google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 19, 2016

Mambo Matatu Ya Kukusaidia Kujua Biashara Unayotakiwa Kuifanya.

No comments :
Pengine umekuwa ukiwaza, ukifikiri ni kwa namna gani au ufanye biashara ipi itakayokusaidia kukuingizia pesa nyingi na za kutosha. Na wakati mwingine umekuwa ukisumbuka pia kutafuta ushauri ni biashara gani ya kufanya. Hayo naamini ndiyo yamekuwa mawazo yako kwa muda mrefu.
Ikiwa kweli hayo ndiyo yamekuwa mawazo uliyonayo kwa muda sasa, hilo lisikupe shida. Unao uwezo mkubwa wa kujua na kutambua aina gani ya biashara unayotakiwa kuifanya na ikakupa faida. Je, unajua ni mbinu gani utatumia kutambua aina ya biashara unayotakiwa kuifanya?
Hivi Ndivyo unavyoweza Kujua Ni Aina Gani Ya Biashara Ufanye.
1. Biashara uliyoichagua inauwezo wa kutatua tatizo katika jamii?  
Hapa sio suala tu kufanya biashara, je jiulize biashara hiyo ina uwezo wa kutatua matatizo ya watu kwa sehemu kubwa? Kama jibu ni ndiyo basi unaweza ukaifanya biashara hiyo na ikakuletea mafanikio. Lakini kama utajikuta umechagua biashara ambayo haina uwezo wa kutatua matatizo ya watu, hiyo haikufai na utapoteza muda wako kuifanya.

IPENDE BIASHARA YAKO.
2. Je, unaipenda kweli biashara hiyo?
Biashara unayokwenda kuifanya uwe na uhakika itakuchukulia muda wako mwingi sana. Kitu cha kujiuliza wewe binafsi je,ni kweli una mapenzi nayo? Unaipenda na upo tayari kutoa kila kitu ili kufanikiwa. Haijalishi biashara yako inatatua matatizo makubwa vipi kwenye jamii kama huna mapenzi nayo ya dhati ni wazi utaiua na hutafika popote.
3. Je, upo tayari kukabiliana na changamoto?
Acha kutegemea ukaingia kwenye biashara leo na ukapata faida ni kitu ambacho hakiwezekani. Kama ni hivyo na unaona una wazo zuri la biashara yako, jiulize je utakuwa tayari kukabiliana na changamoto zozote zile zitakazojitokeza? Kama unaona uwezo huo unao, basi hakuna pingamizi unaweza ukaanza biashara yako mara moja.
Kwa msingi huo kama unataka kuanzisha biashara unayoamini itakupa faida, hayo ndiyo mambo ya msingi sana kwako kuyazingatia.
Dira ya mafanikio inakutakia mafanikio mema katika biashara yako. Na kumbuka endelea kujifunza kila siku bila kuchoka.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani ngwangwalu,
Kama una maswali, changamoto au unahitaji ushauri wa kibiashara, usisite kuwasiliana nasi kwa:-
Simu; 0713 048 035,
E-mail; dirayamafanikio@gmail.com
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.