google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

May 13, 2015

Kama Unafikiri Huna Akili Za Kutosha Kupata Mafanikio Katika Maisha Yako. Hakikisha Unasoma Hapa.

No comments :
Kwa kawaida kila binadamu anapojaribu kufanya shughuli fulani akashindwa hutafuta sababu iliyomfanya ashindwe. Mara nyingine mtu huweza kuhisi kwa mawazo tu kuwa hawezi kufanya shughuli fulani kwa kuwa hana uwezo wa kutosha wa kiakili.
 
Je, wewe huwa unataka kufanya shughuli fulani ya kuendeleza maisha yako lakini ukahisi kuwa huna akili za kutosha kulifanya kwa usahihi hivyo ukaogopa na kuacha kulifanya?

Kama jibu lako ni ndiyo, sihisi uko peke yako. Kuna watu wengi wanaokabiliwa na ugonjwa huu mkubwa ambao ni sumu kubwa ya maendeleo ya binadamu na ambao kila mmoja wetu hana budi kupambana nao. 

Inakadiriwa kuwa karibu watu asilimia 95 huwa wanafikiria kwa viwango mbalimbali kuwa wana upungufu wa akili za kuwawezesha kufanikiwa katika maisha. Watu hawa mara nyingi huweza kujiona ni wanyonge kwa kudhani hawawezi kitu tena katika maisha yao.


Kutokana na hisia hizi potofu za kufikiri kuwa wana upungufu wa akili, kujiona hawawezi ama wanyonge hii huweza kupelekea kudumaza uwezo wao kiakili na kufanya kushindwa kukabiliana na mazingira ya maisha yenye changamoto nyingi.

Lakini mara nyingi huwa wanashangaa wanapowaona watu wengine ambao wana hakika hawana uwezo wa kiakili unaofikia ule wa kwao wanafanya kwa ufanisi shughuli ambazo wao walihisi hawawezi kuzitenda hata kidogo.

 


Ni vyema tukumbuke kuwa kilicho muhimu siyo kiwango gani cha akili ulichonacho bali ni jinsi unavyozitumia akili ulizonazo. Fikra zinazoongoza akili yako ni muhimu zaidi kuliko kiwango cha ubongo wako. Mwanasaikolojia mmoja aliwahi kuulizwa na mzazi, “Je, mwanangu anapaswa kuwa na kiwango gani cha akili ili aweze kuwa mwanasayansi?”

Yule mtaalamu alimjibu mzazi hivi, “ Mtoto wako hahitaji kuwa na akili za kupindukia, wala uwezo maalum wa kukumbuka na wala sio lazima awe mtoto anayepata alama za juu sana masomoni. Haya yote yanasaidia lakini lililo muhimu kuliko yote ni lazima awe na masafa makubwa ya mvuto na upendo wahali ya juu katika sayansi.|”


Katika maisha mtu mwenye imani, matumaini na hisia chanya katika uwezo wake wa kielimu na ambaye ana kiwango cha akili cha IQ 100 ataweza kupata ajira bora, pesa nyingi, maisha mazuri na hadhi ya juu katika jamii kuliko yule mwenye akili kiwango cha IQ 120 na mwenye hisia hasi katika uwezo wake wa akili na hulka ya kukata tamaa.

Nakumbuka mwaka fulani nilikutana na rafiki yangu tuliyesoma naye zamani ambaye alikuwa na akili sana na hata alifaulu vizuri kupindukia katika masomo yake chuo kikuu.

Nilikumbuka alipojiunga na chuo kikuu aliamua kusomea shahada ya biashara kwa azima kuwa baada ya masomo angefanya kazi kwa miaka michache na hatimaye kufungua kampuni ya biashara.

Wakati nilipokutana naye ilikuwa imepita miaka zaidi ya kumi tokea alipomaliza chuo. Nilipomuuliza kama alikuwa ameanza biashara alisikitika na kunieleza kwa unyonge kuwa aliogopa kuingia katika biashara kwa kuwa aligundua uendeshaji wa biashara umebadilika na kuwa mgumu sana.

Hivyo akahisi hana akili ya kutosha kuendesha biashara, kwa ufanisi zaidi. Alitoa mfano wa changamoto alizohisi zilihitaji uwezo mkubwa kuliko aliokuwa nao kama vile kuamua aina ya biashara itakayofaa, jinsi ya kupata wateja, namna ya kupata mitaji kwa mikopo ya benki yenye riba kubwa, makadirio ya faida na kodi ya mapato na vitu vingine kadha wa kadha.


Aliendelea kunieleza kuwa hata hivyo amestaajabu kuwa baadhi ya watu wengine aliosoma nao sekondari ambao alijua hawana akili kama yeye, wameangia katika biashara na wamepata mafanikio makubwa sana. Alisema kuwa wengine ni wale aliosoma nao chuo kikuu lakini hawakuweza kufuzu. 

Ni kitu ambacho hata wewe unaweza ukajiuliza kwanini baadhi ya wasomi hawapati ufanisi katika maisha? Ingawa sio rahisi pia kuamini kuwa baadhi ya wasomi hushindwa kupiga hatua ya kujipambanua katika maisha utafiti ndivyo umethibitisha kuwa huu ni ukweli mtupu.  

Unaweza ukakuta mtu ni msomo mzuri tu kabisa, pengine mwenye ufaulu mzuri alioupata pindi akiwepo darasani. Pamoja na akili zote hizo sio ajabu kumkuta mtu kama huyu akiwa na maisha ambayo hayana maendeleo ya kutosha kulingana na elimu yake, hii yote inatokana na mtu kujiona hana akili za kutosha kuambana na maisha mpaka kufanikiwa.

Ni muhimu sana kwako kufikiria sasa kwa mtazamo chanya zaidi ili kuweza kuachana na hali uliyonayo inayokufanya uweze kujiaminisha mwenyewe kuwa eti huwezi kufikia mafanikio kwa sababu huna akili za kutosha kuweza kufanya hivyo. Kila mtu anauwezo wa kufanya chochote kile akitakacho.

Jifunze na achana kujaza ubongo wako vitu vingi visivyoweza kukusaidia. Tumia ubongo wako kufikiria vitu vitakavyoweza kubadili maisha yako badala ya kuutumia ubongo wako kama ghala ya kuhifadhi mambo mbalimbali. Na muhimu zaidi ni kuweza kuepukana na hisia kuwa huna akili za kukwezesha kupata mafanikio makubwa kaika maisha yako.

Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio, ansante sana kwa kuwa msomaji mzuri wa mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO na karibu sana kujifunza zaidi.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAO YAIMARIKE,  
    
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.