Mawili Usipokuwa Nayo Makini Yatakutesa Na Kukusumbua Sana Katika Maisha Yako.

No comments :
Hebu jaribu kufikiria iwapo unaona kwamba maisha yako hayakuendei vema, huku watu wengine unaofahamiana nao, pamoja na majirani zako, maisha yao yakiwaendea vizuri bila shida yoyote ile. Wenzako hao wananunua magari, wanajenga majumba, wanasomesha watoto wao katika shule nzuri na wanaishi maisha mazuri kuliko wewe. Je wewe utawazaje? Utajisikiaje? Utawaonea kijicho ama?
 
Ni kweli kabisa kwamba, kuna wakati ambapo huwa tunataka kuwa na kila kitu, ili kuoekana kuwa na maisha bora pengine hata zaidi ya hao wengine tunaowaona. Lakini swali la msingi hapa tunalopaswa kujiuliza ni kwamba, je, katika hali halisi jambo hili linawezekana?

Kulingana na maoni ya Jo Anne White ambaye ni profesa wa elimu katika chuo kikuu cha Temple nchini marekani, ni kwamba kijicho huonesha ile hali ya mtu kujitazama na kujijali yeye mwenyewe. Ni suala linalohusu namna watu wanavyojihisi kujielekea wao wenyewe na iwapo kweli wanajiamini kuhusu namna walivyo.

Kijicho na wivi ni kama ndugu mapacha. Kwa mfano, unaweza kuona wivu iwapo mwenzi wako wa ndoa hakujali. Vilevile wivu unaweza ukachochewa endapo mwenzako wa karibu atakufanya usijisikie vizuri kwa kutumia maneno ya kuumiza na vitendo pia.


Ikumbukwe pia katika uhusiano wowote ule, kuaminia, kutamaniana na kuheshimiana kwa dhati ni mambo muhimu katika kufanya uhusiano huo ustawi na kuimarisha mawasiliano yenye nguvu.


Vilevile kama mtu ana picha mbaya na isiyo na nguvu kujihusu, mara nyingi anaweza kuhisi kutishiwa na kuamini kwamba, hana lolote atakaloweza kuchangia katika kumfanya mtu yeyote yule avutiwe naye.

Kwa kawaida, mwanzoni tabia ya wivu inaweza ikaonekana kuwa ni hali fulani ya urafiki, hasa iwapo mtu wako wa karibu atahitaji muda wako mwingi wa kumjali na inaweza pia kuwa ni dalili ya kukosa ukaribu kwenye hisia.

Ni ukweli ulio wazi kwamba, suala la wivu huweza kuibuka pale mtu anapohisi kukosa usalama na kutishiwa, ama kwa kuhofia kupoteza uhusiano wake au kwamba mtu mwingine badala yake anathaminiwa kama yeye ambvyo alikuwa akithaminiwa.

Hata hivyo wivu hauko kwenye uhusiano wa kimapenzi tu, pia upo kwenye mafanikio ndio kitu ninachotaka kuzungumzia hapa kama nilivyoanza makala hii. Kwani, mtu ambaye hana picha kubwa na yenye kujielekea yeye mwenyewe atakuwa ni rahisi kwake kuhisi kwamba watu wengine wanamuonea wivu na kijicho kwa mafanikio yake.


Kulingana na maoni ya Debbie ambaye ni mwandishi wa kitabu kiitwacho Turn off your inner light: Fitness of of body, mind and soul, ni kwamba, wanaume wengi hupatwa na hali ya kijicho kinachohusiana na kujipatia mali, kama vile kazi nzuri, heshima au hadhi fulani,nyumba nzuri, ambapo kwa upande mwingine, wanawake wao huwa ni mwenye kijicho kuhusiana na mwonekano wao ikiwemo sura, watoto na marafiki zao.

Ili kuweza kukabiliana na kijicho katika maisha yetu, mtu anapaswa kutambua uwezo na nguvu zake, kwa maana kwamba anamudu kufanikisha nini, nini malengo yake aliyojiwekea katika maisha yake. Usijilinganishe na mtu au watu wengine, kwa sababu kwa kufanya hivyo ni sawasawa na kuhujumu uwezo wako pekee.

Wahakikishie  watu wengine na wewe mwenyewe kwamba, leo ni siku yako na zamu yako kufanikiwa, na siyo kesho ila fanya hivyo kwa vitendo. Tumia kijicho hicho hicho ulichonacho na kukuchochea uweze kukamilika na kukua. Hapa tunasema kuwa na kijicho cha maendeleo. Jiambie, kuwa kama fulani ameweza , ni wazi kwamba, inawezekana hata kwangu na nitafanya hivyo.

Kama kuna mtu ambaye anapenyeza sumu ili kufanya uone wivu au kijicho katika jambo fulani, basi unalazimika kubadili mada kwenye mazungumzo yenu au kama ni lazima jiondoe machoni pa mtu huyo. Acha kuwa na kijicho ama wivu sana unaokuumiza wa mafanikio yaw engine. Jipange na tafuta mafanikio yako, vinginevyo hayo ndiyo mambo mawili usipokuwa nayo makini yatakutesa na kukusumbua sana katika maisha yako.  

Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza zaidi kila siku.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,

IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.